Nicas Mtei
JF-Expert Member
- Dec 21, 2010
- 11,556
- 7,084
Habari za muda huu waungwana?
Nimepokea taarifa asubuhi hii kuwa member wenzetu Madame B na Kijino wamefiwa na baba yao.
Taarifa niliyoipata toka kwa Madame B mwenyewe inafafanua zaidi kuwa Mzee alikuwa anaumwa. Amefariki asubuhi ya leo tarehe 25-10 2012..
Msiba upo Chama, Mbezi Mwisho{Ya Kimara}. Ni njia ya kuelekea Maramba Mawili..
Mipango ya mazishi inaendelea sasa hivi eneo ambalo msiba upo{Chama. Njia ya kwenda Maramba Mawili}
Taarifa zaidi zitaendelea kuwafikia kadri ambavyo itakuwa imepangwa. Wana JF tuungane pamoja katika kipindi hichi kuwafariji wenzetu {Wafiwa} kwa kuwapa Moyo na kuwaombea faraja na nguvu toka kwa Mungu.
Kwa taarifa na maelezo zaidi jinsi ya kufika eneo la tukio {Kwa wale watakaohitaji kwenda msibani} piga namba hii ya 0716394882..
Updates:
Nimepata taarifa muda huu kutoka kwa Madame B kuwa eneo la msiba limebadilishwa. Msiba umehamishiwa nyumbani Kinondoni B Mtaa wa Dunga. Sio kule Mbezi kama ambavyo taarifa ya awali ilieleza... Namna nzuri ya kufika na kupitia njia ya kuelekea Mwananyamala hospital kutokea Kinondoni Biafra.
Tunawaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Updates.
Taarifa ambayo imetolewa mda huu ni kwamba Mwili wa marehemu utasafirishwa Jumapili tarehe 28-10- 2012 . Mwili unasafirishwa kwenda Lushoto.
Taarifa zaidi zitawajia kadri ambavyo zitatokea..
Update
Mda huu ndo shughuli ya kuaga inamalizika. Safari ya kuelekea Lushoto kwa ajili ya mazishi ndo inaanza. Tuwekane kwenye maombi
Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina lake libarikiwe.
Pumzika kwa Amani Mzee George.
Nimepokea taarifa asubuhi hii kuwa member wenzetu Madame B na Kijino wamefiwa na baba yao.
Taarifa niliyoipata toka kwa Madame B mwenyewe inafafanua zaidi kuwa Mzee alikuwa anaumwa. Amefariki asubuhi ya leo tarehe 25-10 2012..
Msiba upo Chama, Mbezi Mwisho{Ya Kimara}. Ni njia ya kuelekea Maramba Mawili..
Mipango ya mazishi inaendelea sasa hivi eneo ambalo msiba upo{Chama. Njia ya kwenda Maramba Mawili}
Taarifa zaidi zitaendelea kuwafikia kadri ambavyo itakuwa imepangwa. Wana JF tuungane pamoja katika kipindi hichi kuwafariji wenzetu {Wafiwa} kwa kuwapa Moyo na kuwaombea faraja na nguvu toka kwa Mungu.
Kwa taarifa na maelezo zaidi jinsi ya kufika eneo la tukio {Kwa wale watakaohitaji kwenda msibani} piga namba hii ya 0716394882..
Updates:
Nimepata taarifa muda huu kutoka kwa Madame B kuwa eneo la msiba limebadilishwa. Msiba umehamishiwa nyumbani Kinondoni B Mtaa wa Dunga. Sio kule Mbezi kama ambavyo taarifa ya awali ilieleza... Namna nzuri ya kufika na kupitia njia ya kuelekea Mwananyamala hospital kutokea Kinondoni Biafra.
Tunawaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Updates.
Taarifa ambayo imetolewa mda huu ni kwamba Mwili wa marehemu utasafirishwa Jumapili tarehe 28-10- 2012 . Mwili unasafirishwa kwenda Lushoto.
Taarifa zaidi zitawajia kadri ambavyo zitatokea..
Update
Mda huu ndo shughuli ya kuaga inamalizika. Safari ya kuelekea Lushoto kwa ajili ya mazishi ndo inaanza. Tuwekane kwenye maombi
Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina lake libarikiwe.
Pumzika kwa Amani Mzee George.