Tarehe ya maandamano ya Tanzania nzima

Mtaka Haki

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
492
149
Mimi ni miongoni mwa watu ambao wanahimiza amani na kuihubiri.
Vilevile ni muumini mzuri wa utawala wa sheria na haki kama njia ya kuidumisha amani hiyo.
KATIKA MAMBO YANAYOIFANYA NCHI IWE YA AMANI NI UTAWALA WA SHERIA NA MATENDO YA HAKI KUTOKA KWA VYOMBO VYA UTAWALA.

Bunge letu lililopita lilisaidia kuwepo kwa uvumilivu wa watanzania dhidi ya udhalimu uonevu na ufisadi. Matarajio yalikuwa kuwa haki itaonekana.
Kila mmoja aliamini kuwa hatua madhubuti zitachukuliwa dhidi ya maonevu mbalimbali mbali.

Bunge la sasa limeanza kwa dhihaka, vijembe na hata mambo yanayofanana na umbeya. Wengine wameenda mbali na wamesema ni bunge la kimbeya na ndicho CCM ilichokuwa ikitafuta kwa kusisitiza gender wakati huu badala ya sifa.
Sikubaliani na hao waliofika huko kwenye kujibu dhihaka kwa dhihaka.
Wako wanawake wengi serious na pia wako wanaume wengi wambeya.
Bunge letu, serikali yetu, chama tawala vimepoteza matumaini ya watanzania kuwa ufisadi utakemewa pia kuondolewa, na hatimaye haki itafuatwa.
Utawala thabiti wa demokrasia na wa haki ndio ambao watanzania wanaulilia.
Watu wamekata tamaa hata katika kupiga kura kwani hawaamini kuwa haki itatendeka.

SASA KAMA HAKUNA MATUMAINI KWA WATUNGA SHERIA NA KAMA HAKUNA MATUMAINI KWA UONGOZI WA SERIKALI NINI KIFANYIKE?
Njia pekee inayobakia ni maandamano ya kuukataa udhalimu. Mimi ninaunga mkono maandamano ya kudai haki. Na hivi karibuni nitakuwa nikiyasema kwa nguvu na uwazi kwa njia mbalimbali.

NAOMBA MAPENDEKEZO YA TAREHE ZA MAANDAMANO NA ENEO LA KUKUSANYIKA KILA MKOA: VINGINEVYO CCM WATUPE TAREHE ZA KUCHUKUA HATUA ZA KUONDOA UDHALIMU NA KUSHUGHULIKIA KERO. Tunajua hapajawahi kutokea utawala mkamilifu au usio na madoa labda ule ujao wa Yesu Kristo kama wanavyoamini wakristo, lakini angalau utawala uonyeshe kujali raia na kukemea maovu yaliyo wazi.
 
Maandamano nchi nzima ndio yameanza mkoa mpaka mkoa, wilaya kwa wilaya, jimbo kwa jimbo. mwisho tukijumlisha itakuwa imekidhi nchi zima!
 
Maandamano nchi nzima ndio yameanza mkoa mpaka mkoa, wilaya kwa wilaya, jimbo kwa jimbo. mwisho tukijumlisha itakuwa imekidhi nchi zima!

HAYA NINAYOULIZIA HAPA NI KAMA YA MISRI NA TUNISIA. Yale ya nchi nzima ambayo watu hawaondoki mpaka waone mabadiliko.
 
Kwa hali ilivyo...ni chini ya miezi mitatu yatavuma nchini mwetu. Ni iwapo tu organisers kama CDM hawatokengeuka, maana kwa msimu huu WANAKUBALIKA NA KUUZIKA KIRAHISI hivyo kuwawia rahisi.
 
Maandamano nchi nzima ndio yameanza mkoa mpaka mkoa, wilaya kwa wilaya, jimbo kwa jimbo. mwisho tukijumlisha itakuwa imekidhi nchi zima!
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
<br />
maandanano ambayo mwisho wa cku wa2 wanarudi makwao? , Waandamanaji wake squre chadema wawalishe tuone!!!<br />
<br />
Kuchuzana huku simo!!!
 
maandanano ambayo mwisho wa cku wa2 wanarudi makwao? , Waandamanaji wake squre chadema wawalishe tuone!!!
Kuchuzana huku simo!!!
Kwani kwa kawaida waandamaaji huwa hawarudi nyumbani!?...Mkwere kapewa siku tisa baada ya kuzungukia nchi nzima kama hatofanyiakazi maswala mhimu kama mfumo wa bei..
 
Tujiandae kugoma nchi nzima pale polisi watakapo zuia maandamano sehemu yeyote ambayo cdm watapita na hapa ndio mapinduzi yatanzia
 
mi navyoona source nzuri iwe ktk madai ya wafanyakazi Tucta itoe ultimatum hadi mei mosi kima cha chini 315,000/= pamoja na madai mengine ya msingi ambayo najua serikali yetu kiziwi haitayafanyia kazi so siku ya maandamano ya mei mosi ndo tunaliendeleza hadi kung'oa huu utawala usiojali wananchi wake, na hii itakuwa fursa ya kuwahusisha watu wa vyama vyote kuliko yakiwa organized na cdm kuna watu though wana tabu hawatajitokeza coz wana itikadi tofauti. Cha muhimu ni vyama vya wafanyakazi kuplay their role, na workers unions zimeplay part kubwa sana ktk ukombozi wa wanyonge hata kwa tanganyika ziliplay hyo role , so kuanzia mei mosi tulianzishe
 
