Tanzania tuiunge mkono Iran katika mpango wa Nuclear

Zawadi Ngoda

JF-Expert Member
Aug 13, 2009
3,804
1,871
Habari kuwa tatizo la umeme Tanzania ni sugu, sikulipokea kwa mshangao hata kidogo. Picha ya tatizo hili nililielewa pale Rais mstaafu Mwinyi akiwa madarakani, alipolieleza tatizo kama limetokana na upingufu wa maji katika mto Ruvu. Ama wengine wakaeleza kuwa matope yamejaa katika mto huo. Yote hayo kwangu yalikuwa ni majibu ya kisiasa.

Katika nchi zilizoendelea asilimia 80 ya umeme wao hutokana na Nuclear energy. Na katika chanzo hicho cha umeme ndio unaaweza kupata umeme rahisi na imara. Ni kitu cha ajabu sana hawa hawa watu wanapokuja kueleza maaendeleo katika nchi zetu, hufurahia tu pale wanaposema 5% tu ya watanzania wana acces ya umeme. Lakini kuja na maelezo ni jinsi gani wao waliondokana na adha hiyo hawapendi kabisa kujadili. Lazima tujiulize ni kwanini? Je wanatutakia mema?

Pindi nchi zinazoendelea zinapojitosa katika Nuclear power, basi zitasakamwa na kutishiwa kupigwa mabomu. Iran ni moja kati ya nchi zinazoendelea ambazo hazikujali vitisho, na bila majadiliano ikajenga mtambo wa Nuclear kwa matumizi ya amani. Sakata lake limechukua zaidi ya miaka 20, kusakamwa na kutishiwa kila leo. Kibaya zaidi ni kuona nchi zinzoendelea zikaungana mkono na nchi zilizoendelea kama Marekani, Israel na Uingereza kuisakama Iran. Eti kisa ni kutoiruhusu Iran kuwa na Bomu la Nuclear. Lakini "National Convention On Nuclear Power" imeweka wazi katika Article 1, kama ninavyoinukuu hapa chini:

"ARTICLE 1. OBJECTIVES
The objectives of this Convention are to:
a. Accelerate the expansion of nuclear power in industrialized nations
and in the developing areas of the world;
b. Assure that peaceful uses of nuclear energy do not further the
proliferation of nuclear weapons, by providing assured supplies of
specified goods and services including those capable of supporting
the proliferation of nuclear weapons
;
c. Protect against nuclear terrorism involving the potential sabotage of
nuclear installations or transport systems or the theft of nuclear
material or hazardous radioactive materials; and
d. Maintain high safety standards and efficiency and operational
performance."
Soma convention nzima katika www.pysics.havard.edu/~wilson/energypmp/nuclear-forum.pdf

Soma vizuri hicho kipengele "b" kimeeleza wazi kuwa kuwa kila nchi duniani ina haki ya kuwa na Nuclear Energy kwa matumizi ya amani. Sasa iweje hawa hawa wakubwa walioandika hii convention wanaipinga na nchi nyingine sizizoendelea nazo eti zinaunga mkono licha ya kufahamu kipengele hicho.

Mimi nafikiri, nchi zisizoendelea ni lazima zishikamane kuiunga mkono Iran na kuzishinda nchi zilizoendelea. Kama Iran ikifanikiwa basi itakuwa rahisi kwetu kuleta ajenda kama hiyo na ikapita. Kuiunga mkono Iran, hatutafanya hivyo kwa faida ya Iran, bali kwa Faida yetu wenyewe. Waswahili wanasema, mwenzako akinyolewa wewe tayarisha kichwa chako. Kwa hiyo kabla hatujatayarisha vichwa vyetu ni lazima tuhakikishe kuwa kichwa cha Iran hakijanyolewa.

Tatizo la umeme Tanzania na nchi nyingine za Afrika litatoweka pale Afrika tutapokuwa na umeme utokanao na Nuclear. Nchi nyingi za Afrika kama Kenya, Uganda, Angola n.k zimeshaanza kudokeza hayo katika level ya kitaifa. Lakini lazima ieleweke kuwa hiyo sio kazi rahisi, si katika kuipata Teknolojia hiyo bali kwa nchi mabeberu kutukubalia. Na hii itawezekana pale nchi zote zinazoendelea kuwa na lao moja katika hili la Nuclear Energy kwa matumizi ya amani.

