Tanzania yatoa msaada wa tani 300 Somalia

kufuatia njaa iliyokithiri somalia (haijawahi kutokea ndani ya miaka 60) Tanzania imeahidi kuisaidia Somalia tani 300 za mahindi. Huu ni moyo wa utoaji

na hakika likiwa limefanyika kwa moyo basi Mungu ataibariki Tanzania mara dufu.

Lakini kuna jambo moja tuu linanishangaza, hivi ni kweli Tanzania inawapenda watu wake? Leo bungeni nimewasikia wabunge kama watatu

wanalalamika majimboni kwao kuna njaa kali na chakula walichoahidiwa (iwe cha bure/au cha gharama nafuu/gharama halisi) hakijapelekwa zaidi ya

miezi miwili sasa. Huu ndo mwendelezo tabia ya kujali watu wa nje kuliko wazawa? Sipingi kusaidiwa kwa somalia, maana hakika tunapaswa kufanya

hivyo lakini maneno matakatifu yanasema mtu asiyewajali watu wa nyumbani mwake ameikana imani, ni mbaya kuliko asiye amini! Nawasilisha


Kuwajali watuj wa Nje ni kawaida ya JK maana amekuwa waziri wa mambo ya nje muda wote au mmesahau ? Pia kumbuka JK ni mpenda sifa sana mie sishangai kuwapa chakula hicho kama alidiriki kuongopa mchana kweupe kwa ma CCM wenzake tena Darisalama juu ya barabara za juu kwa juu unategemea nini ?
 
Wakati wa njaa huko EThiopia nikiwa std 5 Nyerere alitoa kama USD 1Million na kusifiwa pia na watu wengi ndani na nje. Hivyo siyo miaka 60 kama ulivyosema. Naunga mkono hoja hizo tani ziende ila wasijeteka meli itakayopeleka
 
Wakati wa njaa huko EThiopia nikiwa std 5 Nyerere alitoa kama USD 1Million na kusifiwa pia na watu wengi ndani na nje. Hivyo siyo miaka 60 kama ulivyosema. Naunga mkono hoja hizo tani ziende ila wasijeteka meli itakayopeleka

Siyo miaka sitini ya misaada mkuu. Miaka sitini ya njaa. yaani njaa iliyopo somalia haijawahi kutokea ndani ya miaka sitini iliyopita
 
Kuwajali watuj wa Nje ni kawaida ya JK maana amekuwa waziri wa mambo ya nje muda wote au mmesahau ? Pia kumbuka JK ni mpenda sifa sana mie sishangai kuwapa chakula hicho kama alidiriki kuongopa mchana kweupe kwa ma CCM wenzake tena Darisalama juu ya barabara za juu kwa juu unategemea nini ?
kuwa mpinzani haimaanishi ni kupinga kila kitu hata kama kinakheri kwa wandamu wenzio! wale watu wanahitaji kusaidiwa na kumbuka kutoa ni moyo na wala si utajiri! tatizo la njaa nchini linatokana na baadhi ya watendaji wachache amabao wanashindwa kugawa chakula cha msaada kwa walengwa! hii haiwezi kumzuia mh. rais kutoa kidogo ambacho mwenyezi mungu amemjalia kuvuna!
 
Kwa ile hali iliyopo Somalia, naunga mkono hoja. Nafikiri tuna reserve ya kutosha ya chakula. Si vibaya tuwasaidie hawa wenzetu. Kwa kweli hali yao ni mbaya sana.

Kweli mkuu. Ubinadamu hauna mipaka, kabila, dini, n.k. ila huwa kuna kitu kimoja kinanishangazaga sana. Ishu kama hii ya Somalia nilitegemea mataifa ya kiislamu ndio yangekuwa mstari wa mbele kabisa kuwasaidia waislamu wenzao wa Somalia lakini sikuwahi kusikia siyo Iran, Saudia, Yemen, Quartar, Iraq, n.k. wakiongelea lolote kuhusu Somalia. Badala yake tunasikia makafir wa magharibi ndio wako mbele kwenye hili suala. Kweli baniani mbaya kiatu chake dawa. Hao wa mashariki ya kati pamoja na utajiri wao wa mafuta kazi yao ni kutuletea tende tu na mabaki ya nyama walizojichinjia. Shame upon them.
 
Msaada ni mzuri sana pale ambapo watoto wako nyumbani hawana njaa. "MPENDE MWENZAKO KAMA UNAVYOJIPENDA MWENYEWE" Sasa kama TZ huwezi kuonyesha huruma kwa mikoa yenye njaa, hapo Mungu hawezi kukubaliana na utoaji huo kwani "UMETOA ILI UONEKANE NA WATU/MATAIFA, NA TAYARI UMEONEKANA NA PENGINE UMEPONGEZWA, UNAHITAJI NINI ZAIDI??????"
 
