Ndugu zangu mimi nilibahatika kwenda Tanzania mwaka jana, na niliona kwa macho yangu tatizo la foleni. Tatizo kubwa kwa mawazo yangu ni udogo wa barabara, barabara ni nyembamba sana. Tatizo si magari kuna mtu alinidokeza Tanzania nzima magari hayazidi 1.5 million. Hii idadi ni ndogo kuliko magari yaliyopo Houston, Texas zaidi ya 2 million. Mimi kwa sasa naishi hapa Texas na ninakubaliana na hili tatizo kubwa ni barabara nyingi ni ndogo sana. Hapa Texas ninaweza kuendesha kwa speed ya kawaida ya 60 m/hr ambayo ni sawa na 100km/hr lakini hii speed ni kubwa sana kwa Dar. Kwa ufupi magari yanaenda polepole si kwa sababu ya wingi wa magari pekee bali udogo wa barabara, hata kama barabara nyeupe ni vigumu kukimbiza gari kwa sababu magari yanapishana kwa karibu sana na gari moja likisimama mbele linasimamisha watu wote wa nyuma. Tanzania inatakiwa ifanye jitihada ya kupanua barabara na endapo wakijenga barabara mpya ni lazima iwe pana kwa sababu barabara kuwa nyingi haitakuwa solution kama barabara ni ndogo