Ndugu zangu,
january mwaka huu nilikuja hapa na habari za furaha kuu za kupata mtoto wa kiume (angalia link hiyo hapo chini)
https://www.jamiiforums.com/mahusia...a-kiume-mama-na-mtoto-wanaendelea-vizuri.html
leo hii nina huzuni kuu pia, Mwenyezi Mungu muweza wa yote kamuita mtoto huyo kurejea kwake na kutuacha na majonzi makubwa nisiyoweza kuyaeleza vyema. machozi mengi sana yamenitoka, ila sina la kufanya zaidi.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe
RIP mwanangu mpendwa
january mwaka huu nilikuja hapa na habari za furaha kuu za kupata mtoto wa kiume (angalia link hiyo hapo chini)
https://www.jamiiforums.com/mahusia...a-kiume-mama-na-mtoto-wanaendelea-vizuri.html
Nimepata mtoto wa kiume. Mama na mtoto wanaendelea vizuri
hapa natetemeka kwa furaha, nimeweka muziki wa rose mhando uitwao MUNGU NITAKUSHUKURU. nimejawa na furaha, lakini niko mbali sana nje ya Tanzania, ningependa kuwepo lakini nimesafiri masafa marefu kutafuta maisha lakini mwenzangu kwa ujasiri mwingi kajifungua salama mtoto wa kiume! Glori to God.
nimetafuta kila upande ndugu yangu wa kumshirikisha furaha yangu nimekosa isipokuwa JF members. jamani Mungu ashukuriwe kwa jinsi anavyotujalia waja wake mapaji kwa ukarimu. libarikiwe jina la Bwana wa Mabwana. amen.
nachakarika nirudi mapema nyumbani kumpakata mwanangu... ooo, nimejawa na furaha wapendwa siwezi kusema kwa usahihi
leo hii nina huzuni kuu pia, Mwenyezi Mungu muweza wa yote kamuita mtoto huyo kurejea kwake na kutuacha na majonzi makubwa nisiyoweza kuyaeleza vyema. machozi mengi sana yamenitoka, ila sina la kufanya zaidi.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe
RIP mwanangu mpendwa