Mi naipongeza serikali kwa kuchukua uamuzi huo.Haiwezekani huko Rukwa mazao yanaoza wakati wenzetu wanakufa kwa njaa!
Kuhusu mikoa yenye njaa hapa TZ ni uzembe wa ma RC na ma DC kuwasadia wakazi wa sehemu hizo.Chakula kipo cha kutosha lkn wao wanashindwa kusimamia usambazaji.

Hata Japan pamoja na matatizo waliyopata bado wanaendelea kutoa misaada kwa nchi maskini.Well done tz gvt!!
 
kama kawaida ya jk

masifa mengiiiii kuliko uwezo

Mnakumbuke kile kisa cha Mwakyembe kudai Kulikuwa na njama za Kuuwawa yeye na Dr.Slaa kutumia Kundi la Al-Shaabab? Hapa hakuna cha kushangaa Msaada kupelekwa Somali na Kuachwa watu wa Igunga ambao tulioneshwa hali zao katika TBC1 moja ya taarifa za habari.JK ameomba msaaada wa Sheikh Sharif Sheik Ahmed amuunganishie mawasiliano na Al-Shaabab Malipo hizo tani 300!!!Haiwezekani Watoto wako hata kama unao wengi kwamba wakifa wachache sio issue eti ndio ukatoe msaada kwa Jirani badala ya Wa kwako?Huyu Jk ankaugonjwa nini kamepunguza akili na uwezo wake wa kufikiri?Sifa nazo huwa na kikomo.Please wakuu,mimi mgeni sana hapa JF,lakini kwa hili naamini hata jamii za kina Faiza Foxy watamshushua bosi wao The Great Gambaz JK.Peleka mzigo huo Simanjiro na Igunga "ukaokoe" jimbo kabla Hatujachukua fasta,maana wenzetu wamesema lolote kudadeki.
 
mbona wilaya ya longido kuna wamasai wanalala njaa lakini hawajasaidiwa hata gunia moja? Wakuu mimi c andiki kiushabiki kama ukitaka nenda longido kwa wamasai mjionee wenyewe. Mvua haijashesha miaka miwili. Kuna njaa sawa na somalia
 
Kweli mkuu. Ubinadamu hauna mipaka, kabila, dini, n.k. ila huwa kuna kitu kimoja kinanishangazaga sana. Ishu kama hii ya Somalia nilitegemea mataifa ya kiislamu ndio yangekuwa mstari wa mbele kabisa kuwasaidia waislamu wenzao wa Somalia lakini sikuwahi kusikia siyo Iran, Saudia, Yemen, Quartar, Iraq, n.k. wakiongelea lolote kuhusu Somalia. Badala yake tunasikia makafir wa magharibi ndio wako mbele kwenye hili suala. Kweli baniani mbaya kiatu chake dawa. Hao wa mashariki ya kati pamoja na utajiri wao wa mafuta kazi yao ni kutuletea tende tu na mabaki ya nyama walizojichinjia. Shame upon them.


Mkuu, mimi sijaona sababu za kuwaona wanaotoa msaada makafiri. Sidhani kama wanaangalia huyu ni mtu wa imani gani ndo wampe msaada.

Binadamu yeyote mwenye utu ataangalia uhitaji wa mtu na sio dini. Kwa sisi ambao mnatuita makafiri tunaamini katika upendo. Biblia inasema

unawezafanya yote hayo lakini kama hauna upendo ni bure. Tunawapenda wote, wanaotupenda na wanaotuita makafiri. Wote tunawaonesha

upendo.
 
Mi naipongeza serikali kwa kuchukua uamuzi huo.Haiwezekani huko Rukwa mazao yanaoza wakati wenzetu wanakufa kwa njaa!
Kuhusu mikoa yenye njaa hapa TZ ni uzembe wa ma RC na ma DC kuwasadia wakazi wa sehemu hizo.Chakula kipo cha kutosha lkn wao wanashindwa kusimamia usambazaji.

Hata Japan pamoja na matatizo waliyopata bado wanaendelea kutoa misaada kwa nchi maskini.Well done tz gvt!!

Then hapa lazima tukubaliane tuna majuha wakutosha hapa. Kama mahindi yanaoza Rukwa halafu igunga na longido wanakufa njaa some one is not

serious at all!
 
Kweli nimeamini JF inasomwa na wakubwa. Juzi nililalamika kuwa sisi 'miafrika' tuna roho ngumu na hatuwezi kusaidia hata kwa kidogo tulichonacho na siku zote twangojea kusaidiwa. Leo naona hii. Hata nilithubutu kusema, Tanzania, Botswana na Zambia zina uwezo kabisa wa kutoa angalau tani 50 za mahindi kila moja kuonesha tu kwamba wana 'care'
Nataraji huyo 'kizito' anayesoma hapa asome na hayo mengine.
 
