Paddy
JF-Expert Member
- Sep 22, 2010
- 462
- 304
Mwandosya: Tatizo la maji Dar kuwa historia
TUESDAY, 15 MARCH 2011 19:45 NEWSROOM
NA MWANDISHI WETU
TATIZO la maji Dar es Salaam litakuwa historia ndani ya kipindi cha miaka minne baada ya serikali kuidhinisha kuanza kwa mradi mkubwa wa kitaifa utakaogharimu sh. bilioni 654, imeelezwa. Mradi huo ulioidhinishwa rasmi na serikali juzi kuwa Mradi wa Kitaifa wa Maji Dar es Salaam, utahusisha ukarabati wa mitambo, utafutaji vyanzo vingine vya maji, utandazaji mabomba mapya, ujenzi wa mitambo ya kusafisha majitaka na ulipaji wa fidia kwa watakoathirika. Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya, alisema hayo jana ofisini kwake wakatialipozungumza na waandishi wa habari, kuhusu Wiki ya Maji inayoanza leo nchini kote.
Profesa Mwandosya alisema katika jitihada za kutatua kero ya maji kwa wakazi wa Dar es Salaam na katika kutekeleza ahadi za Rais Jakaya Kikwete kufanya tatizo la maji kuwa historia kabla hajaondoka madarakani, utelekezaji wa mradi huo umeanza na umeidhinishwa rasmi.
Jambo la kufurahisha kwa wakazi wa Dar es Salaam ni kuwa serikali jana (juzi) imeidhinisha rasmi Mradi wa Kitaifa wa Maji Dar es Salaam, ambao utaondoa tatizo kubwa linalowakabili wananchi kwa sasa, alisema Profesa Mwandosya.
Alifafanua kuwa katika mradi huo mkubwa, utahusisha kuongeza vyanzo vya maji ambavyo havijawahi kuongezwa kwa zaidi ya miaka 35 na kuwa asilimia 80 ya fedha za mradi huo zitatolewa na serikali na zilizobaki zitachangiwa na washirika wa maendeleo.
Kutokana na hali hiyo, serikali itatoa sh. bilioni 526 na washirika wa maendeleo watatoa sh. bilioni 128.
Kuhusu kuongeza vyanzo vya maji, Profesa Mwandosya alisema vitachimbwa visima virefu vya hadi mita 500 huko Kimbiji na Mpera, ambavyo vitakuwa na uwezo wa kutoa lita milioni 10 kwa siku.
Jingine ni ujenzi wa bwawa la Kidunda kwa ajili ya kuhifadhi maji ya Mto Ruvu ili yaweze kutumika wakati wa ukame ambapo usanifu wake utakamilika Juni, mwaka huu.
Profesa Mwandosya alitaja hatua nyingine kuwa ni upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu ambao kwa sasa mhandisi anatafutwa kwa lengo la kuongeza uzalishaji kutoka lita milioni 82 hadi milioni 142 kwa siku na kujenga bomba kubwa kutoka Ruvu hadi Kimara Jaribu na Ubungo.
Aliongeza bomba hilo litasaidia kusambaza maji kwa watu wanaoishi maeneo ya milimani kama vile Segerea, Kinyerezi, Kisukuru na kwingineko.
Kuhusu upanuzi wa mtambo wa Ruvu Chini, Mwandosya alisema mradi huo unatekelezwa kwa msaada wa serikali ya Marekani, lengo likiwa kuupanua kutoka utoaji wa maji lita milioni 182 hadi lita milioni 272 na kuwa tayari kampuni kutoka Ufaransa imepewa kazi hiyo.
Mradi huo utahusisha kupitishwa kwa bomba jipya kubwa kutoka Ruvu Chini hadi kwenye matanki yaliyopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, hivyo kusambaza katika maeneo mengine.
Lingine litakalofanyika katika mradi huo mbali ya kulipa fidia ni ujenzi wa vituo vipya vya kusafisha majitaka vitakavyojengwa katika maeneo ya Msimbazi, Mbezi Beach na Kurasani na kuwa vituo hivyo vitatumia teknolojia ya kisasa ambayo haihitaji maeneo makubwa.
Profesa Mwandosya alisema mradi huo unaanza sasa na unatarajiwa kukamilika Desemba 2013.
Mei, mwaka jana, Rais Kikwete alifanya ziara ya mkoa wa Dar es Salaam ambapo alieleza nia yake ya kutaka kuona tatizo la maji linamalizwa Dar es Salaam ifikapo mwishoni mwa uongozi wake.
Rais Kikwete alirudia ahadi yake hiyo wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu Oktoba 28, 2010 alipotembelea mkoa wa Dar es Salaam ambapo alisema anataka kuona baada ya kipindi kifupi, tatizo la maji Dar linakuwa historia.
