Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Unapotafakari hatima ya Taifa letu na mwelekeo wake, kuna jambo ambalo linaongoza na kutawala mawazo na kauli zetu, suala la Uongozi Bora na Siasa Safi kama tulivyoapa katika Azimio la Arusha.
Najiuliza kwa kutumia watu wafuatao katika kujenga kwangu hoja, Mkapa, Kikwete,Migiro, Seleli, Karume, Lowassa, Ole Naiko, Mattaka, Kilewo, Zitto, Nyang'anyi, Mukandara, Mrema, Cheyo, Tibaijuka, Rostam, Kawawa, Dewji, Mengi, Ulimwengu, Pengo, Mwalasusa na wengineo.
Nimeweka mkorogo wa wanasiasa, wafanyabiashara, watu wa dini na watanzania ambao kwa ujumla huwa ni maarufu katika habari, ikiwa na maana wana nafasi fulani inayokuwa na wafuasi kama si washabiki.
Kwa kuangalia mkorogo huu na kuangalia dhana yetu ya kujijenga kama jamii iliyokomaa na endelevu, swali langu laja; Je Tanzania tuna Viongozi, Watawala au Mabwana?
Maana sielewi ni vipi kuwa mpaka leo tunazunguka kama pia bila mwelekeo na kuna kuwa na mvutano mkubwa ambao unatishia kumegua Taifa letu katika vipande vya tabaka la uwezo kimali kati ya walionazo na wasionacho, mvurugano wa kidini, kikabila, kielimu, kijinsia, kiumri na kiitikadi.
Inakuwa kana kwamba Watanzania hatujui tupate wapi hamasa au mvuto wa kutuongoza. Tunakuwa kama kondoo au mbuzi waliopotea malishoni na kuendelea na safari kutafuta nyasi na maji hata pamoja na kuwa jua limechwea na ni wakati wa kurudi zizini!
Ni nini kinachotukabili Watanzania kuwa tunakosa dira ya kujituma tuwe mahiri wenye juhudi, maarifa, uadilifu, utu, hekima na busara?
Ikiwa tuliwapa dhamana kutuoongoza katika Serikali, Mashirika, Taasisi, Jumuiya, Mashule, Nyumba za ibada na hata mitaani na majumbani hawana mwamko au mwelekeo wa kuwa Viongozi wa mfano bali wao ni Watawala na Mabwana, je kuna salama ya huko tunakokwenda?
Cheo hakina maana ya mtu kuwa mtemi, mnyapara, mwenye nguvu, amri au manufaa binafsi, bali ni wajibu mkubwa unaotokana na cheo, ndio unaoleta maana ya mtu kuwa na cheo.
Sawasawa na Uongozi, uongozi ni dhamana, kama tulivyosema "cheo ni dhamana"!
Uongozi si maneno na kauli tuu, bali ni vitendo na nidhamu ya hali ya juu inayoandamana na umakini, busara, uadilifu na wepesi wa kuwa msikivu na hata kuvumilia kubezwa na wafuasi.
Ukiangalia na kupembua matatizo ya Watanzania na Taifa letu, utabaini kuwa kuna ukosefu mkubwa wa Uongozi ambao unajua maana ya uongozi; kufanya kazi kwa bidii, kuwa waadilifu na wenye nidhamu, kujali walio chini, kuwa wenye maono ya mbali na kutafuta njia bora za kutatua matatizo na si kukimbilia viraka.
Kila siku ya Mungu tunapoamka, kuna habari moja kama si mbili ambayo inahusu kuyumba na kukosekana kwa uwajibikaji na Uongozi kutoka kwa wale ambao wanafikirika kuwa ndio viongozi wetu katika jamii.
Nenda Bungeni, Serikalini, Mashirikani, Makanisani, Shuleni, Mijini, Vijijini na hata Majumbani, kuna udhaifu mkubwa sana wa Uongozi ambao ndio msingi mkuu wa Ustawi wetu kama jamii na Taifa.
