Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Tanzania,
Nchi ya babu na bibi zangu. Nakupenda na kukutukuza.
Ila nasikitika kwamba kumbukumbu nzuri na tamu kuhusu wewe ni wimbo na bendera yako.
Vingine vyote nimevisahau. Madini, mito, milima, maziwa, misitu, hifadhi, viwanda, watu n.k. Vyote ni mali za wengine. Hakuna hata kimoja ambacho naweza kutembea kifua mbele nakujisifu kwamba ni changu au chetu.
Kwa muda mrefu sasa wanasiasa wamejidai ni viongozi. Wanachofanya ni siasa na si kuongoza. Wangetuongoza tusingefikia hapa tulipo. Ahadi zao siku zote zilikuwa kulinda mali zako na kutuletea neema. Tuliahidiwa kupigana vita dhidi ya Maradhi, Umasikini na Ujinga siku nyingi sana. Nilikuwa sijazaliwa ila bibi na babu walinihadithia kabla hawajatangulia mbele ya haki. Mpaka leo hii vita haijaanza. Silaha zilizokuwa zimekusanywa kwa ajili ya vita zimekwisha muda wake na muda na saa yoyote zitalipuka zenyewe. Hata hivyo haitakuwa jambo geni kwani kuna silaha nyingine zilikusanywa kwa ajili ya vita ambayo hatuijui zinalipuka zenyewe na kutuua. Sasa hivi wanao wengine wanaishi kwenye mahema.
Tanzania, kama tungeanza vita dhidi ya maradhi wanao wengi wasingekimbilia Loliondo kwa Babu. Angalau Babu anatibu kwa imani. Tunapata matumaini lakini kwa bahati mbaya wengine wetu wanakufa wakati wanapata tiba. Wanafika huko kwa shida na tabu kuu. Wengine wamekufa baada ya magari yao kugongana uso kwa uso kwa sababu ya vumbi!! Hata lile tumaini dogo tunalopata muda mwingine linatuharakishia mauti. Babu anatibu magonjwa sugu ila hazuii ajali zitokanazo na uzembe au barabara mbovu.
Tanzania, kama tungeanza vita dhidi ya umasikini mapema basi wengi wangefika Loliondo kupata tiba ili kufidia kuchelewa kwetu kuanza vita dhidi ya maradhi. maelfu wanalia vijijini. Hawana uwezo wa kufika Loliondo. Tunafanyaje?
Bado sisi ni masikini wa kutupwa. Hakuna anayetuthamini tena. Siku zote asiye na kitu hathaminiwi. Tukiongea tunaambiwa tunatishia amani na utulivu. Tukitembea tunaambiwa ni wazururaji, wezi, hatuna cha kufanya, wanafiki na maneno mengi ya kejeli na dharau.
Eti tunaambiwa tunafadhiliwa na nchi fulani kuleta fujo. Hivi, inawezekanaje nikalipwa au kufadhiliwa ili niseme kwamba nina njaa, sina kazi, nchi yangu inauzwa, naibiwa, nadhalilishwa nk? Kwa nini nilipwe ili niijue hali yangu ya ufukara?
Kama ningekuwa na kiongozi basi maneno hayo yasingesemwa. Kamwe kiongozi hawezi kuacha kazi za umma, akaenda kutumia chombo cha umma kuueleza umma kwamba 'chama fulani kinafadhiliwa na nchi fulani'......Ni kiongozi wa aina gani huyu kama sio mwanasiasa tu? hapo anafanya kazi yake, siasa.
Tanzania, haya yote yanawezekana kwa sababu wanasiasa wanaamini kwamba kwa kutokuanzisha vita dhidi ya Ujinga basi sisi ni wajinga. hilo ndio kosa lao kubwa ambalo muda si mrefu litatuletea neema. Kwa njia moja au nyingine Mungu amewaruhusu walitende hilo kosa.
