Tatizo la Nishati ni janga la taifa!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,605
8,744
Tatizo la Nishati Tanzania sio tatizo la mgao pekee bali ni janga la taifa. Hatuwezi kuwa ma maendeleo kwenye nchi yetu bila kutatua tatizo la nishati.
Raisi wa Nchi anatakiwa kukaa na wahusika wote spika, wasomi, consulting companies, wawakilishi wa nchi zinazotusaidia kama Japan and Norway na kuangalia mikataba, upatikanaji na vitu vyote vinavyohusu tatizo la nishati. Vilevile waje na solution ambazo si za kisiasa bali za kusaidia janga hili la taifa. Vyama vya upinzania vilevile vinatakiwa kuhusika kwenye hili.
 
Wewe nyamazaa!! Unatakatukafanye hivyo hala MAFISADI wao wakale wapi??

Kwani huna habari kwamba ktindamimba cha taifa letu Tanzannia anaitwa UFISADI CHAKACHUA na ni lazima sote tukashirikiane kumdekeza anenepe afurahi???? Na unaposema hivyo wale waliotuchangia fedha kwa ajili ya kununulia madaraka mara kwa mara kwetu na kuthibitishia ulimwengu wote kwamba 'CCM USHINDI NI LAZIMA' utawalipa wewe????

Ukae ukijua ya kwamba leseni tulizowapa wachangiaji wetu ili waje wakaagize nazo Mijenereta kwa kusamehewa kodi bado hazijatumika mpaka sasa na ndio maana kila siku tunatafuta KA-KIPENYO ili wakamwage mali mtaani.

Mali zenyewe zimeshafika ziko kwenye meli pale kwenye mali ukanda wa kimataifa wanasubiri na gharama zinaendelea kupanda tu. Kama isingelikua haka Ka-Slaa na chama chake cha CHADEMA na hivi sasa nao CUF wanaanza kubadilika, tungekua tumeshamaliza mchezo siku nyingi tu mbona.

Lakini kubwa zaidi ujue mwenye dau kubwa zaidi, Rostam Azizi na Edward Lowasa, hivi sasa wanadai chao na MPENDE MSIPENDE ongezeko la asilimia 18 % mtalipa tu. Mnaanza kuleta utani wa ajabu ajabu tu hapa na kuchezea kula za watu, hhaaa!!!
 
Nishati ni kichaka cha upigaji sehemu kubwa ya dunia, hii sekta ni ngumu sana kwa sababu ya ukubwa wa thamani yake na maslahi binafsi.
 
Back
Top Bottom