Zemu
JF-Expert Member
- Jun 5, 2008
- 518
- 80
Wadau nimevumilia nimechoka, kuna miezi inayofikia minne hali ya ulipwaji wa mishahara hapa SUA si nzuri, mishahara hulipwa tarehe 30, 31, 1, 2 nk, na kila kabla mishahara kulipwa lazima itolewe barua inayoeleza mchakato mchakato, mi ni mtu mdogo sana hapa na sina pa kusemea, ila kuwa kutumia jukwaa hili nipenda kusema JAMANI VIONGOZI MNATUUA, mfano krismas tumekula bila mshahara kisa mchakato, na hata mpaka leo hakuna salary kisa machakato, Je michakato hadi lini? na Je wenzetu wa UD, MZUMBE na vyuo vingine vya umma salary tayari au mko kwenye michakato?