Kwa kukosa kwetu elimu ya darasani (tumeipata ile ya shule na vyuo vya kata) wanadhani watatufanyia siasa milele kwa kisingizio wanatuongoza. tutawafundisha adabu. Sasa hatutaki tena kutumiwa. Kama ni AMANI ni yetu wote. Kama ni UTULIVU ni wetu wote.
Tanzania, niruhusu nitubu na kukiri kwamba endapo nyoka ataingia ndani kwangu na kujificha kwenye mtungi wa kioo kisha nishindwe kumtoa, kuliko nirudi kulala atoke aning'ate nitauvunja huo mtungi nimuue. Nadhani nitakuwa salama zaidi.
Nisipofanya hivyo sitalala kwa amani, na sitakuwa salama. Mwenzake atamfuata na wataweka makazi huku wakizaliana kwa imani kwamba sitathubutu kuuvunja mtungi wangu wa kioo. Wataendelea kufurahia ulaini wa kioo pamoja na joto la ndani mwangu na muda wote watakuwa kazi yao ni kujamiiana ili waongezeke huku mimi nikiendelea kukaa macho na wasiwasi tele kuhusu uhai wangu. Sitavumilia. Sivumilii tena.
Tumewachoka wanasiasa. Sasa tunataka tupate viongozi. Tunataka kuikomboa nchi yetu kutoka mikononi mwao. Hatutaki ahadi zao tena. Ni za muda mrefu na zitalipuka na kuleta madhara zaidi tukiwaendekeza.
Na vile vitoto vya nyoka vinavyojidai kuandamana eti kupongeza hotuba baada ya kuona kwamba hakuna maendeleo ya kupongeza tutaviteketeza pamoja na mtungi. Vinakimbilia kujificha ndani ya mtungi pamoja na mijoka mikubwa. Wote hawatasalimika. Vioo vya mtungi na marungu yetu vitawawahusu.
Tanzania, nakupenda. Ila kama Mungu atakupenda zaidi ahadi zake zitimizwe.
Nchi ya babu na bibi zangu. Nakupenda na kukutukuza.
Ila nasikitika kwamba kumbukumbu nzuri na tamu kuhusu wewe ni wimbo na bendera yako.
Vingine vyote nimevisahau. Madini, mito, milima, maziwa, misitu, hifadhi, viwanda, watu n.k. Vyote ni mali za wengine. Hakuna hata kimoja ambacho naweza kutembea kifua mbele nakujisifu kwamba ni changu au chetu.
Kwa muda mrefu sasa wanasiasa wamejidai ni viongozi. Wanachofanya ni siasa na si kuongoza. Wangetuongoza tusingefikia hapa tulipo. Ahadi zao siku zote zilikuwa kulinda mali zako na kutuletea neema. Tuliahidiwa kupigana vita dhidi ya Maradhi, Umasikini na Ujinga siku nyingi sana. Nilikuwa sijazaliwa ila bibi na babu walinihadithia kabla hawajatangulia mbele ya haki. Mpaka leo hii vita haijaanza. Silaha zilizokuwa zimekusanywa kwa ajili ya vita zimekwisha muda wake na muda na saa yoyote zitalipuka zenyewe. Hata hivyo haitakuwa jambo geni kwani kuna silaha nyingine zilikusanywa kwa ajili ya vita ambayo hatuijui zinalipuka zenyewe na kutuua. Sasa hivi wanao wengine wanaishi kwenye mahema.
Tanzania, kama tungeanza vita dhidi ya maradhi wanao wengi wasingekimbilia Loliondo kwa Babu. Angalau Babu anatibu kwa imani. Tunapata matumaini lakini kwa bahati mbaya wengine wetu wanakufa wakati wanapata tiba. Wanafika huko kwa shida na tabu kuu. Wengine wamekufa baada ya magari yao kugongana uso kwa uso kwa sababu ya vumbi!! Hata lile tumaini dogo tunalopata muda mwingine linatuharakishia mauti. Babu anatibu magonjwa sugu ila hazuii ajali zitokanazo na uzembe au barabara mbovu.