Nilitarajia katika mkutano wa UN safari hii, mwenyekiti wa African Union angeliongelea hili, lakini haikuwa hivyo. Ninamuelewa Gadafi anapopata frastratio na kichefu chefu akiisoma Charter ya UN na kuichana na kuitupa. Hii ni kwa sababu Charter hiyo ina double standards. Hiyoa haiwezi kutufujisha popote pale.

Tuungane kupigania kupata Nuclear Energy kwa matumizi ya amani, ili tukuze uchumi wetu. Huwezi kumuita muwekezaji katika hali ya umeme wa mgao. Hapa hatupo makini.
 
Habari kuwa tatizo la umeme Tanzania ni sugu, sikulipokea kwa mshangao hata kidogo. Picha ya tatizo hili nililielewa pale Rais mstaafu Mwinyi akiwa madarakani, alipolieleza tatizo kama limetokana na upingufu wa maji katika mto Ruvu. Ama wengine wakaeleza kuwa matope yamejaa katika mto huo. Yote hayo kwangu yalikuwa ni majibu ya kisiasa.

Katika nchi zilizoendelea asilimia 80 ya umeme wao hutokana na Nuclear energy. Na katika chanzo hicho cha umeme ndio unaaweza kupata umeme rahisi na imara. Ni kitu cha ajabu sana hawa hawa watu wanapokuja kueleza maaendeleo katika nchi zetu, hufurahia tu pale wanaposema 5% tu ya watanzania wana acces ya umeme. Lakini kuja na maelezo ni jinsi gani wao waliondokana na adha hiyo hawapendi kabisa kujadili. Lazima tujiulize ni kwanini? Je wanatutakia mema?

Pindi nchi zinazoendelea zinapojitosa katika Nuclear power, basi zitasakamwa na kutishiwa kupigwa mabomu. Iran ni moja kati ya nchi zinazoendelea ambazo hazikujali vitisho, na bila majadiliano ikajenga mtambo wa Nuclear kwa matumizi ya amani. Sakata lake limechukua zaidi ya miaka 20, kusakamwa na kutishiwa kila leo. Kibaya zaidi ni kuona nchi zinzoendelea zikaungana mkono na nchi zilizoendelea kama Marekani, Israel na Uingereza kuisakama Iran. Eti kisa ni kutoiruhusu Iran kuwa na Bomu la Nuclear. Lakini "National Convention On Nuclear Power" imeweka wazi katika Article 1, kama ninavyoinukuu hapa chini:

"ARTICLE 1. OBJECTIVES
The objectives of this Convention are to:
a. Accelerate the expansion of nuclear power in industrialized nations
and in the developing areas of the world;
b. Assure that peaceful uses of nuclear energy do not further the
proliferation of nuclear weapons, by providing assured supplies of
specified goods and services including those capable of supporting
the proliferation of nuclear weapons;
c. Protect against nuclear terrorism involving the potential sabotage of
nuclear installations or transport systems or the theft of nuclear
material or hazardous radioactive materials; and
d. Maintain high safety standards and efficiency and operational
performance."
Soma convention nzima katika www.pysics.havard.edu/~wilson/energypmp/nuclear-forum.pdf

Soma vizuri hicho kipengele "b" kimeeleza wazi kuwa kuwa kila nchi duniani ina haki ya kuwa na Nuclear Energy kwa matumizi ya amani. Sasa iweje hawa hawa wakubwa walioandika hii convention wanaipinga na nchi nyingine sizizoendelea nazo eti zinaunga mkono licha ya kufahamu kipengele hicho.

Mimi nafikiri, nchi zisizoendelea ni lazima zishikamane kuiunga mkono Iran na kuzishinda nchi zilizoendelea. Kama Iran ikifanikiwa basi itakuwa rahisi kwetu kuleta ajenda kama hiyo na ikapita. Kuiunga mkono Iran, hatutafanya hivyo kwa faida ya Iran, bali kwa Faida yetu wenyewe. Waswahili wanasema, mwenzako akinyolewa wewe tayarisha kichwa chako. Kwa hiyo kabla hatujatayarisha vichwa vyetu ni lazima tuhakikishe kuwa kichwa cha Iran hakijanyolewa.

Tatizo la umeme Tanzania na nchi nyingine za Afrika litatoweka pale Afrika tutapokuwa na umeme utokanao na Nuclear. Nchi nyingi za Afrika kama Kenya, Uganda, Angola n.k zimeshaanza kudokeza hayo katika level ya kitaifa. Lakini lazima ieleweke kuwa hiyo sio kazi rahisi, si katika kuipata Teknolojia hiyo bali kwa nchi mabeberu kutukubalia. Na hii itawezekana pale nchi zote zinazoendelea kuwa na lao moja katika hili la Nuclear Energy kwa matumizi ya amani.

