Tatizo la kula/kutafuna kucha

View attachment 387667

Hiki kitu kina waathirika wengi sana wake kwa waume wakubwa kwa wadogo. Tunaweza kudhani tu kuwa ni tabia mbaya au mazoea! La hasha kutafuna kucha za vidole vya mikononi ni tatizo la kisaikolojia linalomla mtu ndani kwa ndani kwenye ufahamu wake ambapo hupelekea viashiria hivi:-

-woga
-mawazo/msongo wa mawazo
-kutojiamini
-fadhaa/sononi
-kukosa la kufanya
-taharuki
-mapepe/restless mind
-hulka ya kuiga

Hivyo ni viashiria vikuu vya mtafuna kucha na hili jambo hufanya bila kupenda ni involuntary action. Kuna baadhi hufanya wakiwa pekeyao kwenye upweke na wengine hufanya pindi anapokutana na mtu kwa mara ya kwanza ama hadhira.

View attachment 387681

Kwakuwa hili ni tatizo la kisaikolojia zaidi basi hata tiba yake ni ya kisaikolojia, hasa hasa

-councelling/ushauri nasaha
-kumjengea uwezo wa kujiamini mwathirika
-kutafiti kupitia yeye mwenyewe chanzo cha tatizo lake hilo na muda

Wengine hukutana na hii hali katika hatua fulani ya makuzi na ikipita tatizo hujitibu lenyewe!

Je una tatizo kama hili ama ndugu yako? Ama rafiki? Usikimbilie kwa mganga wa kienyeji utaambiwa una jini njaa..! Tiba unayo mwenye
Mshana jr, vipi unatoa tiba mkuu, kuna dogo langu yani huwa nampiga mingumi ila hasikii, huyu ni mgonjwa type gani chronic ama?
 
Kucha tamu sana..cjui solution ya kuacha ni nini..!! Lakn mie hupendelea kuitafuna kucha moja tu
1472153288800.jpg

Tuko weng aisee nataman niache naweza jizuia kwa muda ila naenda narudia tena

Mamaaaa me ndo addicted miakA mi nne sasa
Hili tatizo haitofautiani sana na kujichua....kwahiyo ni lazima na ni muhimu ukubali wewe mwenyewe kubadilika yani ujiwekee nadhiri
 
Mshana jr, vipi unatoa tiba mkuu, kuna dogo langu yani huwa nampiga mingumi ila hasikii, huyu ni mgonjwa type gani chronic ama?
Ana umri gani? Uwe unazichovya kwenye mafuta taa ni tiba nzuri pia kwa wenye kucha zinazokatikakatika
 
Et ni sawa na kujichua..haha wee jamaa
Trust me najua hiki ninachokiandika, unadhani watu wanapenda punyeto? Wengine wana familia kabisa lakini ile kitu huja bila taarifa na baada ya kitendo hubaki na fadhaa kubwa na kujiapiza kutorudia tena...haitofautiani sana na kula kucha
 
17 years-old, dogo kamaliza kucha zimebaki nyama tu
Paka mafuta ya taa kila wakati hamu itatoweka lakini pia angalia asije akawa na tatizo kubwa la kisaikolojia hasa kukosa kujiamini na kujistukia, muweke busy pia jitahidi kumchanganya na makundi ya watu wanaofanya vitu vyenye kushughulisha akili
 
Hebu tupate maarifa zaidi kwa msaada wa mtandao
1. Kuna hawa ambao si wala kucha ila hupenda kuzikata chini sana
1472154801900.jpg

2. Kuna hawa ambao ndio muktadha wa mada wala kucha
1472154842675.jpg

3. Kitunguu saumu kinatajwa kama tiba kwa kupaka kwenye kucha...maajabu ya tiba ya kitunguu saumu yanazidi kuwa mengi
 
Hebu tupate maarifa zaidi kwa msaada wa mtandao
1. Kuna hawa ambao si wala kucha ila hupenda kuzikata chini sanaView attachment 387769
2. Kuna hawa ambao ndio muktadha wa mada wala kuchaView attachment 387770
3. Kitunguu saumu kinatajwa kama tiba kwa kupaka kwenye kucha...maajabu ya tiba ya kitunguu saumu yanazidi kuwa mengi
1472154955223.jpg
japo concept ni kuzuia muwasho na fungus lakini harufu yake huwa kero kwa mtafunaji na kujikuta automatically anaacha
 
  • Thanks
Reactions: MC7
teh teh wengine wanakula mpaka za miguu nimemkuta mtu ameinama anang'ata za miguu anadai ni tamu halaf duuuh wengine bhana
 
Sijawahi, hata kukata kucha tu sipendi

Kama kweli hujawai kukata ata kucha dadangu ww ni kituko...niliwai zamia kitchen party moja nikakuta wanamfunda dada jinsi ya kujiswafi maeneo yenu.....shart moja awe na kucha fupi...sasa ww mwenzangu sjui.....nimesema ila sio kwa ubaya
 
Kuna rafki angu akijihisi yuko mwenyewe anakula kamasi nishamuona mara nyingi ila nakausha.sijui ni ugonjwa gani huu me nahisi labda ana upungufu wa madini chumvi mwilini au kisaikojia
 
Kama kweli hujawai kukata ata kucha dadangu ww ni kituko...niliwai zamia kitchen party moja nikakuta wanamfunda dada jinsi ya kujiswafi maeneo yenu.....shart moja awe na kucha fupi...sasa ww mwenzangu sjui.....nimesema ila sio kwa ubaya
Hujaelewa nilichoandika....
Sijawahi kula kucha, pia kukata kata kucha huwa sipendi, haya Sema tena hoja yako
 
Kuna rafki angu akijihisi yuko mwenyewe anakula kamasi nishamuona mara nyingi ila nakausha.sijui ni ugonjwa gani huu me nahisi labda ana upungufu wa madini chumvi mwilini au kisaikojia
ni kwenye mlolongo huo huo wa kula kucha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom