Tanzania, somalia kubambana na uharamia ukanda wa bahari ya hindi

BabuK

JF-Expert Member
Jul 30, 2008
1,845
329
RAIS wa Somalia, Shehe Sharif Ahmed amesema nchi yake itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha uharamia unakwisha katika Ukanda wa Bahari ya Hindi.

Amesema yeye na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete wamekubaliana kuhakikisha ushirikiano wa kiulinzi na usalama unakuwepo wakati wote katika ukanda huo.

Rais Ahmed ameyasema hayo leo asubuhi alipozungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam muda mfupi kabla ya kurejea nchini kwake.

“Pamoja na kuathiri eneo la ukanda wa Bahari ya Hindi na Tanzania kwa ujumla, maharamia wanatishia maisha ya watu na shughuli za maendeleo katika sehemu kubwa ulimwenguni.

“Nchi yangu itajitahidi kushirikiana na Tanzania kwa kiasi kikubwa katika masuala ya ulinzi na usalama wa ukanda huo na kuukomesha. Hayo ndiyo pia tuliyokubaliana na Rais mwenzangu Kikwete tulipozungumza jana (juzi) na nadhani yatafanikiwa,” alisema Rais Ahmed.

Kuhusu hali ya ukame nchini kwake alisema; “wananchi wangu wapatao milioni 3.5 wanateseka kwa njaa kali lakini ninamshukuru Rais Kikwete na Watanzania wote kwa kutupatia msaada utakaowawezesha kuishi.”

Kuhusu namna ya kufikisha msaada huo na mingine ya kimataifa wakati kukiwa na zuio la kundi la kigaidi la Alshaabab, alisema; “Hatuna budi kuyakomboa maeneo hayo na kuhakikisha watu wake wanafikiwa na kusaidiwa.

“Nia yetu ni kuhakikisha kundi hilo linatoweka kabisa katika nchi hii (Somalia) ndio maana tumekubaliana na Rais Kikwete kushirikiana kuhakikisha linaondoshwa hata kama itakuwa kwa njia ya mazungumzo,” alisema Rais Ahmed.

Kwa maelezo yake, Serikali ya Somalia ipo tayari kufanya mazungumzo na kundi hilo la Alshaabab ingawa anahisi litakataa kukaa mezani.

 
Kwa maelezo yake, Serikali ya Somalia ipo tayari kufanya mazungumzo na kundi hilo la Alshaabab ingawa anahisi litakataa kukaa mezani.

Tatizo sio kuhisi kuwa Alshabab itakataa bail Umoja wa Afrika inatakiwa iombe kuzungumza nao then tusikie response yao.
Hilo likifanikiwa itakuwa ni faida kubwa kwa Umoja wa Afrika kuwa ina uwezo wa kusolve matatizo ya wanachama wake.

Lakini pia itakuwa ni moja ya solution kuhusu UHARAMIA unaotikisa katika Ukanda wa Pwani ya Afrika ya Mashariki katika Bahari ya Hindi eneo la Mombasa, Maharamia ni kundi la watu wanaojipatia ajira rahisi, isiyo na gharama au kwa maneno mengine tunaweza kusema majambazi wanaoteka meli na kudai fidia ya mabilioni ya fedha, ambazo hawajazifanyia kazi yoyote.

Hakuna asojua madhara ya Uharamia tunayopata, Uharamia unaofanywa katika ukanda wa pwani hizo mbili yaani Mombasa na Somalia, unaziathiri kiuchumi nchi zaidi ya 15, zinazotegemea kuingiza bidhaa zake kupitia Bandari ya Hindi.
Tayari hofu kwa mataifa yanayotegemea kupitisha bidhaa zake katika Bandari ya Dar es Salaam, inaathiri Tanzania kiuchumi kwani meli zenye shehena ya kupeleka nchi jirani kama Kongo, Zambia, Burundi, na Rwanda, zitatishika kutokana na tatizo hilo.


Kwakuwa source kubwa ya uharamia ni kukosekana kwa Serikali dhabiti ya Somalia hivyo incase tutawapatanisha wakawa na serikali ya Umoja wa Kitaifa na watadhibiti vizuri suala hilo la Uharamia.

Ni muda mwafaka kwa Umoja wa Afrika kuwapatanisha Al Shabab na serikali ya Somalia.
 
Then its not surprising that Wakili Mwale amekua arrested just a week before rais wa Somalia amekuja Tanzania. Nafikiri Kikwete alikua anataka kumuimpress huyo wa Somalia kua the supposedlly agent wa maharamia wa Somalia amekua arrested in Arusha so Tanzania is serious about fighting piracy in the horn of Africa. Kuna tetesi kua zile 18 billion alizokutwa nazo Mwale ni ransom money paid to Somali pirates for the hijacking of ships.
 
Back
Top Bottom