Nilitarajia katika mkutano wa UN safari hii, mwenyekiti wa African Union angeliongelea hili, lakini haikuwa hivyo. Ninamuelewa Gadafi anapopata frastratio na kichefu chefu akiisoma Charter ya UN na kuichana na kuitupa. Hii ni kwa sababu Charter hiyo ina double standards. Hiyoa haiwezi kutufujisha popote pale.

Tuungane kupigania kupata Nuclear Energy kwa matumizi ya amani, ili tukuze uchumi wetu. Huwezi kumuita muwekezaji katika hali ya umeme wa mgao. Hapa hatupo makini.


Tatizo maraisi wa afrika ni submissive sana , zaidi ya afrika ya kusini sidhani kama kuna nchi nyingine yenye nuclear energy.Nasiki arusha wanajenga research center ya nuclear sijui wale wanaojua, imefika wapi sasa au ulikuwa utai tu
 
Katika nchi zilizoendelea asilimia 80 ya umeme wao hutokana na Nuclear energy. Na katika chanzo hicho cha umeme ndio unaaweza kupata umeme rahisi na imara. Ni kitu cha ajabu sana hawa hawa watu wanapokuja kueleza maaendeleo katika nchi zetu, hufurahia tu pale wanaposema 5% tu ya watanzania wana acces ya umeme. Lakini kuja na maelezo ni jinsi gani wao waliondokana na adha hiyo hawapendi kabisa kujadili. Lazima tujiulize ni kwanini? Je wanatutakia mema?
Tafadhali sana acha kujumuisha mambo kwa nia ya kuongopea watu na hizo takwimu zako!! Nchi zilizoendelea zipi hizo na ni zipi zinazotegemea umeme wa nyuklia kwa asilimia 80?! Acha kuongea kwa hisiahisia kwa lengo la kutuposha. Nchi nijuayo inategemea umeme kwa 80% kwa Europe ni France (http://www.energypolicyblog.com/?p=187). Tutajie nchi nyingine basi katika hizo nchi zilizoendelea...


www.pysics.havard.edu/~wilson/energypmp/nuclear-forum.pdf

[/I]Soma vizuri hicho kipengele "b" kimeeleza wazi kuwa kuwa kila nchi duniani ina haki ya kuwa na Nuclear Energy kwa matumizi ya amani. Sasa iweje hawa hawa wakubwa walioandika hii convention wanaipinga na nchi nyingine sizizoendelea nazo eti zinaunga mkono licha ya kufahamu kipengele hicho.

Mimi nafikiri, nchi zisizoendelea ni lazima zishikamane kuiunga mkono Iran na kuzishinda nchi zilizoendelea. Kama Iran ikifanikiwa basi itakuwa rahisi kwetu kuleta ajenda kama hiyo na ikapita. Kuiunga mkono Iran, hatutafanya hivyo kwa faida ya Iran, bali kwa Faida yetu wenyewe. Waswahili wanasema, mwenzako akinyolewa wewe tayarisha kichwa chako. Kwa hiyo kabla hatujatayarisha vichwa vyetu ni lazima tuhakikishe kuwa kichwa cha Iran hakijanyolewa.
Emotions!

Tatizo la umeme Tanzania na nchi nyingine za Afrika litatoweka pale Afrika tutapokuwa na umeme utokanao na Nuclear. Nchi nyingi za Afrika kama Kenya, Uganda, Angola n.k zimeshaanza kudokeza hayo katika level ya kitaifa. Lakini lazima ieleweke kuwa hiyo sio kazi rahisi, si katika kuipata Teknolojia hiyo bali kwa nchi mabeberu kutukubalia. Na hii itawezekana pale nchi zote zinazoendelea kuwa na lao moja katika hili la Nuclear Energy kwa matumizi ya amani.

Nilitarajia katika mkutano wa UN safari hii, mwenyekiti wa African Union angeliongelea hili, lakini haikuwa hivyo. Ninamuelewa Gadafi anapopata frastratio na kichefu chefu akiisoma Charter ya UN na kuichana na kuitupa. Hii ni kwa sababu Charter hiyo ina double standards. Hiyoa haiwezi kutufujisha popote pale.

Tuungane kupigania kupata Nuclear Energy kwa matumizi ya amani, ili tukuze uchumi wetu. Huwezi kumuita muwekezaji katika hali ya umeme wa mgao. Hapa hatupo makini.
Vyanzo vya maji vipo, gesi ipo, jua lipo, upepo upo, mawimbi ya bahari yapo, chemchemi zipo, hata mafuta yanasemekana yapo! Lakini umeme uzalishwao nchini hautoshelezi hata hiyo asilimia 12 ya wale waliounganishwa kwenye gridi. Leo hii unaanza kuongelea nyuklia na kuwalaumu western.

Nimependa sana kipengele cha mwisho ulichomalizia. NI KWELI - huwezi kuita wawekezaji katika madini na miradi mingine mikubwa kitaifa huku umeme ni wa mgao. Chakushangaza, Mh. Rais wetu ndicho hicho alichofanya au jaribu kukifanya katika kipindi hiki chote.

Swala la umeme kwa kipindi cha miaka minne aliyoongoza nchi hii angedhamiria angelitatua takribani ndani ya miaka mitatu tu. Wanunuzi wa umeme wapo, malighafi ya uzalishaji umeme ipo, uzalishaji hamna lakini anaenda kualika watumiaji wakubwa wa umeme badala ya kualika wawekezaji wanaofahamika katika maswala ya umeme na siyo wapuuzi puuzi tu kama Richmond waliotuletea.

Mfano, kanda ya ziwa, kuna mahitaji ya umeme yameongezeka kwa sababu uzalishaji uliopo wa 60MW hautoshelezi kutokana na mgodi wa dhahabu ulioanzishwa hivi karibuni. Tungelikuwa tunatumia vichwa vyetu ipasavyo, kwanini tusingetafuta wazalishaji umeme kwanza kabla ya kuleta watumiaji? Halafu leo hii kutokana na uzembe wa viongozi wetu katika ku-priotize mambo ya maendeleo unaanza kuongelea nyuklia, tume-exhaust vyanzo vya nishati vilivyopo?!

Tumeshindwa kumtambua mmiliki wa Dowans au aliyerudisha pale BoT junia la pesa za Kagoda, unategemea tutakuwa na wanasayansi au vyombo vya sheria kuweza kujua ni nani ametorosha kilo moja ya plutonium kutoka kiwandani??!! Kwa Tanzania yetu pendwa, hii hoja umewahisha kuileta kwa zaidi ya miaka 120 au zaidi!!!
 
Tafadhali sana acha kujumuisha mambo kwa nia ya kuongopea watu na hizo takwimu zako!! Nchi zilizoendelea zipi hizo na ni zipi zinazotegemea umeme wa nyuklia kwa asilimia 80?! Acha kuongea kwa hisiahisia kwa lengo la kutuposha. Nchi nijuayo inategemea umeme kwa 80% kwa Europe ni France (http://www.energypolicyblog.com/?p=187). Tutajie nchi nyingine basi katika hizo nchi zilizoendelea...



Emotions!


Vyanzo vya maji vipo, gesi ipo, jua lipo, upepo upo, mawimbi ya bahari yapo, chemchemi zipo, hata mafuta yanasemekana yapo! Lakini umeme uzalishwao nchini hautoshelezi hata hiyo asilimia 12 ya wale waliounganishwa kwenye gridi. Leo hii unaanza kuongelea nyuklia na kuwalaumu western.

Nimependa sana kipengele cha mwisho ulichomalizia. NI KWELI - huwezi kuita wawekezaji katika madini na miradi mingine mikubwa kitaifa huku umeme ni wa mgao. Chakushangaza, Mh. Rais wetu ndicho hicho alichofanya au jaribu kukifanya katika kipindi hiki chote.

Swala la umeme kwa kipindi cha miaka minne aliyoongoza nchi hii angedhamiria angelitatua takribani ndani ya miaka mitatu tu. Wanunuzi wa umeme wapo, nishati ya umeme ipo, uzalishaji hamna lakini anaenda kualika watumiaji wakubwa wa umeme badala ya kualika wawekezaji wanaofahamika katika maswala ya umeme na siyo wapuuzi puuzi tu kama Richmond waliotuletea.

Mfano, kanda ya ziwa, kuna mahitaji ya umeme yameongezeka kwa sababu uzalishaji uliopo wa 60MW hautoshelezi kutokana na mgodi wa dhahabu ulioanzishwa hivi karibuni. Tungelikuwa tunatumia vichwa vyetu ipasavyo, kwanini tusingetafuta wazalishaji umeme kwanza kabla ya kuleta watumiaji? Halafu leo hii kutokana na uzembe wa viongozi wetu katika ku-priotize mambo ya maendeleo unaanza kuongelea nyuklia, tume-exhaust nishati zilizopo?!