Fungua gazeti lako leo, utakutana na habari za kusikitisha, ajira hakuna, ubadhirifu, ufujaji, kukosekana maadili, ubabe, dharau, vitisho, kubeza, amri na kila aina ya Udikteta alimradi mtu anatumia misuli ya shingo na kutunisha kifua kuonyesha kuwa yeye ni Bwana Mkubwa!
Zimekwenda wapi Busara, Hekima, Ufanisi, Uwajibikaji, Hamasa, Unyenyekevu, Usikivu na hata Upendo?
Iweje tangu tujitawale kwa kupiga vita ukoloni na uonevu na hata siasa za Kibeberu, leo hii tunakubali kuburuzwa na Watanzania wenzetu ambao ni Watawala na Mabwana na si Viongozi?
Tunapokwenda kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa Serikali za Mitaa, diwani na meya tutakayemchagua tutampa mamlaka awe Mtawala, Bwana na Mnyapara au ni ndugu yetu tunayemuamini kuwa anajituma na kujitolea kutumia hekina na busara kutuongoza na kutetea haki zetu?
Na hata mwakani tutakapoanza kutafuta Wabunge, Wawakilishi na Marais wa Muungano na Zanzibar, tuko tayari kuanza kuwapima wanaotaka nafasi hizo kwa kuangalia kama kweli wana uwezo wa kuongoza au tutajinyong'onyea kwa unyonge na kuruhusu kutawaliwa na Mabwana Wakubwa ambao wao ni Mwanzo na Mwisho wa kila kitu na sisi hatuna hata sauti moja au kauli ila ni kusema "ndiyo mzee", "ndiyo bosi" "ndiyo mkubwa" na kuwa na nidhamu ya woga badala ya kuwa na heshima na kutembea kifua mbele tukijigamba kuwa tuna Viongozi wachapa kazi wenye kujali maslahi yetu kama Jamii na Taifa?
Je kizazi cha mababu zetu, mababa zetu na hata chetu cha sasa, hakina hata watu kumi ambao wanaweza kuwa na mfano chanya wa maana ya uongozi na hivyo kuliondoa Taifa letu kutoka unyonge wa kuwa watumwa na kunyanyaswa na kupuuzwa?
Hivi kweli ndani ya Bunge, hakuna watu weye Busara kumi ambao wanaweza kulonga na Bunge zima likaafiki kufanya mambo ya Busara na Hekima na si Ushabiki wa Pwagu na Pwaguzi?
Je kwenye bodi za menejimenti, hakuna wajumbe wenye msimamo na kauli ambao wanaweza kusimama kidete an kusema "hapa tumekosea" "lile halikuwa sahihi" "matumizi haya hayana manufaa" nao wakazikilizwa na kuheshimiwa na hivyo shirika, taasisi au jumuiya ikaonelea kuwa kuna umuhimu wa kujirudi na kujisahihisha?
Je tuende kuazima Viongozi kutoka kwa Wazungu, Warwanda na Wachina?
Ni lini tutaanza kuzalisha uzao wa Viongozi wenye maono, wachapakazi, jasiri, wabunifu, fanisi, wanyenyekevu, waadilifu, wakweli, wasiopenda makuu na wenye kuelewa maana ya Uongozi na umuhimu wa kuhamasisha na kutetea haki za jamii zao na si kujifikiria wao kwanza?
Mwisho, kwa walio madarakani, je wanaelewa kuwa mafanikio yanatokana na ushirikishi na kuaminika kutoka kwetu sisi Wananchi? Ikiwa Walioko juu tunaowaita Vigogo, Vibosile, Wakubwa, Pedeje, Wanene na Wenyewe hawatambui kuwa sisi tulio chini tuliowapa dhamana ya kuongoza ni muhimu na tuna thamani, kuna faida gani kuendelea kuwa na watu kama hao wanaodhani wao ni Miungu watu na kuwa Uongozi wa Taifa na Jamii yetu ni Urithi wao wa milele au hakuna mwingine zaidi yao?