Ni kukaba junctions muhimu kila mkoa, kwa Dar ni Mnazi mmoja, Mbeya-Mafiati, Iringa - posta, Dodoma - Nyerere grounds, etc
 
msione kirahisi namna hiyo. Maandamano ni kitu kingine kabisa. Kwa sababu mtakuwa mmejunja katiba ya inchi kwahiyo mkiona wanajeshi wanawafyatulia risasi muone kawaida. Kuigeza inchi tz kuwa kama somalia,kwa sababu mnaweza kuongeza shida zaidi ya tulizonazo,tuanze maandamano halafu gala la siraha lifunguliwe kila mtu awe bunduki yake tuone kama kuna mtu atabaki
 
mi navyoona source nzuri iwe ktk madai ya wafanyakazi Tucta itoe ultimatum hadi mei mosi kima cha chini 315,000/= pamoja na madai mengine ya msingi ambayo najua serikali yetu kiziwi haitayafanyia kazi so siku ya maandamano ya mei mosi ndo tunaliendeleza hadi kung'oa huu utawala usiojali wananchi wake, na hii itakuwa fursa ya kuwahusisha watu wa vyama vyote kuliko yakiwa organized na cdm kuna watu though wana tabu hawatajitokeza coz wana itikadi tofauti. Cha muhimu ni vyama vya wafanyakazi kuplay their role, na workers unions zimeplay part kubwa sana ktk ukombozi wa wanyonge hata kwa tanganyika ziliplay hyo role , so kuanzia mei mosi tulianzishe



Kweli kamanda. Maandamano yatafanikiwa yakiwa organised na at least trade/workers unions. Ila yatafanikiwa zaidi pale waTZ wenyewe (raia wa kawaida) watakapoamua kuingia barabarani na kutaka utawala dhalimu wa CCM uondoke haraka.

CHADEMA wakiandaa sidhani kama yatafanikiwa sana,kwani itakua rahisi kwa serikali kucrack down viongozi wa CHADEMA na kuvunja nguvu ya maandamano. Itakua ngumu kwa serikali kucrack down wananchi wote endapo sisi wananchi ndo tukaokua behind maandamano kutokana na kuguswa na ugumu wa maisha.
 
HAYA NINAYOULIZIA HAPA NI KAMA YA MISRI NA TUNISIA. Yale ya nchi nzima ambayo watu hawaondoki mpaka waone mabadiliko.

Sawa kabisa. Ni vema kuandamana kwa lengo la kuuondoa utawala legelege wa kikwete kulikoni tu kuandamana kwa lengo la kupinga tu jambo hiyo haitasaidia.
 
msione kirahisi namna hiyo. Maandamano ni kitu kingine kabisa. Kwa sababu mtakuwa mmejunja katiba ya inchi kwahiyo mkiona wanajeshi wanawafyatulia risasi muone kawaida. Kuigeza inchi tz kuwa kama somalia,kwa sababu mnaweza kuongeza shida zaidi ya tulizonazo,tuanze maandamano halafu gala la siraha lifunguliwe kila mtu awe bunduki yake tuone kama kuna mtu atabaki
Mkubwa:
Wengi humu ndani ni mazungumzo ya kijiweni tu wala si ya kuyapa kipaumbele. Utawasikia wanasema oooh, naunga mkono, tupo pamoja nk lakini wao wenyewe pengine wamejilipua USA na kwingine hawawezi hata kurudi nchini kwa sababu wamechemsha. Sasa wanataka pa kutoke,, kwamba kuwe na machafuko nchini wapewe hifadhi za kisiasa huko walipo,, utumbo mtupu!
Hizi ni dalili halisi za frustrations. Msitake kuwachuuza watu na raia wema waache kujitafutia riziki eti wakaandamane. Kuna atakayeweza kukaa siku 18 kama wamisri? au mnaongeaongea tu?
 
Mkubwa:
Wengi humu ndani ni mazungumzo ya kijiweni tu wala si ya kuyapa kipaumbele. Utawasikia wanasema oooh, naunga mkono, tupo pamoja nk lakini wao wenyewe pengine wamejilipua USA na kwingine hawawezi hata kurudi nchini kwa sababu wamechemsha. Sasa wanataka pa kutoke,, kwamba kuwe na machafuko nchini wapewe hifadhi za kisiasa huko walipo,, utumbo mtupu!
Hizi ni dalili halisi za frustrations. Msitake kuwachuuza watu na raia wema waache kujitafutia riziki eti wakaandamane. Kuna atakayeweza kukaa siku 18 kama wamisri? au mnaongeaongea tu?


Baloney!
 
Kwa sababu mtakuwa mmevunja katiba ya inchi kwahiyo mkiona wanajeshi wanawafyatulia risasi muone kawaida.


Katiba ya TZ au? Ebu toa ushahidi wapi katiba ya TZ inasema maandamano ni uvunjifu wa sheria!
 
msione kirahisi namna hiyo. Maandamano ni kitu kingine kabisa. Kwa sababu mtakuwa mmejunja katiba ya inchi kwahiyo mkiona wanajeshi wanawafyatulia risasi muone kawaida. Kuigeza inchi tz kuwa kama somalia,kwa sababu mnaweza kuongeza shida zaidi ya tulizonazo,tuanze maandamano halafu gala la siraha lifunguliwe kila mtu awe bunduki yake tuone kama kuna mtu atabaki

Nimeipenda hii! Umeona mbali lazima kupima the outcomes!
 
Jamani tatizo letu wa TZ ni kuwa mlo wa kesho hutegemea leo so mtu kuandamana siku nzima inakuwa ngumu lakini pia hali bado haijawa ngumu kwa watu wote lakini itafika siku watu watu wote watazinduka na ndo utakuwa mwisho wa mafisadi na vibaraka wao. binafsi naona kama tunawachelewesha hawa maduwanzi hebu tulianzisheni kama Libya mbona tunaweza jamani woga wanini?



:spider:
 
Back
Top Bottom