Informer
JF-Expert Member
- Jul 29, 2006
- 1,582
- 6,627
UTAJIRI wa gesi asilia Tanzania, unatishiwa na ufisadi ndani ya mfumo wa utawala na kuna taarifa za uhamishaji wa fedha zinazohofiwa kutokana na uwekezaji katika sekta hiyo.
Uchunguzi umeonyesha kwamba, kwa miaka kadhaa, baadhi ya watu ndani ya mfumo wamekua wakitumia mbinu chafu kujinufaisha na rasilimali ya gesi nchini.
Tanzania inatarajiwa kuongeza makisio ya kiwango cha utajiri wake wa gesi asilia hadi kufikia takriban futi za ujazo trilioni 30.
Pamoja na marekebisho hayo, kuna mashaka kama mapato mengi yatakayotokana na gesi hiyo yatatumika vema bila kuathiriwa na ufisadi.
Hata hivyo Kabwe amekuwa akijumuisha pamoja ufisadi mdogona mkubwa ili kulitohoa suala la ufisadi na kuishinikiza serikali.
Agosti 15, 2012 Zitto alitangaza kwamba taarifa ya mwezi Juni ya benki kuu ya Uswisi, Swiss National Bank (SNB), ilionyesha kwamba viongozi serikalini pamoja na wafanyabiashara wakubwa walikuwa wameficha fedha katika akaunti zao nchini humo zinazofikia 315.5bilioni/- (USD 200million).
Kila mwaka Benki Kuu ya Uswisi huchapisha jumla ya fedha na mikopo zinazomilikiwa na wageni, ingawaje taarifa hiyo haichambui kiasi ambacho kila mwenye akaunti anamiliki.
Kabwe aliliambia bunge, "Kambi rasmi ya upinzani imepata taarifa kwamba kiongozi mmoja mwandamizi na mawaziri kadhaa katika utawala uliopita wamo katika orodha ya watu wenye mapesa hayo.
Sehemu kubwa ya pesa hizo zililipwa na makampuni yanayotafuta mafuta na gesi katika pwani ya Mtwara yaliyopewa leseni kati ya mwaka 2004 na 2006.
"Kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali kutoa tamko rasmi kuhusu hatua ilizochukua tangu tangu ripoti hiyo ya Benki Kuu ya Uswisi ilipotoka. Tunaitaka serikali iliambie taifa hatua itakazochukua ili kuzirejesha fedha hizi pamoja na nyingine ambazo zimefichwa katika nchi nyingine za nje. Kambi rasmi ya upinzani itayatangaza majina ya wanaomiliki fedha hizi katika mabenki nchini Uswisi kama serikali haitotoa taarifa rasmi juu ya suala hili."
Kampuni ya Kiingereza ya Ophir Energy, ambayo inamilikiwa kwa ubia na kigogo mmoja katika chama tawala nchini Afrika ya Kusini cha African National Council, Waziri wa Makazi Tokyo Sexwale, kilipewa Kitalu 1 katika pwani ya Mtwara katika duru ya tatu ya utoaji leseni mwaka 2005.
Ophir ilipewa vitalu viwili zaidi, Kitalu 3 na 4, bila kushindanishwa mwaka uliofuata. Hii si kutoa hisia kwamba rushwa ilihusika. BG, zamani ikiitwa British Gas, baadaye ilinunua hisa katika vitalu hivyo na ndiyo inayoviendesha wakati Ophir ni mbia mwenye hisa chache.
Mtu wa kati ambaye ni mfanyabiashara raia wa Afrika ya Kusini na mwenye mahusiano ya karibu na ANC, Moto Mabanga, alisaidia Ophir kupata vitalu hivyo. Alifungua kesi jijini London mwezi Juni 2012 dhidi ya Ophir kuhusiana na mgao wake wa asilimia tano (5%) ya faida kwa mujibu wa mkataba wa kuchangia uzalishaji uliofikiwa.
Mabanga pia aliliingia katika mgogoro na kampuni ya nchini Afrika ya Kusini ya Vodacom juu ya ada kwa huduma zake baada ya kufanisha matatizo yaliyokuwa yanaitatiza kampuni hiyo nchi Kongo-Kinshasa.
