Kizimkazimkuu
JF-Expert Member
- Nov 8, 2007
- 337
- 234
Ukiachilia mbali kuwa matokeo ya suluhu dhidi ya Ageria mchezo uliofanyika Ijumaa katika mjia wa BILDA, Algeria utaacha kumbukumbu nyingine ambayo pengine itachukua kipindi kirefu kufutika. Kikosi chote kilichocheza mchezo huo hakikumuhusisha hata mchezaji mmoja wa SIMBA SC jambo ambalo wafuatiliaji wa soka wanaeleza liliwahi kutokea mwaka 1990 katika michuano ya challenge! Kikosi kilichocheza Bilda kilikuwa hivi: Kado (Mtibwa). Mwasika(Azam), Jabir Idrisa (sofapaka),Nsajigwa (Yanga), Cannavaro (Yanga), Abdi/Babi(Yanga),Agrey Morris (Azam), Ngassa(Azam), Mrwanda(Vietnam), Henry Joseph (Sweden) Nizar(Canada). Mshambuliaji wa Simba Mgosi na Beki Kanoni hawakuwepo hata katika orodha iliyokuwa Benchi. Source: Mwanaspoti Jumanne, 7th Sept, 2010
Kwa muda mrefu washabiki wa Simba na Yanga wamekuwa wakiamini kuwa bila wachezaji wa vilabu hivyo vikubwa mpira hautachezwa..na makocha wengi wameingia matatizo kwa kuwaacha wachezaji fulani vipenzi wa Timu hizo. Mhanga wa mwisho alikuwa ni Maximo ambaye ameondoka akibebeshwa lkawama kwa kuwaacha Chuji, Kaseja na Boban wa Msimbazi. Jan Poulsen ametufungulia ukurasa mpya tumpe nafasi.........
Kwa muda mrefu washabiki wa Simba na Yanga wamekuwa wakiamini kuwa bila wachezaji wa vilabu hivyo vikubwa mpira hautachezwa..na makocha wengi wameingia matatizo kwa kuwaacha wachezaji fulani vipenzi wa Timu hizo. Mhanga wa mwisho alikuwa ni Maximo ambaye ameondoka akibebeshwa lkawama kwa kuwaacha Chuji, Kaseja na Boban wa Msimbazi. Jan Poulsen ametufungulia ukurasa mpya tumpe nafasi.........