Tanzania ready to send Army to Zimbabwe-Kikwete

Status
Not open for further replies.
Mbinu ya kaburu na wale walioiuza nchi ni moja!
Kusafishana kama kawa!
Sinclair anaweza akawa ameutumia ushawishi wake kwa kushirikiana na kina Bush ili kumpa madaraka ya Afrika kikwete!
Wamejitahidi sana!
Angalia hata mgogoro wa kenya wamarekani walivyompa misifa!
Niliwaambia huko nyuma...Blair alimpa sapoti bush ya iraqi..Na yeye anampa ya Zimbabwe!
Mtu wa kumbana mwenye matatizo makubwa na mwenye ushawishi ni Tanzania!
Kwani wanajua atawatumikia kwa nidhamu ya woga!
Na kama asingefanya hivyo hata yeye wangemtoa madarakani!
Halafu wakawa wanajua kuhusu kahfa hizi ambazo zinazidi kuhatarisha utawala wa kikwete!
Wakapanga dili lingine la kusafishana!
Plan B.
wananchi msikubali huu uoza!
Nyie ndio wenye sauti!
Daini hojas za TAIFA BUNGENI!
Huo ni ushauri wangu...Mwenye masikio na asikie.
 
gharama ya kuingia kijeshi zimbabwe ni kubwa sana....na records nilizonazo ni kuwa pamoja na hali ngumu ya uchumi...zimbabwe wanalo moja ya majeshi ya kisomi kabisa afrika....smalll but well trained army..,pia jeshi lao la anga ni zuri sana ...,na wana ndege nzuri pamoja na kuwa karibuni ndege zao nyingi zimekuwa grounded kwa ukosefu wa spears....bado huwezi kubeza...

kikwete kuwa mwenyekiti wa AU aitake kuleta millitary solutions kila mahali...haiwezeka...ninavyojua serikali za kiafrika mnaweza kukubaliana kuingiza jeshi then at last minutes tukishaingiza jeshi wengine wanajitoa ..tunabakiwa na burden peke yetu......gharama tulizotumia comoro ni bilioni 10...na hadi leo serikali haijarejeshewa pesa ,AU hawana pesa!!!

hatua yoyote ya kuingiza jeshi zimbabwe ni lazima liwe PEACE KEEPING na kamwe sio INVATION[UVAMIZI]...na hata kama ni peace keeping lazima ikubaliwe pamoja na serikali ya zimbabwe na MDC ili lisishambuliwe!

pia kulikuwa na mpango wa kuwa na brigade ya peace keeping ya SADC ...makao makuu yakiwa KIBAHA ....naona hilo bado halijatekelezwa....hiyo brigade ingesaidia ..kama ECOWAS wanavyofanya!
 
Mh Rais,ushauri wangu,hata itakapofikia kuja kupeleka jeshi zimbabwe nakuomba usilipeleke kweli tishia tu, wale wazimbabwe siyo wacomoro,fikiria mheshimiwa kabla haujaamua, hatutaki zile enzi za mitume kuoa wake wengi zirudi,(mitume walikuwa wakioa wake wengi sababu,wanaume wengi walikuwa wanakufa vitani)
 
Kwanini kikwete akubali MAKABURU WATUPIGANISHE HOVYO HOVYO?
HAMJUI KUNA WANAOSUBIRI KUANZA KUPORA MALI ZETU NA KUUZA SILAHA ZAO?
WAZALENDO GANI HAWA TUMEWAPA NCHI?
HAWAJUI USEMI WA DIVIDE AND RULE?
AMA KWELI VITA YA PANZI...
 
Sidhani kama kuna nchi ya kiafrika ambayo inataka kupeleka majeshi yake Zimbabwe. JK kama kawaida yake anacheza na maneno tu hapa.... ahadi kibao .... issue ya Comoro ni tofauti kabisa na Zimbabwe na JK anajua hilo.
 
