Tatizo la kuongezeka vibaka.

Mlachake

JF-Expert Member
Oct 13, 2009
4,412
4,559
Hivi karibuni kumekua na ongezeko kubwa sana la vibaka! Tukianzia wanaokwapua laptops maeneo ambao tulishaonywa hapa Jf mpaka wale wanakwapua Simu Maeneo ya Tandale kwa mtogole.
Hivi hamna tiba ya huu ugonjwa?
Tujue kwamba huu ugonjwa huwa unaongezeka kila ukipita msamaha wa rais kwa wafungwa wenye kesi ndogo ndogo.
Hapa iringa kuna sehemu moja ni maarafu sana kwa hao vibaka. Maeneo ya Takrima Lodge kuelekea Holiday. Kila m2 analijua hilo. Cha kushangaza Kuna patrol inayofanywa na Askari usiku wakitumia gari aina ya Landrover lakini sijawahi kusikia hata siku moja hawa vibaka wamekamatwa!!
Hivi hawa vibaka watatutesa mpaka lini?
Sidhani kama Tunamhitaji Augustine Lytonga Mrema na Ubunifu wake wa sungusungu! Nafikiri waliopo Kwenye kitengo hicho wana uwezo wa kuja na Mbinu Mpya!!
Chonde chonde IGP MWEMA. VIBAKA WANATUMALIZA!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom