Tanzania tumepigwa bao na Wakenya, Kiswahili is not the official language of EAC!

Kiswahili ni kizuri lakini kimedumaza sana watanzania to the outside world. Leo hii watu wanahitimu shahada zao hata kuandika barua ya kuomba kazi kwa kiingereza kilicho nyooka hapana. Nenda kawaweke wahitimu wetu na wa Ug na Kenya kwenye labour market wafanyiwe usaili utaona tunashindwa badly. Let us be honest jamani, achilia mbali EAC! Ni lini humu nchini watu wameomba kazi kwa Kiswahili? Ama umeenda usaili unaofanywa kwa kiswahili kwenye nyadhifa muhimu? Jibu hapana!
Mimi nafikiri, kama tayari tunakifahamu Kiswahili kwa ustadi kabisa kwanini basi tusihamie kujifunza lugha nyingine na kuitumia? Kwanini tung'ang'anie tu Kiswahili na tunakijua?
Kwa wale wanaotembea na kutafuta ajira ng'ambo wanaweza kukubaliana nami kuwa Nchi zote za kiarabu hususan U.A.E ( Umoja wa Falme za Kiarabu yenye Dubai na Abudhabi----), Qatar na nyinginezo zimetoa ajira sana kwa waafrika wengi wao wakiwa wakenya.
Hawa jamaa wako kila mahari mpaka karibuni wanafanya kazi kama walinzi ama security guard wakiwareplace wahindi na wapakistan, lakini kwanini waajiri wanawataka? Jibu kiingereza sababu kazi nyingine haziitaji elimu kubwa huko middle east bali ufahamu tu wakiingereza na wanaajiriwa. Sasa sisi bado tunalalamika - ni ujinga tu.
Jamaa wanaenda na wanaita ndugu zao, wako mahotelini mpaka top hotels in town wapo! Sisi twang'ang'ana na Kiswahili, jamaa wanaanza na security guard kesho unamuona ameingia sales keshokutwa anafanya jambo lingine! Tukisubiri serikali itufanyie tutabaki kulalama pasipo msaada!
Anyway let us wake up and run badala ya kuendelea kupiga mayowe ya usingizi wakati mda umeshasogea!!!
Mbona mie siwaelewi, hivi mnaongelea outside world ipi? kwa mfano Msumbiji hawajui kiingereza kabisa bora hata sie lakini mbona hawaoti kabisa kuamua kutumia kiingereza? nchi kama vile Korea, nchi za marekani ya kusini, Guinea, Ufilipino, vietnam hawajui kiingereza mbona naona bado hawawazi kuanza matumizi ya kiingereza? Tusidanganyane bwana watanzania kukosa exposure sio kwasababu ya lugha ni kutokana na mfumo ovyo wa ccm tangu zamani. nchi inaenda kwa propaganda na hivyo wananchi wamejaa hofu ktk kila kitu kiasi kwamba huwa hawathubutu kabisa. Nikupe mfano; kuna watanzania wengi wamekuwa wakizamia Afrika ya kusini huku hawajui kabisa kiswahili lakini wanaweza kufika na kufanya biashara hata kama wanakua wahamiaji haramu, sasa hao wanawezaje kama kiswahili ndo tatizo?
 
Mbona mie siwaelewi, hivi mnaongelea outside world ipi? kwa mfano Msumbiji hawajui kiingereza kabisa bora hata sie lakini mbona hawaoti kabisa kuamua kutumia kiingereza? nchi kama vile Korea, nchi za marekani ya kusini, Guinea, Ufilipino, vietnam hawajui kiingereza mbona naona bado hawawazi kuanza matumizi ya kiingereza? Tusidanganyane bwana watanzania kukosa exposure sio kwasababu ya lugha ni kutokana na mfumo ovyo wa ccm tangu zamani. nchi inaenda kwa propaganda na hivyo wananchi wamejaa hofu ktk kila kitu kiasi kwamba huwa hawathubutu kabisa. Nikupe mfano; kuna watanzania wengi wamekuwa wakizamia Afrika ya kusini huku hawajui kabisa kiswahili lakini wanaweza kufika na kufanya biashara hata kama wanakua wahamiaji haramu, sasa hao wanawezaje kama kiswahili ndo tatizo?