Ahadi za kutuzuga ili tusahau EPA,RICHMOMD,KIWIRA KAGODA NK!
Nimewashauri waje na PLAN B!
Lakini mijitu hii ina akili ngumu mno mpaka nashangazwa ni kivipi walipewa madaraka makubwa ya nchi amabayo wengi wetu tunayaogopa kama nini!
 
Hii safi kabisa kwani ndio tunataka tuelekee kwenye siasa ambazo hakuna kuzulumu na muelekeo anaoupeleka Mheshimiwa sio mbaya kwani naona ameanza kufahamu kuwa ubabe wa kutumia maguvu kwenye uchaguzi sio jambo la busara ,hivyo akumbuke yale mambo ya kupeleka vifaru na marocket loncha kule Unguja na kwenda kuwahanisisha watu na familia zao kule Pemba si mambo ambayo yanawanyima uhuru wa kuchagua serikali yao wazanzibari bali ni siasa za ukandamizaji na unyanyasaji ,zikichangiwa na tabia za kinyama maana ubinadamu huondoka na kuingia tabia za unyama na hilo Muungwana analifahamu kwani katika Uislamu tabia ya binadamu ina kiwango na hutokea ikawa mnyama ni bora kuliko binadamu.
soldier_with_rocketlauncher.jpg

_40958996_zanzibar-body203.jpg

policebeat.jpg

_40961720_zanz_army_ap203x300.jpg

_1186269_zanzibar300.jpg
 
Kitu ambacho nadhani wengi tumekisahau au kushindwa kuconnect dots ni kile kile kilichotokea kwa upande wa Kenya. Kweli JK anatumiwa kupitisha ujumbe kwa Mugabe. Hilo ndilo jambo ambalo binafsi linanikera sana na niliandika kwenye barua kwa JK. Hatuwezi kusubiri wazungu watuambie kuwa Zimbabwe hali ni mbaya.

Kuhusu matumizi ya nguvu inasikitisha kuona kuwa JK ananukuliwa kusema haya siku moja baada ya wabunge wa Uingereza kutoa mawazo ya kutumia jeshi kuingilia Zimbabwe. Na sitoshangaa US nao wakasema wako tayari kutoa financial and logistical support kwa ajili ya jeshi hilo. Tofauti na AU Marekani na Uingereza wanazo fedha za kufanikisha hilo kama wakitaka.

Ni kwa sababu hiyo siamini kuwa JWTZ inaweza kushiriki moja kwa moja kwenye uvamizi ikibidi, ila sitoshangaa tukatakiwa kutoa viwanja na staging area ya Operation ya kijeshi. Hivyo manowari na meli za kivita za Uingereza na hata Ufaransa zinaweza kusogea katika pwani yetu na kuwa staging area. Tunaweza tusitakiwe kutoa hata askari mmoja lakini tukatakiwa kutoa ruhusa ya kutumia anga letu kwa ndege zao za kivita. Hayo yote yanawezekana and me being a military analyst pia naweza kusema kwamba uwezekano wa kutumia jeshi letu moja kwa moja ni mdogo lakini tunaweza kutumika kama ilivyotumika Saudi Arabia au Qatar au Kazikstan katika vita vya Iraq.

Ni kwa sababu hiyo naamini the best approach for Kikwete is not the "war talk" bali kusimama na kuitisha mkutano wa ufumbuzi wa suala la Zimbabwe mojawapo ni kuhakikisha kuwa Mugabe anaanchia ngazi na analindwa asishtakiwe na wakati huo huo kuandaa uchaguzi mpya na huru. Hata hiyo mazungumzo haya ya vita yana lengo moja tu, nalo ni kuweka pressure kwa Mugabe.

Itakuwa ni aibu sana kwa Afrika endapo Mugabe ataondolewa madarakani kwa nguvu.
 
