BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Date::11/2/2008
Tanzania yatoa chipukizi kucheza soka ya kulipwa Ulaya
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi
HATIMAYE Tanzania imetoa nyota watatu wa mpango wa Vodacom Global Soccer Star (VGSS) ambao wataondoka karibuni kwenda Ulaya kujiunga na mpira wa kulipwa.
Nyota hao, Cosmas Mwazembe, Francis Casto (Mbeya) ambao watajiunga na timu ya Reading FC ya Uingereza inayocheza Ligi Daraja la Kwanza baada ya msimu uliopita kushuka daraja kutoka ile ya Barclays Premier League wakati Salum Saad (Zanzibar) atajiunga na shule maalum ya michezo iliyopo Marbella Hispania .
Mdau maarufu wa michezo nchini, Kanali Iddi Kipingu, mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuwatangaza nyota hao aliipongeza Kampuni ya Vodacom kwa kudhamini mpango huo.
Alisema Tanzania inapiga hatua kubwa kwa upande wa michezo kwani kwa mara ya kwanza inakuwa na wachezaji wa kulipwa katika ligi kubwa na maarufu duniani, yaani Uingereza.
Alisema wachezaji hao pia wataimarisha timu ya taifa ya Tanzania (Stars) kwa siku za usoni na kuomba wadau wengine wa michezo wajiingizie katika mchakato kutafuta na kuendeleza vipaji kwa vijana kwani ndiyo njia pekee ya kuifanya Tanzania isomeke katika ramani ya soka duniani.
Vijana hao wamepatikana kutokana na kura za Watanzania ambao walikuwa wakiwapigia kura vijana 35 waliokuwa kambini jijini Dar es Salaam kwa wiki tano na hatimaye wamepatika watatu.
Habari za ndani ya Vodacom Tanzania zinasema kwamba awali alitakiwa kijana mmoja tu kujiunga na timu ya Reading, lakini baada ya kuridhishwa na kiwango chao, timu hiyo iliomba ipatiwe wachezaji wawili.
Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania, Ephraem Mafuru alisema kwamba zaidi ya vijana 11,000 kote nchini walipitia mchujo huo ambao umewezesha vijana watatu kuwa nyota.
Aliwapongeza vijana hao na kusema kwamba Vodacom Tanzania itanendelea kuwekeza katika soka.
Naye Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodegar Tenga aliipongeza Vodacom kwa kuanzisha programu hiyo ya kusaka vipaji.
Alisema ni faraja kubwa kwa Tanzania kuanza kuwa na nyota wake Ulaya ambao wamekenda huko baada ya kuonyesha vipaji katika vya kusakata soka katika umri mdogo.
Mpango huo wa kusaka vipaji ulianza Mei mwaka huu na vituo vya kukusanyikia vijana viligawanywa katika kanda ambapo vijana wenye umri wa miaka kati ya 16 na 22 walikusanywa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya Zanzibar na Arusha.
Tanzania yatoa chipukizi kucheza soka ya kulipwa Ulaya
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi
HATIMAYE Tanzania imetoa nyota watatu wa mpango wa Vodacom Global Soccer Star (VGSS) ambao wataondoka karibuni kwenda Ulaya kujiunga na mpira wa kulipwa.
Nyota hao, Cosmas Mwazembe, Francis Casto (Mbeya) ambao watajiunga na timu ya Reading FC ya Uingereza inayocheza Ligi Daraja la Kwanza baada ya msimu uliopita kushuka daraja kutoka ile ya Barclays Premier League wakati Salum Saad (Zanzibar) atajiunga na shule maalum ya michezo iliyopo Marbella Hispania .
Mdau maarufu wa michezo nchini, Kanali Iddi Kipingu, mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuwatangaza nyota hao aliipongeza Kampuni ya Vodacom kwa kudhamini mpango huo.
Alisema Tanzania inapiga hatua kubwa kwa upande wa michezo kwani kwa mara ya kwanza inakuwa na wachezaji wa kulipwa katika ligi kubwa na maarufu duniani, yaani Uingereza.
Alisema wachezaji hao pia wataimarisha timu ya taifa ya Tanzania (Stars) kwa siku za usoni na kuomba wadau wengine wa michezo wajiingizie katika mchakato kutafuta na kuendeleza vipaji kwa vijana kwani ndiyo njia pekee ya kuifanya Tanzania isomeke katika ramani ya soka duniani.
Vijana hao wamepatikana kutokana na kura za Watanzania ambao walikuwa wakiwapigia kura vijana 35 waliokuwa kambini jijini Dar es Salaam kwa wiki tano na hatimaye wamepatika watatu.
Habari za ndani ya Vodacom Tanzania zinasema kwamba awali alitakiwa kijana mmoja tu kujiunga na timu ya Reading, lakini baada ya kuridhishwa na kiwango chao, timu hiyo iliomba ipatiwe wachezaji wawili.
Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania, Ephraem Mafuru alisema kwamba zaidi ya vijana 11,000 kote nchini walipitia mchujo huo ambao umewezesha vijana watatu kuwa nyota.
Aliwapongeza vijana hao na kusema kwamba Vodacom Tanzania itanendelea kuwekeza katika soka.
Naye Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodegar Tenga aliipongeza Vodacom kwa kuanzisha programu hiyo ya kusaka vipaji.
Alisema ni faraja kubwa kwa Tanzania kuanza kuwa na nyota wake Ulaya ambao wamekenda huko baada ya kuonyesha vipaji katika vya kusakata soka katika umri mdogo.
Mpango huo wa kusaka vipaji ulianza Mei mwaka huu na vituo vya kukusanyikia vijana viligawanywa katika kanda ambapo vijana wenye umri wa miaka kati ya 16 na 22 walikusanywa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya Zanzibar na Arusha.