Tatizo la Panya

Kanyafu Nkanwa

JF-Expert Member
Jul 8, 2010
849
103
Wama Jukwaa naombeni msaada

Panya wamevamia nyumba yangu mwezi wa tano huu. Nimejaribu sana kupambana nao kwa namna zote imeshindikana kabisa. Mwanzoni nilijaribu kuwauwa kwa sumu. Kwa hakika walikufa sana. Nyumba ikawa kimya kabisa. Waliporudi mara hii, sumu hata ukiweka nyama hawaikaribii. Wanapita mbali kabisa. NImejaribu gundi ya panya. Mwanzoni walinasa kadhaa na kufa. Lakini sasa hivi nikiweka njia zao ama hawapita au wanaruka!

Ni tatizo kubwa sana. Nawaomba wajuzi wa kupambana na panya wanisaidie.

Natanguliza shukrani sana
 
Wama Jukwaa naombeni msaada

Panya wamevamia nyumba yangu mwezi wa tano huu. Nimejaribu sana kupambana nao kwa namna zote imeshindikana kabisa. Mwanzoni nilijaribu kuwauwa kwa sumu. Kwa hakika walikufa sana. Nyumba ikawa kimya kabisa. Waliporudi mara hii, sumu hata ukiweka nyama hawaikaribii. Wanapita mbali kabisa. NImejaribu gundi ya panya. Mwanzoni walinasa kadhaa na kufa. Lakini sasa hivi nikiweka njia zao ama hawapita au wanaruka!

Ni tatizo kubwa sana. Nawaomba wajuzi wa kupambana na panya wanisaidie.

Natanguliza shukrani sana

Panya huwa hawahitaji hasira mzee. Uliwachukia ukaamua kuwapa sumu kali ili wafe. Lakini huwa hawafi wote kinamna hiyo.

Kwanza ufahamu kuwa ukitaka kuwacontrol wasije kwako, lazima na majirani zako wafanye hivyo hivyo. vinginevyo ukiwaua ndani ya nyumba yako, wale wa jirani wanachukulia nyumba yako kama hilo ni jimbo huru, wanajimuvuzisha na kuanzisha makao.

Pili ufahamu kuwa panya ana akili kuliko kuku na ana kumbukumbu inayokaa muda wa karibu miezi 6. Na huwa anatilia mashaka kitu chochote kipya kwenye eneo lake. Hivyo ukimwekea mtego mpya leo, anaweza akaushit kwanza mpaka auzoee.

Ukiwapa sumu kali inayoua haraka, si wote watakula ile sumu. Na watakapokufa, waliobaki watakumbuka muda mrefu kuwa hiyo kitu siyo ya kugusa. Ndio maana mtego au sumu za namna hiyo zinafanikiwa mwanzo halafu baadaye hamna kitu.

Dawa inayofaa ni ile inayoua taratibu (chronic poisoning). Leo wanakula, hawafi, kesho wanakula tena hivyo hivyo, baada ya siku kadhaa wanaanza kufa. Na hapo hawawezi kukumbuka chakula gani ndio kimewaua kwa vile wanakula na kuchanganya na vingine. Utawazoa mpaka utafurahia.

Dawa ya namna hiyo inatakiwa iambatane na juhudi zingine kama vile usafi wa jumla, kuziba maeneo wanakofichama, pamoja na ufugaji wa paka. Pia kama unaweza kula (kanyafu nkanwa) nayo inasaidia kuwapunguza (Don't take this seriously, It is just a joke).

Sumu inayoua taratibu, inapatikana katika kitengo cha utafiti wa mapanya (wizara ya kilimo) pale morogoro, njia ya kwenda Mzinga karibu na lango kuu la kuingilia SUA. Wameichanganya kwenye tambi za rangi ambayo ndege hawaipendi kwa hiyo usiwe na wasi wasi kama wewe ni mfugaji.
 
Panya huwa hawahitaji hasira mzee. Uliwachukia ukaamua kuwapa sumu kali ili wafe. Lakini huwa hawafi wote kinamna hiyo.

Kwanza ufahamu kuwa ukitaka kuwacontrol wasije kwako, lazima na majirani zako wafanye hivyo hivyo. vinginevyo ukiwaua ndani ya nyumba yako, wale wa jirani wanachukulia nyumba yako kama hilo ni jimbo huru, wanajimuvuzisha na kuanzisha makao.

Pili ufahamu kuwa panya ana akili kuliko kuku na ana kumbukumbu inayokaa muda wa karibu miezi 6. Na huwa anatilia mashaka kitu chochote kipya kwenye eneo lake. Hivyo ukimwekea mtego mpya leo, anaweza akaushit kwanza mpaka auzoee.

Ukiwapa sumu kali inayoua haraka, si wote watakula ile sumu. Na watakapokufa, waliobaki watakumbuka muda mrefu kuwa hiyo kitu siyo ya kugusa. Ndio maana mtego au sumu za namna hiyo zinafanikiwa mwanzo halafu baadaye hamna kitu.