Mkuu ni colonial mentality period; kwa wa Tanzania kuifanya kiswahili lugha ya Taifa wanapata faida zaidi

a. Kitendo hicho kitaifanya nchi zote, makampuni na watu binafsi (watafiti) zinazotaka kufanya biashara na Tanzania kujifunza kiswahili kwanza hivyo kuongeza exposure, kazi na kufahamika kwa kiswahili duniani fikiria tuna watu mil.40..linganisha na watu mil1 wa ugiriki

b. Walimu na wataalamu wa kiswahili kuwa exported duniani kutoka Tanzania

c. Kuongeza uelewa wa masomo darasani kwa wanafunzi, kuongeza ufanisi na uwezo wa kisayansi...
etc

faida ni nyingi sana basi tu..sijui viongozi wetu wakoje..tired and sick
 
Mimi nakwambia kiwango cha kulalamika nchi hii kimefikia kwenye alarming stage. Kuna tatizo gani Kiingereza kuwa official language wakati population ya Kenya, Uganda na hapo baadae South Sudan hiyo ndiyo official language yao. Kwa nini tudhani kwamba Tanzania tuna haki ya ku-impose kile tunachokitaka? Kwanza kwa kusema official language kunabadilisha nini? Watu wa jumuiya watakuwa na uhuru wa kuwasiliana kwa lugha wanayoihitaji na kuelewana lakini majadiliano katika mijadala na mikusanyiko maalum itafanywa kwa kiingereza, kitu ambacho hata hapa Tanzania tunakifanya.

Hivi ni lazima mtu ulie lie hata kwa kitu ambacho siyo issue? Tumewachoka sasa!
hii ndiyo type ya watu tulio nao, hebu shangaa swala la utaifa mtu anasema kulialia.. hawajiulizi ukienda kusoma Japan/Ujerumani/China nk kuna mwaka mzima wa kujifunza lugha? Sasa EAC hatuna utaifa wetu zaidi ya kujikabidhi kwenye koloni la Uingereza na Mbopo unaona sawa tu. Wewe unawakilisha kundi kubwa la viongozi/watawala wasio na uzalendo maana uzalendo ni kulialia tu.. Umoja huu hautadumu maana una kasoro nyingi zenye maslahi kwa wajanja wachache hivyo itafika mahali wananchi wengi wataukataa tu..
 
Kwa nilivyosoma post zako nadhani hujanielewa, kimsingi niko pamoja nawe kimtazamo. Nilimaanisha kwanini sasa EAC isiwe na lugha official mbili kwa maana ya kiswahili na kiingereza. Hata hivyo nchi zenye lugha official zaidi ya moja ninazozifahamu ni: Cameroon, South Africa, Canada,Eritrea na DRC
Nimekuelewa sana na ndio maana nikataka tu nawe ufute wazo hata la lugha mbili official kwa sababu nchi zote ulizozitaja wananchi wake wanaongea lugha mbili miaka yote...Yaani kuna matabaka mawili ya makabila au ndio unazungumzia kukoloniwa na ukitazama koloni hizo walilazimishwa kuzikataa lugha zao na kutumia lugha za kigeni hivyo wananchi wake na kizazi kilichofuata walizungumza na kuwasiliana kwa lugha hizo. Hivyo matumizi ya lugha hizo kuna historia nyuma yake..

Canada kuna lugha mbili official kwa sababu wananchi wake wanawasiliana ktk lugha hizo mbili bila hata kuwa official toka miaka na miaka hivyo zinakuwepo lugha mbili kwa sababu ya watu wake. Tofauti na sisi ambao tunataka ku import lugha ambayo wananchi wake hawaizungumzi wala hawafanyi mawasiliano yao kwa lugha hiyo na hakuna sababu za maana kabisa zaidi ya kufikiria nje ya mipaka yetu yaani hiyo lugha itujenge sisi tuwe jamii ya aina fulani (Limbukeni) krtk mawasiliano..

Bahati mbaya leo badala ya kiingereza kuwa lugha imekuwa ndio ELIMU na vijana wetu wanaposhindwa mitihani tusitake kuwalalamikia walimu ama vijana wenyewe kwa sababu maamuzi yetu ndio yamefanya mtoto anayejua Serengeti ni mbuga ya wanyama lakini hajui kama ni ecosystem kwa sababu hajui ecosystem ni madudu gani.
 
Back
Top Bottom