mchemsho
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 3,212
- 867
Kufuatia vuta nikuvute baina ya serikali na madaktari juu ya kuboresha maslahi na mazingira bora ya kufanyia kazi, madaktari waliipa 'ultmutum' serikali kushughulikia madai yao. Ultmutum hiyo iliyoishia jana kwamba kwakuwa madai mengi ya madaktari hayakufanyiwa kazi, na kama kawaida yake Pm Pinda akatumia Jazba badala ya busara kuwajibu madaktari eti serikali haiwezi kushinikizwa kuwafukuza ka waziri na naibu wake, Je kama madaktari wataamua kugoma bila kikomo nini utakuwa wajibu/ jukumu letu kama watanzania wazalendo. Karibuni.