Dawa inayofaa ni ile inayoua taratibu (chronic poisoning). Leo wanakula, hawafi, kesho wanakula tena hivyo hivyo, baada ya siku kadhaa wanaanza kufa. Na hapo hawawezi kukumbuka chakula gani ndio kimewaua kwa vile wanakula na kuchanganya na vingine. Utawazoa mpaka utafurahia.

Dawa ya namna hiyo inatakiwa iambatane na juhudi zingine kama vile usafi wa jumla, kuziba maeneo wanakofichama, pamoja na ufugaji wa paka. Pia kama unaweza kula (kanyafu nkanwa) nayo inasaidia kuwapunguza (Don't take this seriously, It is just a joke).

Sumu inayoua taratibu, inapatikana katika kitengo cha utafiti wa mapanya (wizara ya kilimo) pale morogoro, njia ya kwenda Mzinga karibu na lango kuu la kuingilia SUA. Wameichanganya kwenye tambi za rangi ambayo ndege hawaipendi kwa hiyo usiwe na wasi wasi kama wewe ni mfugaji.

Dah! Asante sana ndugu yangu kwa maelezo mazuri namna hii. Tatizo hapa ni namna ya kupata hiyo dawa. Sehemu ingine mikoani, kwa mfano huku Dom, siwezi ipata?
Pili, suala la usafi najitahidi sana. Kuziba nyumba nimefanya ila hata sijui wanaingilia wapi?! Majirani kuwapangia maisha ni ngumu, kwani wengine hata toilet zao kuingia siwezi kwa jinsi zilivyo chakaa!
Nadhani nimechagua sehemu siyo kuishi.
 
Dah! Asante sana ndugu yangu kwa maelezo mazuri namna hii. Tatizo hapa ni namna ya kupata hiyo dawa. Sehemu ingine mikoani, kwa mfano huku Dom, siwezi ipata?
Pili, suala la usafi najitahidi sana. Kuziba nyumba nimefanya ila hata sijui wanaingilia wapi?! Majirani kuwapangia maisha ni ngumu, kwani wengine hata toilet zao kuingia siwezi kwa jinsi zilivyo chakaa!
Nadhani nimechagua sehemu siyo kuishi.

Kama una jamaa yeyote aliyeko pale morogoro mjini anaweza kukuchukulia na kukutumia kwa njia ya basi. Dawa haizidi sh 1000 kwa kisachet kimoja. Ukinunua hata viwili vinakutosha. Gharama ya kutuma haizidi 5000 kwa mabasi ya HOOD na ABOOD, mabasi mengine sifahamu. Ni kitu rahisi. Hata mimi nimeishaagiza sana kwa njia ya basi nikaletewa.
 
Kuna pia dawa ya kiteknolojia, ni kifaa kinatoa kelele kubwa sana (yaani kama vile umefunga mashine ya kuranda mbao chumbani kwako) ila binadamu haisikii hii sauti ipo katika frequency (masafa) wanayosikia panya (rodents), so kwao ni bonge la kelele. Ulizia madukani mie sikumbuki maduka, ila vipo bongo for sure.
 
Dawa pekee ni kufuga Paka na kuweka mazingira safi na kuziba mianya yote inayotumiwa na panya kujificha na kuingia ndani.
 
Kwa uharaka nakushauri ununue vidonge aina ya Indocid caps (za binadamu)na uchanganye unga wake na chakula kingine kama vile dagaa, unga wa mahindi, samaki nk. Hakikisha kauna maji karibu na vyakula hivyo kwani dawa hii humkausha utumbo panya, process ambayo huleta kiu kali kwake. Akinywa maji tu amepona, na akikosa maji ndo kiama chake.
 
Kwa uharaka nakushauri ununue vidonge aina ya Indocid caps (za binadamu)na uchanganye unga wake na chakula kingine kama vile dagaa, unga wa mahindi, samaki nk. Hakikisha kauna maji karibu na vyakula hivyo kwani dawa hii humkausha utumbo panya, process ambayo huleta kiu kali kwake. Akinywa maji tu amepona, na akikosa maji ndo kiama chake.
...Kwa nini asijaribu Valiums angalau atakuta wamelala fofofo then unawamalizia tu na makwenzi ya vichwani.....Ugumu waweza kuwa kugundua walipolalia...
 
Kuna pia dawa ya kiteknolojia, ni kifaa kinatoa kelele kubwa sana (yaani kama vile umefunga mashine ya kuranda mbao chumbani kwako) ila binadamu haisikii hii sauti ipo katika frequency (masafa) wanayosikia panya (rodents), so kwao ni bonge la kelele. Ulizia madukani mie sikumbuki maduka, ila vipo bongo for sure.

Unaweza kutusaidia jina la hiki kifaa mkuu?, maana ukitaka kuuliza uwe angalau na jina.
Shukrani.
 
Back
Top Bottom