Tulikuwa tunafikiria kuwa kuja kwa Bush na ahadi ya burungutu la karibu $700 million ni kwa vile tunafanya mambo vizuri. Sasa zitatutokea puani, tulianzia Commoro. Sasa Zimbabwe, pengine itafuatia Somalia, Dafur n.k. Tukimaliza hapo hizo $700 millioni ndio zitakapoachiwa kidogo kidogo.

Kweli, ukiwa na raisi kiwete na nchi nayo inakuwa vivyo hivyo.
 
Hii safi kabisa kwani ndio tunataka tuelekee kwenye siasa ambazo hakuna kuzulumu na muelekeo anaoupeleka Mheshimiwa sio mbaya kwani naona ameanza kufahamu kuwa ubabe wa kutumia maguvu kwenye uchaguzi sio jambo la busara ,hivyo akumbuke yale mambo ya kupeleka vifaru na marocket loncha kule Unguja na kwenda kuwahanisisha watu na familia zao kule Pemba si mambo ambayo yanawanyima uhuru wa kuchagua serikali yao wazanzibari bali ni siasa za ukandamizaji na unyanyasaji ,zikichangiwa na tabia za kinyama maana ubinadamu huondoka na kuingia tabia za unyama na hilo Muungwana analifahamu kwani katika Uislamu tabia ya binadamu ina kiwango na hutokea ikawa mnyama ni bora kuliko binadamu.
soldier_with_rocketlauncher.jpg

_40958996_zanzibar-body203.jpg

policebeat.jpg

_40961720_zanz_army_ap203x300.jpg

_1186269_zanzibar300.jpg

Good point!

Na Sherrif naye amuombe Mugabe msaada wa kumwodoa Kikwete?
Tunakwenda wapi?

Hivi hujui wanataka kuifanya AFRIKA MUFLIS?
No No No!

Hata hao wanaosadikiwa kuua watu huko waweza kuwa mapandikizi tu na huku wakisema wametumwa na Mugabe!

Vita ya Iraqi niliifuatilia toka mwanzo hadi mwisho.

Tooo much interests to the extent kwamba hakuna kumwamini FISADI TENA KWA LOLOTE LILE!

KIKWETE HAWEZI KUPATA SAPOTI YA WATAZANIA KWA KUKOMALIA MAMBO YA ZIMBAWE WAKATI NA SISI WENYEWE HATUKO HURU!
 
Kwa mujibu wa ile taarifa ya thread, jeshi letu ni kubwa zaidi ya mara mbili ya lile la Zimbabwe. Sasa, I hope Rashid Othman kampa Kikwete better Intelligence Estimates, than simply relative military sizes. Wanaweza kuwa wana nondo kali zaidi yetu ( juzi Mchina Mwekundu kashusha shehena za ammo kwa Mugabe hapo).

Tusije tukaenda kichwa kichwa tukatembezewa mkong'oto. Wenye "dataz" za Nuclear Stockpiles za Mugabe mpo?

rashid othman hahusiki na millitary intelligence gathering......jeshi wana utaratibu wao wa kukusanya millitary intelligence kwa kutumia KITENGO CHA USALAMA JESHINI.....mkuu wa usalama jeshini ni BREGADIER MELLA!....waliomtangulia ni GEN.DAVIS MWAMUNYANGE[AKIWA BRIGADIER]...akafuatia LT GEN SHIMBO[AKIWA BRIGADIER]....Akafuaatia yule brigadier aliyekuwa mwambata wa burundi aliyefariki mata tu baada ya uteuzi hata kabla hajaaza kazi...ndio akaja huyu brig .mella ..ambaye kabla alikuwa kanali [mwambata wa kiujeshi msumbiji]
 
Wakuu,

Naona tunasahau jambo moja kubwa hapa kuhusu Zimbabwe.

Matatizo yanayoikabili Zimbabwe ni global na wale political elite wote Kikwete sasa akiwa mmojawapo wanajaribu kutaka kuidhibiti Zimbabwe kwenye suala la global financial interests.