Tanzania, kama tungeanza vita dhidi ya umasikini mapema basi wengi wangefika Loliondo kupata tiba ili kufidia kuchelewa kwetu kuanza vita dhidi ya maradhi. maelfu wanalia vijijini. Hawana uwezo wa kufika Loliondo. Tunafanyaje?
Bado sisi ni masikini wa kutupwa. Hakuna anayetuthamini tena. Siku zote asiye na kitu hathaminiwi. Tukiongea tunaambiwa tunatishia amani na utulivu. Tukitembea tunaambiwa ni wazururaji, wezi, hatuna cha kufanya, wanafiki na maneno mengi ya kejeli na dharau.
Eti tunaambiwa tunafadhiliwa na nchi fulani kuleta fujo. Hivi, inawezekanaje nikalipwa au kufadhiliwa ili niseme kwamba nina njaa, sina kazi, nchi yangu inauzwa, naibiwa, nadhalilishwa nk? Kwa nini nilipwe ili niijue hali yangu ya ufukara?
Kama ningekuwa na kiongozi basi maneno hayo yasingesemwa. Kamwe kiongozi hawezi kuacha kazi za umma, akaenda kutumia chombo cha umma kuueleza umma kwamba 'chama fulani kinafadhiliwa na nchi fulani'......Ni kiongozi wa aina gani huyu kama sio mwanasiasa tu? hapo anafanya kazi yake, siasa.
Tanzania, haya yote yanawezekana kwa sababu wanasiasa wanaamini kwamba kwa kutokuanzisha vita dhidi ya Ujinga basi sisi ni wajinga. hilo ndio kosa lao kubwa ambalo muda si mrefu litatuletea neema. Kwa njia moja au nyingine Mungu amewaruhusu walitende hilo kosa.
Kwa kukosa kwetu elimu ya darasani (tumeipata ile ya shule na vyuo vya kata) wanadhani watatufanyia siasa milele kwa kisingizio wanatuongoza. tutawafundisha adabu. Sasa hatutaki tena kutumiwa. Kama ni AMANI ni yetu wote. Kama ni UTULIVU ni wetu wote.
Tanzania, niruhusu nitubu na kukiri kwamba endapo nyoka ataingia ndani kwangu na kujificha kwenye mtungi wa kioo kisha nishindwe kumtoa, kuliko nirudi kulala atoke aning'ate nitauvunja huo mtungi nimuue. Nadhani nitakuwa salama zaidi.
Nisipofanya hivyo sitalala kwa amani, na sitakuwa salama. Mwenzake atamfuata na wataweka makazi huku wakizaliana kwa imani kwamba sitathubutu kuuvunja mtungi wangu wa kioo. Wataendelea kufurahia ulaini wa kioo pamoja na joto la ndani mwangu na muda wote watakuwa kazi yao ni kujamiiana ili waongezeke huku mimi nikiendelea kukaa macho na wasiwasi tele kuhusu uhai wangu. Sitavumilia. Sivumilii tena.
Tumewachoka wanasiasa. Sasa tunataka tupate viongozi. Tunataka kuikomboa nchi yetu kutoka mikononi mwao. Hatutaki ahadi zao tena. Ni za muda mrefu na zitalipuka na kuleta madhara zaidi tukiwaendekeza.
Na vile vitoto vya nyoka vinavyojidai kuandamana eti kupongeza hotuba baada ya kuona kwamba hakuna maendeleo ya kupongeza tutaviteketeza pamoja na mtungi. Vinakimbilia kujificha ndani ya mtungi pamoja na mijoka mikubwa. Wote hawatasalimika. Vioo vya mtungi na marungu yetu vitawawahusu.
Tanzania, nakupenda. Ila kama Mungu atakupenda zaidi ahadi zake zitimizwe.