Taswira Mbalimbali Za Mikutano Ya Mwenyekiti Wa Chadema Freeman Mbowe Na Godbless Lema

Kiganyi

JF-Expert Member
Apr 30, 2012
1,242
765
Pix-5.jpg

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akiwasili kwenye Uwanja wa Kwa Mbombe katika kijiji cha Madizini, Kata ya Mtibwa mkoani Morogoro ambako alihutubia mkutano wa hadhara wa Opereshi Sangara juzi.
DSC05147%5B5%5D.jpg

Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kabla ya Mahakama kutengua Ubunge wake, Mh Godbless Lema amefungua matawi katika Kata ya Daraja Mbili Jijini Arusha juzi August 18,2012.


Katika ziara hiyo, Lema aliambatana na Mbunge wa Arumeru Masariki Mh Joshua Nassari(wa pili kulia) pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM kabla ya kujiengua na kujiunga na Chadema mapema mwezi Aprili mwaka huu, Ndg James Ole Millya, ambao nao kwa nyakati tofauti walipata fursa ya kuzunumza.

Mbali na suala la uzinduzi na upokeaji wanachama wapya, Lema alifanya harambee ya kukusanya fedha kusaidia shughuli za chama hicho katika Kata hiyo ambapo jumla ya Sh 219,500 zilichangwa na wananchi.

Akiondoka eneo hilo, Lema alilazimika kuwatuliza mamia ya watu waliokuwa wanafuatilia msafara wake ili kuepusha kutokea mwanya kwa watu wenye nia mbaya kuleta vurugu na uharibifu wa mali. Baadae msafara wake ulikatiza mitaa ya Stand Kuu ya mabasi makubwa na kisha kuelekea bustani ya City Park huku njiani akishangiliwa sana na baadhi ya watu wakinyoosha vidole kama ishara ya ushindi.
DSC05146%5B5%5D.jpg

Wanachama wapya aliojiunga na chadema wakigombania kadi za chama hicho
DSC05126%5B5%5D.jpg

Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kabla ya Mahakama kutengua Ubunge wake, Mh Godbless Lema akiunguruma kwenye uzindusi wa matawi katika Kata ya Daraja Mbili Jijini Arusha juzi August 18,2012.
Pix-6.jpg

Jitihada za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) za kuwafikia wanachi ili kunadi sera zake, hususan katika mikutano inayoendelea katika mkoa wa Morogoro, zilikumbana na vikwazo mbali mbali katika baadhi ya maeneo, kama inavyoonyesha pichani, mtaro uliochimbwa katika barabara ya kuingia kijiji cha Namgezi kitongoji cha Kambi ya Keya jimbo la Ulanga Mashariki, kwa lengo la kuzuia magari yasipite.Picha na Joseph Senga​

 
Dah ... napata matumaini makubwa sana kwa kizazi kijacho cha watanzania .. hii kazi inayofanywa na CDM ni nguvu ya mungu
 
kwa kweli hao viongozi wa ccm na serikali waliowatuma watu kuchimba mtaro magari yasipite hawakuwatendea haki kwani wamewachosha bure na bado mkutano ukafanyika. M4C haizuiliki!
 
kwa kweli hao viongozi wa ccm na serikali waliowatuma watu kuchimba mtaro magari yasipite hawakuwatendea haki kwani wamewachosha bure na bado mkutano ukafanyika. M4C haizuiliki!

Jamaa wanatumia mikakati ya Vyama vya KIKOMONST, hii mikakati ilitumiwa miaka ya 50 sasa nashangaa CCM kuitumia mida hii,
 
Safiii,safi sanaaaa
Mchakamchaka mpaka magamba wakimbie nchi hii.

Naona mwitikio mkubwa sana wa akina mama huko morogoro, hii ni dalili njema sana kwamba ukombozi wa nchi yetu umekaribia sana.

Mungu ibariki Chadema na harakati zake.
 
Pix-5.jpg

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akiwasili kwenye Uwanja wa Kwa Mbombe katika kijiji cha Madizini, Kata ya Mtibwa mkoani Morogoro ambako alihutubia mkutano wa hadhara wa Opereshi Sangara juzi.
DSC05147%5B5%5D.jpg

Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kabla ya Mahakama kutengua Ubunge wake, Mh Godbless Lema amefungua matawi katika Kata ya Daraja Mbili Jijini Arusha juzi August 18,2012.


Katika ziara hiyo, Lema aliambatana na Mbunge wa Arumeru Masariki Mh Joshua Nassari(wa pili kulia) pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM kabla ya kujiengua na kujiunga na Chadema mapema mwezi Aprili mwaka huu, Ndg James Ole Millya, ambao nao kwa nyakati tofauti walipata fursa ya kuzunumza.

Mbali na suala la uzinduzi na upokeaji wanachama wapya, Lema alifanya harambee ya kukusanya fedha kusaidia shughuli za chama hicho katika Kata hiyo ambapo jumla ya Sh 219,500 zilichangwa na wananchi.

Akiondoka eneo hilo, Lema alilazimika kuwatuliza mamia ya watu waliokuwa wanafuatilia msafara wake ili kuepusha kutokea mwanya kwa watu wenye nia mbaya kuleta vurugu na uharibifu wa mali. Baadae msafara wake ulikatiza mitaa ya Stand Kuu ya mabasi makubwa na kisha kuelekea bustani ya City Park huku njiani akishangiliwa sana na baadhi ya watu wakinyoosha vidole kama ishara ya ushindi.
DSC05146%5B5%5D.jpg

Wanachama wapya aliojiunga na chadema wakigombania kadi za chama hicho
DSC05126%5B5%5D.jpg

Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kabla ya Mahakama kutengua Ubunge wake, Mh Godbless Lema akiunguruma kwenye uzindusi wa matawi katika Kata ya Daraja Mbili Jijini Arusha juzi August 18,2012.
Pix-6.jpg

Jitihada za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) za kuwafikia wanachi ili kunadi sera zake, hususan katika mikutano inayoendelea katika mkoa wa Morogoro, zilikumbana na vikwazo mbali mbali katika baadhi ya maeneo, kama inavyoonyesha pichani, mtaro uliochimbwa katika barabara ya kuingia kijiji cha Namgezi kitongoji cha Kambi ya Keya jimbo la Ulanga Mashariki, kwa lengo la kuzuia magari yasipite.Picha na Joseph Senga​

Na huku kwenye mitandao watachimba mitaro? Kweli CCM imekwisha kabisa. Ni afadhali hata wangekaa tu kimywa huku wakitazama wenye nguvu wakichukua madaraka. Kwa kuifanyia CDM hivi hata kipofu ataondoka CCM. Madhara ni makubwa sana kwa CCM kuliko hata CDM. Mungu ibariki CDM. Wasaidie viongozi wake watukomboe watanzania tumeteseka ya kutosha.
 
Nimeipenda hiyo picha waliochimba mtaro, ukiona wameanza kucheza rafu za aina hii ujue game umeshawashinda
 
Nimeipenda hiyo picha waliochimba mtaro, ukiona wameanza kucheza rafu za aina hii ujue game umeshawashinda

Kweli ccm imewaumiza watu c kiuchumi tu bali kiakili,sasa nn significance ya kuharibu miundombinu kuzuia tu M4C?kesho washindwe kupitisha mama mjamzito kumwahisha hospital kisa waliharibu barabara
 
Back
Top Bottom