Huko nyuma kulikuwa na nchi kama za Angola, Msumbiji, DRC na Sudan ambayo bado ina matatizo kule Darfur. Lakini hii kitu global financial markets inakuwa siku zote subsidised na rasilimali kutoka Afrika na Zimbabwe ilikuwa na mazao ya biashara na madini ambavyo kwa sasa havina soko.

Inajulikana sasa kwamba hizi financial interests zinakabiliwa na credit crunch, high inflation na pia the rise of commodity prices hasa mafuta na chakula.

Pia Mugabe pamoja na kusema kwamba Tsvangirai ni puppet wa mabepari lakini ni ukweli usiofichika kwamba ni lazima mabepari hawa watafanikiwa katika azma yao.

Kwa hio mimi naona kwamba kama kweli Kikwete ametoa wazo hili ni katika kujaribu kuona kwamba litakuwa digested vipi na hadhira kabla ya kufanya hivyo na baadae kusaidiwa na mabepari wenzie chini ya mwavuli wa UN resolutions zisizo na kichwa wala mkia.

By the way Mugabe alipewa nchi pale Lancaster House, lakini kwa kutaka sifa kupitia mgongo wa wakoloni wa zamani sasa anachemsha na wao hawako tayari kumuona anafanya hivyo.

Sijui wenzangu mnaonaje wazo hili.
 
Kitu ambacho nadhani wengi tumekisahau au kushindwa kuconnect dots ni kile kile kilichotokea kwa upande wa Kenya. Kweli JK anatumiwa kupitisha ujumbe kwa Mugabe. Hilo ndilo jambo ambalo binafsi linanikera sana na niliandika kwenye barua kwa JK. Hatuwezi kusubiri wazungu watuambie kuwa Zimbabwe hali ni mbaya.

Kuhusu matumizi ya nguvu inasikitisha kuona kuwa JK ananukuliwa kusema haya siku moja baada ya wabunge wa Uingereza kutoa mawazo ya kutumia jeshi kuingilia Zimbabwe. Na sitoshangaa US nao wakasema wako tayari kutoa financial and logistical support kwa ajili ya jeshi hilo. Tofauti na AU Marekani na Uingereza wanazo fedha za kufanikisha hilo kama wakitaka.

Ni kwa sababu hiyo siamini kuwa JWTZ inaweza kushiriki moja kwa moja kwenye uvamizi ikibidi, ila sitoshangaa tukatakiwa kutoa viwanja na staging area ya Operation ya kijeshi. Hivyo manowari na meli za kivita za Uingereza na hata Ufaransa zinaweza kusogea katika pwani yetu na kuwa staging area. Tunaweza tusitakiwe kutoa hata askari mmoja lakini tukatakiwa kutoa ruhusa ya kutumia anga letu kwa ndege zao za kivita. Hayo yote yanawezekana and me being a military analyst pia naweza kusema kwamba uwezekano wa kutumia jeshi letu moja kwa moja ni mdogo lakini tunaweza kutumika kama ilivyotumika Saudi Arabia au Qatar au Kazikstan katika vita vya Iraq.

Ni kwa sababu hiyo naamini the best approach for Kikwete is not the "war talk" bali kusimama na kuitisha mkutano wa ufumbuzi wa suala la Zimbabwe mojawapo ni kuhakikisha kuwa Mugabe anaanchia ngazi na analindwa asishtakiwe na wakati huo huo kuandaa uchaguzi mpya na huru. Hata hiyo mazungumzo haya ya vita yana lengo moja tu, nalo ni kuweka pressure kwa Mugabe.

Itakuwa ni aibu sana kwa Afrika endapo Mugabe ataondolewa madarakani kwa nguvu.

Mkjj,

Kwa bahati mbaya maamuzi yalishafanyika. Maelezo nyuma ya pazia yanatisha kuliko hata yanayosemwa kwenye stage. Mtego ni mbaya ila hilo la kutumia kambi na anga lina nafasi kubwa zaidi kufanyika wakati huu kuliko ule uliopita.
 