Waaaii hamna kitu japo. Jizo mi semi 10tuu ambapo ni around 10mn tunauwezo wa kufanya zaidi kwani yanayosepa huko mpakani kinyemela kwenda kenya ni mengi sana
 
Watu wanakufa na njaa tz.hakuna kazi inafanyika kwa sababu umeme hakuna
na kama hakuna umeme unahitaji jeneretai,jenereta utawashia nini????? mafuta hakuna.
Tuna waua ndugu zetu tz kwa makusudi
 
Kuisaidia Somalia ni jambo jema... Lakini hatuna sababu ya kuipongeza hii serikali ya majuha, sababu kelele za kuomba msaada kwa ajili ya somalia zimekuwepo kwa mda mrefu sasa lkn Tz ilikuwa kimya kabisa. Juzi wameona rais wa somalia kaenda Bongo ndo wanajibaraguza eti wanatoa msaada. Walikuwa wanasubiri nini?! Tulitakiwa tuwe kati ya mataifa ya kwanza kuisaidia somalia siyo kusubiri rais wao aje..
BTW mbona ****** hajawatambulisha kwa rais wao wale wasomali wanaoporomosha magorofa hapo Bongo??? Tena wangetaitiwa watoe michango ya nguvu kwa ndugu zao...
 
TANZANIA itatoa msaada wa tani 300 za mahindi kuwasaidia kupunguza makali ya njaa
inayowakabili wananchi milioni 3.5 wa Jamhuri ya Somalia.

Mbali na mahindi, Tanzania pia itatoa misaada mingine kwa nchi hiyo kwa kadri uwezo wa
nchi unavyoruhusu kuisaidia ikabiliane na matatizo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiusalama yanayoikabili kwa miaka 20 sasa.

Rais Jakaya Kikwete alitangaza mchango huo jana wakati wa mazungumzo na mgeni wake Rais wa Somalia, Shehe Sharif Ahmed aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili iliyomalizika jana.

“Tunasikitika kuona matatizo ya ukosefu mkubwa wa chakula yanayoikabili nchi yako. Kama unavyojua Tanzania ni nchi masikini na uwezo wetu siyo mkubwa.

“Lakini tuna methali hapa isemayo kutoa ni moyo siyo utajiri. Kwa hiyo kwa moyo huo wa mtu masikini, tumeamua kutoa mchango wetu mdogo wa tani 300 za mahindi.

“Tutazungumza na kampuni za kutengeneza maji hapa nchini kama nazo zinaweza kuchangia kupambana na janga hili kubwa linalowakabili wananchi wa Somalia,” alisema Rais Kikwete.

Rais Kikwete pia amempongeza Rais wa Somalia na ujumbe wake kwa mafanikio ya
kijeshi dhidi ya kikundi cha kigaidi cha El Shabaab ambacho kimefukuzwa katika maeneo mengi ya Mji Mkuu wa Mogadishu.

Rais pia amempongeza Rais Ahmed kwa mafanikio yake mengine ya kuleta utulivu zaidi ndani ya Serikali yake na kuongeza muda wautumishi wa Serikali na Bunge kama moja ya njia ya kuleta maelewano ndani yaSerikali, na kati ya Serikali na Bunge la nchi hiyo.

HabariLeo | Tanzania yatoa msaada wa tani 300 Somalia
 
TANZANIA itatoa msaada wa tani 300 za mahindi kuwasaidia kupunguza makali ya njaa
inayowakabili wananchi milioni 3.5 wa Jamhuri ya Somalia.

Rais Kikwete pia amempongeza Rais wa Somalia na ujumbe wake kwa mafanikio ya
kijeshi dhidi ya kikundi cha kigaidi cha El Shabaab ambacho kimefukuzwa katika maeneo mengi ya Mji Mkuu wa Mogadishu
.

HabariLeo | Tanzania yatoa msaada wa tani 300 Somalia

Nimefarijika kwa hili suala la kusaidia Somalia kwa mahindi, ila kuna sentensi imepindishwa hapo.. Sio kweli kwamba jeshi la Somalia/Afrisom lilowaondoa Al-Shabab maeneo ya Mogadishu ila ni Alshabab wenyewe ndo waliamua kuondoka.

- For more reference please click here Al-Shabab Militants Retreat from Mogadishu | Africa | English
 
Muislam ndugu yake ni muislam
ila iliniuma sana al shabab walipokataa kuruhusu chakula kusambazwa mogadishu
jamani dini inaelekeza hivii isaidieni?
 
Back
Top Bottom