TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 4,973
- 15,304
Nimejaribu kufanya tathmini ya maisha tunayoishi watanzania wa leo nikajaribu kukumbuka somo la historia na nimegundua system ya maisha na uongozi wetu unafanana kwa kiasi kikubwa na middle ages (miaka ya 1400) kule ulaya. Kipindi hicho, watawala walikua wanawagawia mashamba marafiki zao (feudal lords) ambao nao waliyatumia kuwanyonya wanyonge. Viongozi na watawala walitajirika kwa kujilimbikizia mali zilizotokana na kodi za wananchi wanyonge hivyo kuwawezesha kuishi maisha ya kifahari! Enzi hizo, hakukuwa na demokrasia na wale wote walioonekana kupingana na utawala walikiona. Sasa fananisha na viongozi wa tz, tafakari, chukua hatua.