Najiuliza kwa kutumia watu wafuatao katika kujenga kwangu hoja, Mkapa, Kikwete,Migiro, Seleli, Karume, Lowassa, Ole Naiko, Mattaka, Kilewo, Zitto, Nyang'anyi, Mukandara, Mrema, Cheyo, Tibaijuka, Rostam, Kawawa, Dewji, Mengi, Ulimwengu, Pengo, Mwalasusa na wengineo.
Nimeweka mkorogo wa wanasiasa, wafanyabiashara, watu wa dini na watanzania ambao kwa ujumla huwa ni maarufu katika habari, ikiwa na maana wana nafasi fulani inayokuwa na wafuasi kama si washabiki.
Kwa kuangalia mkorogo huu na kuangalia dhana yetu ya kujijenga kama jamii iliyokomaa na endelevu, swali langu laja; Je Tanzania tuna Viongozi, Watawala au Mabwana?
Maana sielewi ni vipi kuwa mpaka leo tunazunguka kama pia bila mwelekeo na kuna kuwa na mvutano mkubwa ambao unatishia kumegua Taifa letu katika vipande vya tabaka la uwezo kimali kati ya walionazo na wasionacho, mvurugano wa kidini, kikabila, kielimu, kijinsia, kiumri na kiitikadi.
Inakuwa kana kwamba Watanzania hatujui tupate wapi hamasa au mvuto wa kutuongoza. Tunakuwa kama kondoo au mbuzi waliopotea malishoni na kuendelea na safari kutafuta nyasi na maji hata pamoja na kuwa jua limechwea na ni wakati wa kurudi zizini!
Ni nini kinachotukabili Watanzania kuwa tunakosa dira ya kujituma tuwe mahiri wenye juhudi, maarifa, uadilifu, utu, hekima na busara?
Ikiwa tuliwapa dhamana kutuoongoza katika Serikali, Mashirika, Taasisi, Jumuiya, Mashule, Nyumba za ibada na hata mitaani na majumbani hawana mwamko au mwelekeo wa kuwa Viongozi wa mfano bali wao ni Watawala na Mabwana, je kuna salama ya huko tunakokwenda?
Cheo hakina maana ya mtu kuwa mtemi, mnyapara, mwenye nguvu, amri au manufaa binafsi, bali ni wajibu mkubwa unaotokana na cheo, ndio unaoleta maana ya mtu kuwa na cheo.
Sawasawa na Uongozi, uongozi ni dhamana, kama tulivyosema "cheo ni dhamana"!
Uongozi si maneno na kauli tuu, bali ni vitendo na nidhamu ya hali ya juu inayoandamana na umakini, busara, uadilifu na wepesi wa kuwa msikivu na hata kuvumilia kubezwa na wafuasi.
Ukiangalia na kupembua matatizo ya Watanzania na Taifa letu, utabaini kuwa kuna ukosefu mkubwa wa Uongozi ambao unajua maana ya uongozi; kufanya kazi kwa bidii, kuwa waadilifu na wenye nidhamu, kujali walio chini, kuwa wenye maono ya mbali na kutafuta njia bora za kutatua matatizo na si kukimbilia viraka.
Kila siku ya Mungu tunapoamka, kuna habari moja kama si mbili ambayo inahusu kuyumba na kukosekana kwa uwajibikaji na Uongozi kutoka kwa wale ambao wanafikirika kuwa ndio viongozi wetu katika jamii.
Nenda Bungeni, Serikalini, Mashirikani, Makanisani, Shuleni, Mijini, Vijijini na hata Majumbani, kuna udhaifu mkubwa sana wa Uongozi ambao ndio msingi mkuu wa Ustawi wetu kama jamii na Taifa.
