Habari za muda huu waungwana?
Nimepokea taarifa asubuhi hii kuwa member wenzetu Madame B na Kijino wamefiwa na baba yao.
Taarifa niliyoipata toka kwa Madame B mwenyewe inafafanua zaidi kuwa Mzee alikuwa anaumwa. Amefariki asubuhi ya leo tarehe 25-10 2012.
Msiba upo Chama, Mbezi Mwisho{Ya Kimara}. Ni njia ya kuelekea Maramba Mawili..
Mipango ya mazishi inaendelea sasa hivi eneo ambalo msiba upo{Chama. Njia ya kwenda Maramba Mawili}
Taarifa zaidi zitaendelea kuwafikia kadri ambavyo itakuwa imepangwa. Wana JF tuungane pamoja katika kipindi hichi kuwafariji wenzetu {Wafiwa} kwa kuwapa Moyo na kuwaombea faraja na nguvu toka kwa Mungu.
Kwa taarifa na maelezo zaidi jinsi ya kufika eneo la tukio{Kwa wale watakaohitaji kwenda msibani} piga namba hii ya 0716394882..
Updates:
Nimepata taarifa muda huu kutoka kwa Madame B kuwa eneo la msiba limebadilishwa. Msiba umehamishiwa nyumbani Kinondoni B Mtaa wa Dunga. Sio kule Mbezi kama ambavyo taarifa ya awali ilieleza... Namna nzuri ya kufika na kupitia njia ya kuelekea Mwananyamala hospital kutokea Kinondoni Biafra.
Tunawaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Pole wangu rafiki najua inaumiza sana najua vile unajisikia zidi kumwomba MUNGU ampe baba rehema ya kuuona uso wake!Asanteni sana,sana tena sana jamii yote ya wana Jf kwa kutufariji ktk kipindi hiki kigumu.
Ila hatutaweza kuupindisha ukweli kuwa Baba yetu Kipenzi hayupo tena nasi hapa Duniani.
Ameondoka wakati bado tunamuhitaji Baba.
Mbele yetu,Nyuma yako,sote tu wapitaji na Kwake Tutarejea.
Nawashukuru woote kwa Kutufariji.
Asanteni sana.
Pole sana Kijino MUNGU awape nguvu kupita hapa salama na wadogo zako.Asanteni kwa kutufariji wanajamii wenzetu, ndio hvyo tumefiwa, na tumebaki yatima, mama yetu alitangulia miaka 4 nyuma, mimi ndio mkubwa, nimebaki na jukumu la kuwalea wadogo zangu, tunaomba muendelee kutufariji