TUESDAY, 15 MARCH 2011 19:45 NEWSROOM
NA MWANDISHI WETU
TATIZO la maji Dar es Salaam litakuwa historia ndani ya kipindi cha miaka minne baada ya serikali kuidhinisha kuanza kwa mradi mkubwa wa kitaifa utakaogharimu sh. bilioni 654, imeelezwa. Mradi huo ulioidhinishwa rasmi na serikali juzi kuwa Mradi wa Kitaifa wa Maji Dar es Salaam, utahusisha ukarabati wa mitambo, utafutaji vyanzo vingine vya maji, utandazaji mabomba mapya, ujenzi wa mitambo ya kusafisha majitaka na ulipaji wa fidia kwa watakoathirika. Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya, alisema hayo jana ofisini kwake wakatialipozungumza na waandishi wa habari, kuhusu Wiki ya Maji inayoanza leo nchini kote.
Profesa Mwandosya alisema katika jitihada za kutatua kero ya maji kwa wakazi wa Dar es Salaam na katika kutekeleza ahadi za Rais Jakaya Kikwete kufanya tatizo la maji kuwa historia kabla hajaondoka madarakani, utelekezaji wa mradi huo umeanza na umeidhinishwa rasmi.
Jambo la kufurahisha kwa wakazi wa Dar es Salaam ni kuwa serikali jana (juzi) imeidhinisha rasmi Mradi wa Kitaifa wa Maji Dar es Salaam, ambao utaondoa tatizo kubwa linalowakabili wananchi kwa sasa, alisema Profesa Mwandosya.
Alifafanua kuwa katika mradi huo mkubwa, utahusisha kuongeza vyanzo vya maji ambavyo havijawahi kuongezwa kwa zaidi ya miaka 35 na kuwa asilimia 80 ya fedha za mradi huo zitatolewa na serikali na zilizobaki zitachangiwa na washirika wa maendeleo.
Kutokana na hali hiyo, serikali itatoa sh. bilioni 526 na washirika wa maendeleo watatoa sh. bilioni 128.
Kuhusu kuongeza vyanzo vya maji, Profesa Mwandosya alisema vitachimbwa visima virefu vya hadi mita 500 huko Kimbiji na Mpera, ambavyo vitakuwa na uwezo wa kutoa lita milioni 10 kwa siku.
Jingine ni ujenzi wa bwawa la Kidunda kwa ajili ya kuhifadhi maji ya Mto Ruvu ili yaweze kutumika wakati wa ukame ambapo usanifu wake utakamilika Juni, mwaka huu.
Profesa Mwandosya alitaja hatua nyingine kuwa ni upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu ambao kwa sasa mhandisi anatafutwa kwa lengo la kuongeza uzalishaji kutoka lita milioni 82 hadi milioni 142 kwa siku na kujenga bomba kubwa kutoka Ruvu hadi Kimara Jaribu na Ubungo.
Aliongeza bomba hilo litasaidia kusambaza maji kwa watu wanaoishi maeneo ya milimani kama vile Segerea, Kinyerezi, Kisukuru na kwingineko.
Kuhusu upanuzi wa mtambo wa Ruvu Chini, Mwandosya alisema mradi huo unatekelezwa kwa msaada wa serikali ya Marekani, lengo likiwa kuupanua kutoka utoaji wa maji lita milioni 182 hadi lita milioni 272 na kuwa tayari kampuni kutoka Ufaransa imepewa kazi hiyo.
Mradi huo utahusisha kupitishwa kwa bomba jipya kubwa kutoka Ruvu Chini hadi kwenye matanki yaliyopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, hivyo kusambaza katika maeneo mengine.
Lingine litakalofanyika katika mradi huo mbali ya kulipa fidia ni ujenzi wa vituo vipya vya kusafisha majitaka vitakavyojengwa katika maeneo ya Msimbazi, Mbezi Beach na Kurasani na kuwa vituo hivyo vitatumia teknolojia ya kisasa ambayo haihitaji maeneo makubwa.
Profesa Mwandosya alisema mradi huo unaanza sasa na unatarajiwa kukamilika Desemba 2013.
Mei, mwaka jana, Rais Kikwete alifanya ziara ya mkoa wa Dar es Salaam ambapo alieleza nia yake ya kutaka kuona tatizo la maji linamalizwa Dar es Salaam ifikapo mwishoni mwa uongozi wake.
Rais Kikwete alirudia ahadi yake hiyo wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu Oktoba 28, 2010 alipotembelea mkoa wa Dar es Salaam ambapo alisema anataka kuona baada ya kipindi kifupi, tatizo la maji Dar linakuwa historia.