Mwl Ngasa
Member
- Aug 9, 2012
- 32
- 7
Kupenda kila mtu anaruhusiwa, lakini baada ya kupenda unachukua tahadhari gani? watoto wengi kuanzia miaka 14...... wanajikuta wanatumbukia kwenye ngono ambazo hazina kibali hivyo kufanya maisha yao ya shule kuwa hatarini hii ni kwa sababu tu eti sisi utamaduni wetu hauruhusu familia au jamii kuzungumzia mambo ya mapenzi! Walimu nao badala ya kuwapa nasaha watoto nao ndo kwanza wanavkandamiza sasa msichana mdogo tu keshatembea na wanaume wenye umri wa baba yake hivi hii nini sasa? ukiuliza eti watoto wamekosa maadili hivi mtoto alielala na mtu mzima ni nani aliekosa maadili? watoto hawajapewa maadili na maadili si kuwakataza tu waambiwe wazi kwa nini na badala yake wafanye nini kuepuka!