Mpe Mungu utukufu kwa kila jambo maana ana mipango na kila kinachotokea. Alimleta duniani na kamchukua kwa wakati wake. Pole sana mkuu.
Pole sana mtu mmoja.Mungu akutie nguvu katika hiki kipindi kigumu.Mungu ailaze roho ya marehemu mtoto wa mtu mmoja mahali pema peponi,Amen.
mkuu pole sana bwana alileta na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe vumilia katika wakati huu mgumu
Ndugu zangu,
january mwaka huu nilikuja hapa na habari za furaha kuu za kupata mtoto wa kiume (angalia link hiyo hapo chini)
https://www.jamiiforums.com/mahusia...a-kiume-mama-na-mtoto-wanaendelea-vizuri.html
leo hii nina huzuni kuu pia, Mwenyezi Mungu muweza wa yote kamuita mtoto huyo kurejea kwake na kutuacha na majonzi makubwa nisiyoweza kuyaeleza vyema. machozi mengi sana yamenitoka, ila sina la kufanya zaidi.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe
RIP mwanangu mpendwa
poe sana mkuu ndio kazi yake mola haina makosa cha msingi ni kumwomba mwenyezi mungu aipumzishe roho ya marehemu pahala pema peponi na awajalie moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.Pole sana
Pole sana ndugu yangu, Mungu amlaze mahali pema peponi. Amina.
Mh pole sana sana kaka yetu mpendwa mungu akutie nguvu ktk kipind iki kigumu! may his soul rest in eternal peace! amen! pole sana sana kaka! mungu na awatie nguvu leo na daima.
Ndugu yangu pole sana!