Wakuu,

Naona tunasahau jambo moja kubwa hapa kuhusu Zimbabwe.

Matatizo yanayoikabili Zimbabwe ni global na wale political elite wote Kikwete sasa akiwa mmojawapo wanajaribu kutaka kuidhibiti Zimbabwe kwenye suala la global financial interests.

Huko nyuma kulikuwa na nchi kama za Angola, Msumbiji, DRC na Sudan ambayo bado ina matatizo kule Darfur. Lakini hii kitu global financial markets inakuwa siku zote subsidised na rasilimali kutoka Afrika na Zimbabwe ilikuwa na mazao ya biashara na madini ambavyo kwa sasa havina soko.

Inajulikana sasa kwamba hizi financial interests zinakabiliwa na credit crunch, high inflation na pia the rise of commodity prices hasa mafuta na chakula.

Pia Mugabe pamoja na kusema kwamba Tsvangirai ni puppet wa mabepari lakini ni ukweli usiofichika kwamba ni lazima mabepari hawa watafanikiwa katika azma yao.

Kwa hio mimi naona kwamba kama kweli Kikwete ametoa wazo hili ni katika kujaribu kuona kwamba litakuwa digested vipi na hadhira kabla ya kufanya hivyo na baadae kusaidiwa na mabepari wenzie chini ya mwavuli wa UN resolutions zisizo na kichwa wala mkia.

By the way Mugabe alipewa nchi pale Lancaster House, lakini kwa kutaka sifa kupitia mgongo wa wakoloni wa zamani sasa anachemsha na wao hawako tayari kumuona anafanya hivyo.

Wameshajitayarisha kuivamia ZIMBABWE MARK MA WORDS!
Kikwete kasema akiombwa!
Tsivangarai keshakataa mambo ya uchaguzi.
Subiri ukisikia tu amri ya Tsivangarai...Basi ujue ni amri ya Blair kupitia kwa Bush hadi kwenye channel ya Kikwete ambaye keshajitayarisha kutake action ili makaburu wampe sapoti na yeye kuwa safi na huru dhidi ya tuhuma chini ya ufadhili wa mataifa yanayoitwa wafadhili ambayo sasa yanaipigania Afrika UPYA!
 
Hivi kuna tofauti yoyote kati ya Zimbabwe na kinachoendelea Zanzibar tangu mwaka 1995?

Ndiyo,tofauti ni kwamba huko Zimbabwe ni kwa maslahi ya wakubwa wanaotoa 'hand out'.

lakini ukija kwenye udikteta na matumizi ya nguvu kuzima matakwa ya wananchi hakuna tofauti.
 
Wandugu,
Zimbabwe mambo ni mabaya hivi sasa lakini chaguzi zake, ukiachilia mbali huu unaokuja, zimeendeshwa vema zaidi kuliko nyingi hapa Africa. Hiyo piga nikupige ya Mugabe inaambiwa imeua 80, Kenya wanakufaga wangapi wakati wa uchaguzi?

Tatizo la hivi sasa ni kuwa Mzee Mugabe maisha yake yako hatarini, kwani wazungu wa Zimbabwe, SA, AUS, NZ na UK, wote wanataka kichwa chake, kitu ambacho inabidi naye ajinginge kwa nguvu zote alizo nazo.

Kama wakiondoa vitisho vyao na kukaa naye chini, kuwa hataguswa baada ya uchaguzi, sidhani kama angeng'ang'ania kiti hadi hivi sasa.

Tanzania kwa misemo yetu ikiwemo huu wa kupeleka majeshi, ingawa mimi bado siamini kama JK kasema, maana umetokea kwenye www ya pro Tsvangirai, ni kama imejitoa kwenye upatanishi, maana sidhani kama Mugabe atatuamini tena kwa misimamo yetu.
 
Hivi Mugabe naye alijua nini kuwa haya yanakuja, otherwise ile kontena nzima ya SMGs ilikuwa kwa ajili ya nini?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom