Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Friday, 28 October 2011 19:38 |
Chanzo MWANANCHI Esther Mwimbula, Kilosa SERIKALI imeombwa kuwakamata na kuwaondoa wawekezaji waliovamia mashamba mbalimbali wilayani Kilosa, mkoani Morogoro, ambao wamebadili matumizi na kukodishia wananchi wengine ambao siyo wakazi wa wilaya hiyo. OfisaTarafa ya Magole, Conradi Mzwalandili, alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, alipotembelea tarafa hiyo kuwa wilaya hiyo ina mashamba makubwa yenye ardhi yenye rutuba kwa kilimo cha mazao mbalimbali. Hata hivyo, Mzwalandili alisema wawekezaji hao wamewakodishia watu wengine na kuwafanya wakazi wa wilaya hiyo kukosa eneo la kuishi, hali inayowafanya kukumbwa na njaa mara kwa mara. Mzwalandili alisema wilaya hiyo ina maeneo yenye rutuba, lakini wakazi wake wana tatizo la ukosefu wa ardhi kwa ajili ya kuendesha kilimo baada ya maeneo makubwa kupewa watu wachache wanaojidai wawekezaji, ambao hawaitumii kama kulingana na walivyoomba. Alisema imefikia wakati wakulima na wafugaji kutengewa maeneo yao ili kuzuia migogoro isiyo ya lazima wilayani humo.Alisema licha ya wakulima kulima maeneo yao, ruzuku ya pembejeo haziwafikii wakulima kwa wakati hivyo kusababisha kuchelewesha maandalizi ya mashamba. Mzwalandili aliendelea kuwa kiasi ambacho wamepangiwa wakulima kutoa ili wapate ruzuku za pembejeo, ni kubwa tofauti na kipato cha wakulima hao.Hivyo aliomba Serikali kupunguza kiwango cha ruzuku za pembejeo na kuwaondoa wawekezaji waliovamia mashamba kwa maslahi binafsi. |