Tanzania: Tatizo la ajira kwa vijana ni kubwa sana, lisifanyiwe masihara!

Leo hii nimetangaza kazi ya bartender aliyemaliza form six na mpaka sasa nimepigiwa simu na watu kumi graduates,inatisha
 
kama utampata January Makamba niliwahi kuona uwasilisho wake mmoja umesheheni takwimu hizo
 
Habari zenu wana Jf

Ajira imekua ni janga katika nchi yetu ya Tanzania, ilhali hatuna wataalamu wa kujitosheleza katika ujuzi wa biashara, sanaa, mawasiliano na uhandisi. Na hili linatokana na mfumo wa serikali kushindwa kutengenza vyanzo vya ajira kwa vijana wake na hili linatokana na uzembe na ubinafsi wa viongozi husika.

Pia hata mitaala itumikayo kufundisha vyuoni kutoendana na mahitaji ya waajiri. Cha msingi kwa wewe mpanda maendeleo yako binafsi kutokana na janga hili jitahidi kutengeneza mazingira ya kujiajili kuepusha kupoteza mda wako mtaani ukiangaika kutafuta ajira huku ukiwa haujui ni lini utaipata hiyo ajira.

Na kama mjuavyo kadri mda unavyo kwenda ile thamani ya Elimu yako inapungua, muajiri awezi kumuacha kijana alie toka chuoni mwaka huu kichwa kikiwa moto aje akuchukue wewe ulie kaa mtaani miaka mitano pasipo hata ku upgrade elimu yako.

Ingawa katika kujiajili kuna changamoto ila ndio njia sahihi iliyobaki kwako usie kua na ajira kujikomboa. Ki ukweli tunalilia ajira, but kuajiliwa ni mateso na kama utumwa
 
Mtawala wa taifa hili na wateule wake wanavyojua kuyatumia majukwaa yaliyoko katika kona mbalimbali hapa nchini wakihubiri na kueneza propaganda kuhusu ajira kwa vijana hapa nchini huko wengine wakithubutu kuwaeleza vijana eti waache kufikiria kuajiriwa na serikali badala yake wajiajiri wao wenyewe kwa ajira binafsi.

Huyu anayewaambia vijana wajiajiri muulize yeye kajiajiri? Yaani nikifikiria mifumo mingi iliyopo serikalini zama hizi hususani ile ya kuajiri natamani kutapika nyongo.

Ndugu wasio na sifa stahilivu wanajazana kwenye taasisi moja mfano mzuri nenda kajioneeni kwa macho yenu pale BoT. Wale wote wenye shahada na hawana ndugu kwenye system serikali ya CCM inawashauri wachangamkie fursa za kilimo bado kwanza.

Yaani huu ni uchuro mtupu.

Matatizo ya ajira yanaweza kuisha au kupungua iwapo sekta binafsi zitawezeshwa kukua na kupanuka zaidi. Sasahivi zinashindwa kukua kwa sababu kodi kibao, umeme wenyewe ndo huo tena mtu anazalishaje?

Tunategemea zaidi ajira chache za serikali ambazo zinataka darasa. Kila mkoa ungekuwa na viwanda na maduka makubwa 5-10 nina hakika ungekuwa unauliza kwanini Dar es Salaam ina watu wachache?
 
litakwisha tu pale vyuo vikuu vyetu vitakapobadilisha mitaala yake iwe inalenga zaidi wahitimu kujiajiri wenyewe kuliko kuajiriwa
 
Kwa watawala hawahawa
Akili hizi hizi
mtazamohuuhuu
na mfumo huuhuu ni tatizo la kudumu CCM Hoyeeeeeee! Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeee!
 
Matatizo ya ajira yanaweza kuisha au kupungua iwapo sekta binafsi zitawezeshwa kukua na kupanuka zaidi. Sasahivi zinashindwa kukua kwa sababu kodi kibao, umeme wenyewe ndo huo tena mtu anazalishaje?

Tunategemea zaidi ajira chache za serikali ambazo zinataka darasa. Kila mkoa ungekuwa na viwanda na maduka makubwa 5-10 nina hakika ungekuwa unauliza kwanini Dar es Salaam ina watu wachache?
 
Ndugu zangu wa Jamii Forum na wadau wanaoweza kuchangia, tatizo la ajira kwa vijana linatisha hapa nchini. Lakini leo nazungumzia vijana waliomaliza Vyuo Vikuu, ambao hawana ajira na wanazagaa kila mahali. Taifa limetumia fedha nyingi kuwapa elimu kwa mategemeo makubwa kwamba watalisaidia kuliendeleza kiuchumi.

Lakini pia wazazi na walezi wamekuwa na matumaini makubwa kwamba wahitimu hawa watapata ajira na kubadilisha maisha. Matokeo yake ni kinyume na matarajio. Kwahiyo wahitimu wenyewe, wazazi/walezi na Taifa kwa ujumla linafadhaika kwa hali hii tete.

Nimekuwa nikijiuliza hivi kwamba hakuna kazi za kuajiriwa au vijana wetu hawana maandalizi ya awali ili waweze kutafuta ajira?

Je vijana hawa wanauzika?wanaweza kushiriki usahili na wakafaulu kwa kujenga mazingira ya kuwavutia wanaotaka kuwaajili?

Je wanaandika je wadhifa wao (CVs).


Tatizo liko sehemu zote, kinachowaumiza vijana ni kuwa na matarajio makubwa baada ya kumaliza msomo yao. Mtu akimaliza bachelor anawaza kupata kuanzia laki saba huyo ukimuambia nitakulipa laki 3 hakuelewi hata kama hana kazi anahisi anaidharirisha degree yake wakati hata uzoefu hana.

Serikali haina mipango endelevu ya kuweka mazingira ya kuwaajiri hawa inao wasomesha bado haijafikiria mikopo watarudishaje kama hawana kazi mitaala yenyewe hawawajengei wanafunzi hawa kuwa na elimu ya ujasiliamali kiasi kwamba kinageuka kitendawili.

Leo unapomwambia ajiajiri wakati hata hajui anaanzaje.
 
kwanza we maoni yako ni yapi? unahisi tatizo liko wapi?

sikia bro. ukisoma kila tangazo la kazi, wanahitaji experience ya miaka.3+ hafu mimi sina ata ya week moja, je ilo ni.kosa langu?
na hizo kazi wanazowekana watoto wa mjomba na shangazi yake mpwa wake je? nazo ni.kwasababu sikuandika cv nzuri?

yatasemwa mengi sana, lakini tatizo ni viongozi wa juu hadi wa chini katika sector husika. hii issue ni kubwa, kuizungumzia unahitaji counter book la 4 quire ili ukamilishe abstract tu.
 
Tatizo liko sehemu zote, kinachowaumiza vijana ni kuwa na matarajio makubwa baada ya kumaliza msomo yao. Mtu akimaliza bachelor anawaza kupata kuanzia laki saba huyo ukimuambia nitakulipa laki 3 hakuelewi hata kama hana kazi anahisi anaidharirisha degree yake wakati hata uzoefu hana.

Serikali haina mipango endelevu ya kuweka mazingira ya kuwaajiri hawa inao wasomesha bado haijafikiria mikopo watarudishaje kama hawana kazi mitaala yenyewe hawawajengei wanafunzi hawa kuwa na elimu ya ujasiliamali kiasi kwamba kinageuka kitendawili.

Leo unapomwambia ajiajiri wakati hata hajui anaanzaje.
 
kwanza we maoni yako ni yapi? unahisi tatizo liko wapi?

sikia bro. ukisoma kila tangazo la kazi, wanahitaji experience ya miaka.3+ hafu mimi sina ata ya week moja, je ilo ni.kosa langu?
na hizo kazi wanazowekana watoto wa mjomba na shangazi yake mpwa wake je? nazo ni.kwasababu sikuandika cv nzuri?

yatasemwa mengi sana, lakini tatizo ni viongozi wa juu hadi wa chini katika sector husika. hii issue ni kubwa, kuizungumzia unahitaji counter book la 4 quire ili ukamilishe abstract tu.

you have said it all sir,
 
smtym vijana tunachagua kazi,wakati mwingine inabidi ukubali to start small

that was back then,watu siku hizi hawachagui kazi maana hata hizo za kuchagua hazipo.Mambo yanabadilika kwa kasi sana!hakuna nafasi za kuvolunteer,intern ,hata kupata field attachment ni shida,the unemployed wasilaumiwe kwa haya!
 
Wazee wana miaka mia, elimu std 4 ya mkoloni hawataki kuachia chance
kibongo bongo mtu 1 vyeo kibao, ni mwenyekiti wa nini sijui, ni director, ni nani huko sijui
yani ana cover nafasi za watu hata 7 watu watapata wapi hizo nafasi
wanasisitiza kujiajiri mtaji ndo ishu hakuna asiependa kufanya ishu zake
 
Back
Top Bottom