Fungua gazeti lako leo, utakutana na habari za kusikitisha, ajira hakuna, ubadhirifu, ufujaji, kukosekana maadili, ubabe, dharau, vitisho, kubeza, amri na kila aina ya Udikteta alimradi mtu anatumia misuli ya shingo na kutunisha kifua kuonyesha kuwa yeye ni Bwana Mkubwa!
Zimekwenda wapi Busara, Hekima, Ufanisi, Uwajibikaji, Hamasa, Unyenyekevu, Usikivu na hata Upendo?
Iweje tangu tujitawale kwa kupiga vita ukoloni na uonevu na hata siasa za Kibeberu, leo hii tunakubali kuburuzwa na Watanzania wenzetu ambao ni Watawala na Mabwana na si Viongozi?
Tunapokwenda kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa Serikali za Mitaa, diwani na meya tutakayemchagua tutampa mamlaka awe Mtawala, Bwana na Mnyapara au ni ndugu yetu tunayemuamini kuwa anajituma na kujitolea kutumia hekina na busara kutuongoza na kutetea haki zetu?
Na hata mwakani tutakapoanza kutafuta Wabunge, Wawakilishi na Marais wa Muungano na Zanzibar, tuko tayari kuanza kuwapima wanaotaka nafasi hizo kwa kuangalia kama kweli wana uwezo wa kuongoza au tutajinyong'onyea kwa unyonge na kuruhusu kutawaliwa na Mabwana Wakubwa ambao wao ni Mwanzo na Mwisho wa kila kitu na sisi hatuna hata sauti moja au kauli ila ni kusema "ndiyo mzee", "ndiyo bosi" "ndiyo mkubwa" na kuwa na nidhamu ya woga badala ya kuwa na heshima na kutembea kifua mbele tukijigamba kuwa tuna Viongozi wachapa kazi wenye kujali maslahi yetu kama Jamii na Taifa?
Je kizazi cha mababu zetu, mababa zetu na hata chetu cha sasa, hakina hata watu kumi ambao wanaweza kuwa na mfano chanya wa maana ya uongozi na hivyo kuliondoa Taifa letu kutoka unyonge wa kuwa watumwa na kunyanyaswa na kupuuzwa?
Hivi kweli ndani ya Bunge, hakuna watu weye Busara kumi ambao wanaweza kulonga na Bunge zima likaafiki kufanya mambo ya Busara na Hekima na si Ushabiki wa Pwagu na Pwaguzi?
Je kwenye bodi za menejimenti, hakuna wajumbe wenye msimamo na kauli ambao wanaweza kusimama kidete an kusema "hapa tumekosea" "lile halikuwa sahihi" "matumizi haya hayana manufaa" nao wakazikilizwa na kuheshimiwa na hivyo shirika, taasisi au jumuiya ikaonelea kuwa kuna umuhimu wa kujirudi na kujisahihisha?
Je tuende kuazima Viongozi kutoka kwa Wazungu, Warwanda na Wachina?
Ni lini tutaanza kuzalisha uzao wa Viongozi wenye maono, wachapakazi, jasiri, wabunifu, fanisi, wanyenyekevu, waadilifu, wakweli, wasiopenda makuu na wenye kuelewa maana ya Uongozi na umuhimu wa kuhamasisha na kutetea haki za jamii zao na si kujifikiria wao kwanza?
Mwisho, kwa walio madarakani, je wanaelewa kuwa mafanikio yanatokana na ushirikishi na kuaminika kutoka kwetu sisi Wananchi? Ikiwa Walioko juu tunaowaita Vigogo, Vibosile, Wakubwa, Pedeje, Wanene na Wenyewe hawatambui kuwa sisi tulio chini tuliowapa dhamana ya kuongoza ni muhimu na tuna thamani, kuna faida gani kuendelea kuwa na watu kama hao wanaodhani wao ni Miungu watu na kuwa Uongozi wa Taifa na Jamii yetu ni Urithi wao wa milele au hakuna mwingine zaidi yao?