CHANZO - Fikra Pevu
Uchunguzi umeonyesha kwamba, kwa miaka kadhaa, baadhi ya watu ndani ya mfumo wamekua wakitumia mbinu chafu kujinufaisha na rasilimali ya gesi nchini.
Tanzania inatarajiwa kuongeza makisio ya kiwango cha utajiri wake wa gesi asilia hadi kufikia takriban futi za ujazo trilioni 30.
Pamoja na marekebisho hayo, kuna mashaka kama mapato mengi yatakayotokana na gesi hiyo yatatumika vema bila kuathiriwa na ufisadi.
------- Nimeruka mistari kadhaa-------
Hata hivyo ni uwezekano mkubwa wa ufisadi wa kutisha katika kutoa leseni mpya za utafutaji gesi baharini unakowaogofya wachambuzi wa mambo katika tasnia hiyo.
Hata hivyo Kabwe amekuwa akijumuisha pamoja ufisadi mdogona mkubwa ili kulitohoa suala la ufisadi na kuishinikiza serikali.
Agosti 15, 2012 Zitto alitangaza kwamba taarifa ya mwezi Juni ya benki kuu ya Uswisi, Swiss National Bank (SNB), ilionyesha kwamba viongozi serikalini pamoja na wafanyabiashara wakubwa walikuwa wameficha fedha katika akaunti zao nchini humo zinazofikia 315.5bilioni/- (USD 200million).
Kila mwaka Benki Kuu ya Uswisi huchapisha jumla ya fedha na mikopo zinazomilikiwa na wageni, ingawaje taarifa hiyo haichambui kiasi ambacho kila mwenye akaunti anamiliki.
Kabwe aliliambia bunge, "Kambi rasmi ya upinzani imepata taarifa kwamba kiongozi mmoja mwandamizi na mawaziri kadhaa katika utawala uliopita wamo katika orodha ya watu wenye mapesa hayo.
Sehemu kubwa ya pesa hizo zililipwa na makampuni yanayotafuta mafuta na gesi katika pwani ya Mtwara yaliyopewa leseni kati ya mwaka 2004 na 2006.
"Kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali kutoa tamko rasmi kuhusu hatua ilizochukua tangu tangu ripoti hiyo ya Benki Kuu ya Uswisi ilipotoka. Tunaitaka serikali iliambie taifa hatua itakazochukua ili kuzirejesha fedha hizi pamoja na nyingine ambazo zimefichwa katika nchi nyingine za nje. Kambi rasmi ya upinzani itayatangaza majina ya wanaomiliki fedha hizi katika mabenki nchini Uswisi kama serikali haitotoa taarifa rasmi juu ya suala hili."
Kampuni ya Kiingereza ya Ophir Energy, ambayo inamilikiwa kwa ubia na kigogo mmoja katika chama tawala nchini Afrika ya Kusini cha African National Council, Waziri wa Makazi Tokyo Sexwale, kilipewa Kitalu 1 katika pwani ya Mtwara katika duru ya tatu ya utoaji leseni mwaka 2005.
Ophir ilipewa vitalu viwili zaidi, Kitalu 3 na 4, bila kushindanishwa mwaka uliofuata. Hii si kutoa hisia kwamba rushwa ilihusika. BG, zamani ikiitwa British Gas, baadaye ilinunua hisa katika vitalu hivyo na ndiyo inayoviendesha wakati Ophir ni mbia mwenye hisa chache.
Mtu wa kati ambaye ni mfanyabiashara raia wa Afrika ya Kusini na mwenye mahusiano ya karibu na ANC, Moto Mabanga, alisaidia Ophir kupata vitalu hivyo. Alifungua kesi jijini London mwezi Juni 2012 dhidi ya Ophir kuhusiana na mgao wake wa asilimia tano (5%) ya faida kwa mujibu wa mkataba wa kuchangia uzalishaji uliofikiwa.
Mabanga pia aliliingia katika mgogoro na kampuni ya nchini Afrika ya Kusini ya Vodacom juu ya ada kwa huduma zake baada ya kufanisha matatizo yaliyokuwa yanaitatiza kampuni hiyo nchi Kongo-Kinshasa.
CHANZO - Fikra Pevu