Tumeshindwa kumtambua mmiliki wa Dowans au aliyerudisha pale BoT junia la pesa za Kagoda, unategemea tutakuwa na wanasayansi au vyombo vya sheria kuweza kujua ni nani ametorosha kilo moja ya plutonium kutoka kiwandani??!! Kwa Tanzania yetu pendwa, hii hoja umewahisha kuileta kwa zaidi ya miaka 120!!!


Si ndo hapo watu wanakimbilia nuclear na wakati uwezo wa kutengeneza umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo vya nature vipo. Stat aliyotoa Zitto imeniua...12% ya nchi ndo yenye umeme. Na bado kwa huo tunakuwa na mgao. Umeme kwetu bado ni privileged na sio haki.
Na kinachoboa zaidi, Dowans analipwa pesa kila siku, lakini hatujui hiyo pesa inaenda wapi! Ivi rais amelala au vipi? Wamefutanya mafala sasa...
 
Sijasoma hiyo post yako nzima, but nakubali kuwa nuclear ndo suluhisho la matatizo ya energy duniani. Lakini kwa hapa bongo haitawezekana kabisa, lazima watapiga panga bajeti ya safety equipment tufe wote.

Bora umeweka hiyo LAKINI!

Solid waste

For more details on this topic, see Radioactive waste.

The safe storage and disposal of nuclear waste is a significant challenge and yet unresolved problem. The most important waste stream from nuclear power plants is spent fuel. A large nuclear reactor produces 3 cubic metres (25–30 tonnes) of spent fuel each year.[68] It is primarily composed of unconverted uranium as well as significant quantities of transuranic actinides (plutonium and curium, mostly). In addition, about 3% of it is made of fission products. The actinides (uranium, plutonium, and curium) are responsible for the bulk of the long term radioactivity, whereas the fission products are responsible for the bulk of the short term radioactivity.[69]

High-level radioactive waste


Spent fuel is highly radioactive and needs to be handled with great care and forethought. However, spent nuclear fuel becomes less radioactive over the course of thousands of years of time. After about 5 percent of the rod has reacted the rod is no longer able to be used. Today, scientists are experimenting on how to recycle these rods to reduce waste. In the meantime, after 40 years, the radiation flux is 99.9% lower than it was the moment the spent fuel was removed, although still dangerously radioactive.[59]

Spent fuel rods are stored in shielded basins of water (spent fuel pools), usually located on-site. The water provides both cooling for the still-decaying fission products, and shielding from the continuing radioactivity. After a few decades some on-site storage involves moving the now cooler, less radioactive fuel to a dry-storage facility or dry cask storage, where the fuel is stored in steel and concrete containers until its radioactivity decreases naturally ("decays") to levels safe enough for other processing. This interim stage spans years or decades or millennia, depending on the type of fuel. Most U.S. waste is currently stored in temporary storage sites requiring oversight, while suitable permanent disposal methods are discussed.

As of 2007, the United States had accumulated more than 50,000 metric tons of spent nuclear fuel from nuclear reactors.[70] Underground storage at Yucca Mountain nuclear waste repository in U.S. has been proposed as permanent storage. After 10,000 years of radioactive decay, according to United States Environmental Protection Agency standards, the spent nuclear fuel will no longer pose a threat to public health and safety.[citation needed]

The amount of waste can be reduced in several ways, particularly reprocessing. Even so, the remaining waste will be substantially radioactive for at least 300 years even if the actinides are removed, and for up to thousands of years if the actinides are left in.

Source: http://en.wikipedia.org/wiki/Nuclear_power

Kwa yale yote niliyokwisha jisomea na kuyasikia, siwezi nika endorse nuclear power kuwa ndiyo suluhisho la matatizo ya umeme duniani. Nakubali kwamba matumizi ya nuclear yata/yanasaidia kupunguza kwa kiwango fulani utegemezi wa uzalishaji umeme kutoka vyanzo vyenye CO2 emission kubwa. Pia nakubali kuendelea kuwepo kwa matumizi ya nuclear kwenye mambo mbalimbali ya kisayansi.

Iceland mbona wameweza kuwa na 100% renewable energy, soma hapa: http://www.verneglobal.com/icelandic_advantage/energy. Jua la Dodoma na Singida tungelikuwa watu wakuchunguza kisayansi na kupenda maendeleo ya jamii yetu, huchelewi kukuta sasa hivi lingekuwa linatupatia walau 1/5 ya mahitaji yetu ya umeme.

Katika hili la Tanzania kuanza kwenda kwenye nuclear power wakati hata kumudu tu vyanzo vya maji tulivyo navyo, na maliasiri nyinginezo nyingi zenye kuweza kutuletea au kuwa vyanzo vya umeme kumetushinda, ni ulimbukeni wa mambo. Hata hivyo kuwepo kwa research institute kwa ajili ya mambo ya kisayansi na kwa ajili ya kuelimisha watu ni jambo jema na lakuendelezwa. Lakini kuanza ku-prioritize nuclear energy wakati hatujui mmiliki wa Dowans ni utekelezaji wa 'miafrika ndivyo tulivyo'. Na inavyoonekana FORETHOUGHT yetu katika mambo mengi kwa tathmini ya matatizo ambayo tuliyonayo tayari na tumeshindwa kuyatatua ni asilimia ndogo!!!
 
Sakata la Iran kuwa na Nuclear power energy kwa matumizi ya amani, limezua mgogoro mkubwa wa kisiasa katika mataifa makubwa. Lakini Tanzania inasemaje juu ya mpango huo wa Iran? Hili ndio suala linaloniumiza kichwa, na ninaimani kuwa mimi si pekee niliyeguswa na hili.

Nchi zote zilizoendelea hutumia umeme wa nuclear kukidhi mahitaji yao ya umeme katika viwanda na matumizi ya watu binafsi. Umeme wa maji na mafuta (dizeli) haukidhi mahitaji makubwa kama hayo, isitoshe ni gharama kubwa. Na katika mantiki hii, ndio maana nchi nyingi zinazoendelea kama Iran, pakistan, India n.k zimepata wazo la kuziuata nchi hizo ziliziendelea katika kutatua matatizo yao ya nishati kwa kuendeleza teknolojia ya Nuclear. Maendeleo haya yamepingwa vikali sana na nchi zilizoendelea, hata Marekani na Israel kwenda mbali zaidi na kutishia kuishambulia Iran.

Thomas E Shea, PhD wa World Nuclear University ameguswa na swala hili na ameandika ifuatavyo katika
Author's Note
"How much nuclear power will be needed to meet mankind's needs for an abundant
and reliable source of electricity, potable water, and process heat, while staving
off carbon-induced environmental calamity? What are the barriers to the global
expansion of nuclear power, especially to countries not currently operating
nuclear power plants, and how could those barriers best be overcome to
accelerate the responsible, safe and secure use of nuclear power?"


Na katika maana hiyo ya ujenzi wa Nuclear power kwa matumizi ya amani, ndio msimamo wa Iran katika utetezi wake. Na katika National Convention On Nuclear Power, imeelezwa wazi kuwa kila nchi inaruhusiwa kujenga mtambo wa Nuclear kwa matumizi ya amani. Hii unaweza kuisoma katika Article No 1, inayosomeke kama ifuatavyo (zingatia kipengele "b"):

"ARTICLE 1. OBJECTIVES
The objectives of this Convention are to:
a. Accelerate the expansion of nuclear power in industrialized nations
and in the developing areas of the world;
b. Assure that peaceful uses of nuclear energy do not further the
proliferation of nuclear weapons, by providing assured supplies of
specified goods and services including those capable of supporting
the proliferation of nuclear weapons;

c. Protect against nuclear terrorism involving the potential sabotage of
nuclear installations or transport systems or the theft of nuclear
material or hazardous radioactive materials; and
d. Maintain high safety standards and efficiency and operational
performance."
Angalia conventional nzima katika www.pysics.havard.edu/~wilson/energypmp/nuclear-forum.pdf

Kwa maana hiyo naona Tanzania ina kila sababu ya kuiunga mkono Iran katika mpango mzima wa Nuclear kwa matumizi ya amani. Nchi yetu ina sababu kubwa mbili za kuiunga mkono Iran: Kwanza ni kuhakikisha kuwa hakuna double standard katika katika sheria za kimataifa. Pili ushindi wa Iran utafungua wigo wa nchi zinazoendelea kupata teknolojia hiyo muhimu ambayo ndio utatuzi wa kweli wa matatizo ya umeme katika nchi yetu. Hii inamaana kubwa sana, kwani ikiwa Iran itafanikiwa, huko mbeleni nchi zote zinazoendelea hazitapata shinyikizo kama inayopata Iran leo hii. Hivyo itarahisisha usambazaji wa teknolojia hiyo duniani na kupunguza umasikini.

Tanzania kuinga mkono Iran, iwe kama mbinu (strategy) mzunguko (indirect) katika kujiwekezea kwa baadae kuipata teknolojia hiyo. Mpaka leo nchi kama Kenya, Nigeria, Uganda, Angola n.k zimeshaonyesha nia ya kupata Teknolojia hiyo.
 
Umesha waunga mkono inatosha .Si lazima tutangaze kama Taifa maana hatuna faida na Nuclear yao wale wana mambo yao mbona hawa tuungi mkono kupambana na mafisaidi Tanzania ?
 
Sakata la Iran kuwa na Nuclear power energy kwa matumizi ya amani, limezua mgogoro mkubwa wa kisiasa katika mataifa makubwa. Lakini Tanzania inasemaje juu ya mpango huo wa Iran? Hili ndio suala linaloniumiza kichwa, na ninaimani kuwa mimi si pekee niliyeguswa na hili.

Nchi zote zilizoendelea hutumia umeme wa nuclear kukidhi mahitaji yao ya umeme katika viwanda na matumizi ya watu binafsi. Umeme wa maji na mafuta (dizeli) haukidhi mahitaji makubwa kama hayo, isitoshe ni gharama kubwa. Na katika mantiki hii, ndio maana nchi nyingi zinazoendelea kama Iran, pakistan, India n.k zimepata wazo la kuziuata nchi hizo ziliziendelea katika kutatua matatizo yao ya nishati kwa kuendeleza teknolojia ya Nuclear. Maendeleo haya yamepingwa vikali sana na nchi zilizoendelea, hata Marekani na Israel kwenda mbali zaidi na kutishia kuishambulia Iran.

Thomas E Shea, PhD wa World Nuclear University ameguswa na swala hili na ameandika ifuatavyo katika
Author’s Note
"How much nuclear power will be needed to meet mankind’s needs for an abundant
and reliable source of electricity, potable water, and process heat, while staving
off carbon-induced environmental calamity? What are the barriers to the global
expansion of nuclear power, especially to countries not currently operating
nuclear power plants, and how could those barriers best be overcome to
accelerate the responsible, safe and secure use of nuclear power?"

Na katika maana hiyo ya ujenzi wa Nuclear power kwa matumizi ya amani, ndio msimamo wa Iran katika utetezi wake. Na katika National Convention On Nuclear Power, imeelezwa wazi kuwa kila nchi inaruhusiwa kujenga mtambo wa Nuclear kwa matumizi ya amani. Hii unaweza kuisoma katika Article No 1, inayosomeke kama ifuatavyo (zingatia kipengele "b"):

"ARTICLE 1. OBJECTIVES
The objectives of this Convention are to:
a. Accelerate the expansion of nuclear power in industrialized nations
and in the developing areas of the world;
b. Assure that peaceful uses of nuclear energy do not further the
proliferation of nuclear weapons, by providing assured supplies of
specified goods and services including those capable of supporting
the proliferation of nuclear weapons;
c. Protect against nuclear terrorism involving the potential sabotage of
nuclear installations or transport systems or the theft of nuclear
material or hazardous radioactive materials; and
d. Maintain high safety standards and efficiency and operational
performance."
Angalia conventional nzima katika www.pysics.havard.edu/~wilson/energypmp/nuclear-forum.pdf

Kwa maana hiyo naona Tanzania ina kila sababu ya kuiunga mkono Iran katika mpango mzima wa Nuclear kwa matumizi ya amani. Nchi yetu ina sababu kubwa mbili za kuiunga mkono Iran: Kwanza ni kuhakikisha kuwa hakuna double standard katika katika sheria za kimataifa. Pili ushindi wa Iran utafungua wigo wa nchi zinazoendelea kupata teknolojia hiyo muhimu ambayo ndio utatuzi wa kweli wa matatizo ya umeme katika nchi yetu. Hii inamaana kubwa sana, kwani ikiwa Iran itafanikiwa, huko mbeleni nchi zote zinazoendelea hazitapata shinyikizo kama inayopata Iran leo hii. Hivyo itarahisisha usambazaji wa teknolojia hiyo duniani na kupunguza umasikini.

Tanzania kuinga mkono Iran, iwe kama mbinu (strategy) mzunguko (indirect) katika kujiwekezea kwa baadae kuipata teknolojia hiyo. Mpaka leo nchi kama Kenya, Nigeria, Uganda, Angola n.k zimeshaonyesha nia ya kupata Teknolojia hiyo.


Mode hamisha hii peleka kule kwenye International naona huyu kaanza zake
 
Umesha waunga mkono inatosha .Si lazima tutangaze kama Taifa maana hatuna faida na Nuclear yao wale wana mambo yao mbona hawa tuungi mkono kupambana na mafisaidi Tanzania ?

Madogo tuliyonayo bado hatujayamaliza,kujitakia makubwa ya nini?tunayo gas kibao kule mtwara haina hata mtumiaji,tukiamua inaweza kutosha kuhudumia Dar yote kwa umeme.Mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe.
 
Hatujawahi kuona Iran ikituunga mkono kwa lolote lenye maslahi kwetu! Sisi tuwaunge mkono kwa ajili ya nini? Si kutafuta ugomvi usio na sababu toka nchi nyingine na kuongeza matatizo kwenye yale ambayo tayari tunayo na kuifanya nchi iwe kama ya Mugabe ambayo inflation ilifikia 100,000%? Ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo usirushe mawe!
 
Hatujawahi kuona Iran ikituunga mkono kwa lolote lenye maslahi kwetu! Sisi tuwaunge mkono kwa ajili ya nini? Si kutafuta ugomvi usio na sababu toka nchi nyingine na kuongeza matatizo kwenye yale ambayo tayari tunayo na kuifanya nchi iwe kama ya Mugabe ambayo inflation ilifikia 100,000%? Ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo usirushe mawe!
Soma Thread vizuri na uielewe.

Nimeandika wazi sababu za kuiunga mkono, ikiwa kama Strategy. Ili huko mbele itusaidie kupata teknolojia hiyo kirahisi.

Soma tena Thread.
 
Umesha waunga mkono inatosha .Si lazima tutangaze kama Taifa maana hatuna faida na Nuclear yao wale wana mambo yao mbona hawa tuungi mkono kupambana na mafisaidi Tanzania ?
Haitoshi, kwa vile haitasaidia kwa mtu binafsi kuwaunga mkono. Lakini kama nchi ikiingilia ndio tutafaidika, kwa kile nilichokiita kama mbinu ya kijanja (strategy).
 
Soma Thread vizuri na uielewe.

Nimeandika wazi sababu za kuiunga mkono, ikiwa kama Strategy. Ili huko mbele itusaidie kupata teknolojia hiyo kirahisi.

Soma tena Thread.

sababu peke yake hazitutoshi kujiingiza kwenye matatizo yasiyo na msingi,angalia na negative impact yake ambayo ni kubwa zaidi.tuache tuendelea na kilimo kwanza yetu.
 
Hatujawahi kuona Iran ikituunga mkono kwa lolote lenye maslahi kwetu! Sisi tuwaunge mkono kwa ajili ya nini? Si kutafuta ugomvi usio na sababu toka nchi nyingine na kuongeza matatizo kwenye yale ambayo tayari tunayo na kuifanya nchi iwe kama ya Mugabe ambayo inflation ilifikia 100,000%? Ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo usirushe mawe!

Pengine rais wao hajui hata kama kuna taifa linaitwa Tz!

Soma Thread vizuri na uielewe.

Nimeandika wazi sababu za kuiunga mkono, ikiwa kama Strategy. Ili huko mbele itusaidie kupata teknolojia hiyo kirahisi.

Soma tena Thread.

ukitaka nuclear wewe ni rahisi sana hauhitaji kuunga mkono Iran, huna tatizo na threat za Iran katika sayari hii. Issue za USA na iran hazijaanza leo wala jana mkuu.

hata leo ukisema uanzishe hakuna atakayekuuliza, hatuna tunayemtisha dunia hii.

Ila ukiunga mkono Iran, then utaleta picha na sura mpya.
 
Achana na geopolitics!Tuna matatizo kibao bongo,ya kwetu!Tunalichangia Freedom struggle nchi za kusini mwa afrika,hakuna tulichopata!Ukienda South africa ,they dont care kama wewe ni mtanzania!!!!!!!!Weusi wenzako mtaani wanakubagua!!!!!!

Tufight mafisadi kwanza,hii kujali mambo ya Irani,ni siasa duni za kibongo
 
................Nadhani hoja iwe kwa Tanzania kufikiria matumizi ya nuklia ktk nishati katika siku za usoni. Sioni haja ya kuanza kwa kuunga mkono Iran!!!
 
Yaani Iran pamoja na ukichaa wa uongozi wake na historia yake ya kupenda vita bado tuna entertain wapate nuclear? Tunataka nini, waanzishe nuclear war?
 
Back
Top Bottom