Tanzania Railway Ltd kulipa Dola Milioni Saba za mkopo!

Wajerumani walikuja ku bid na ramani ya 1905.Kama serikali ingeshirikiana na ya ujerumani, US,Canada au UK tusingefika hapa mahali pa kusaini contract halafu tunalipa deni la kusaini contract c'mon!
Tulihoji RITES wanasifa gani, tukababaishwa baibashwa na serikali kwa vile 10% walishakula.

Futa bid ni uchafu, tuombe wenye akili watusaidie.period.
Kwa kweli inasikitisha sana nchi kukosa mwelekeo na mipango madhubuti, inaudhi sana kwakweli
 
Kwa kweli inasikitisha sana nchi kukosa mwelekeo na mipango madhubuti, inaudhi sana kwakweli
Pitia bajeti ya miundombinu kama utaweza kuamini kuna uwekezaji wowote kwenye miundo mbinu kama reli. Iliyojaa ni siasa na haditihi tu hakuna chochote cha leo au miaka 10 ijayo. Inasikitisha
 
Hizi sredi nyingine hizi bana mtu huwezi kuchangia bila kutukana... aaarrrgh!!!! xxxqqqqqqqqhiiiiiii (msonyo)
 
Bila kubinafsiha na kuwa na kampuni za reli "independent" hata wawekeze trillioni kumi, zitakufa tu. Hakuna kitu kiitwacho mali ya umma kikaendelea Tanzania hii.

...you could be right, you know too well what can and cannot be achieved under CCM!!
 
Hahahh!
Jumanne+Rashid.jpg
 
Wakuu,
Baada ya kuona treni imeanza kazi nimepitia tena thread nyingi na kuona kumbe tunaweza kama tutaongozwa.
Kwanza kabisa treni ya abiria katika jiji imeanza kazi. Wapo watakaocheka na inawezekana isiwe kama ile ya New York au London. Kitu kimoja muhimu sana ni kuona kuwa japo basi kuna watu wanafikiri kuliko kutokuwa na wasiofikiri.
Huu ni ushhidi mzuri kuwa kukiwa na usimamizi mzuri wa malengo tunaweza kujikongoja hata kama ni kutumia magongo.

Treni itakabiliwa na changamoto nyingi sana. Nimeona mabehewa yalivyokarabatiwa bado hayajakidhi haja ya treni ya mjini, hilo si tatizo kwasababu ni mwanzo tu.
Changamoto ya pili ni uendeshaji unaoweza kukwaza na gharama kubwa. Treni kama hizi huwa na vituo maalumu vilivofungwa ili kupunguza idadi ya wasimamizi. Hilo nalo pia ni kutokana na uchanga.
Ratiba na mambo mengine yanaweza kuwa ni changamoto za kila mara lakini basi japo kuna mahali pa kuanzia.

Sasa tunategemea kuona treni ya haraka kutoka Morogoro hadi Dar, Tanga Dar, Tanga Arusha. Huduma za kila siku Dar Mwanza, treni za haraka Dodoma Dar n.k.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
mwanzoni nilikuwa naamini kuwa mambo tunayowaambia CCM na serikali ni mambo mageni kiasi kwamba wanaweza kuyafanyia kazi. Baadaye nikaja kuguundua kuwa yote tunayoyasema yameshasemwa sana na kujadiliwa. Tatizo ni kuwa yakitekelezwa yataondoa mianya ya ulaji. Ndio maana UDA imeuzwa, ATCL, na upuuzi mwingine wote tunaoujua.

Fikiria kwa mfano, hakuna mahali pazuri pa kuanzia treni za kasi kama Moro - DAR na Dar - Tanga. Maeneo hayo kwa treni iendayo kasi yanafikika chini ya dakika 45. Moro iko karibu 120Miles, wakati Tanga iko 223Miles kutoka Dar. Sasa tatizo kubwa la kwetu litakuwa bado ni umeme! Iwe kwenye Maglev trains au conventional trains. Lakini kabla ya kwenda huko tungeimprove hizi hizi conventional kama tulivyokuwa tunafanya (nadhani bado) kwenye TAZARA ambako tulikuwa na ile express na ordinary trains. Watu wangeweza kujenga na kuishi Tanga au Moro wanakuja asubuhi kufanya shughuli zao na kugeuza jioni na wengine wangeweza kufungua biashara huko kwingine na kuishi Dar.. miji yote miwili ingeweza kabisa kuabsorb the growing population ya Dar na hata Zanzibar.

Tukumbuke kwamba kwetu tatizo si fedha, siyo teknolojia wala siyo uwezo au haja. Vyote hivyo vipo. Tatizo ni uongozi. Ninaangalia hapa jitihada za Nyerere kuunganisha sehemu nyingine za Tanzania na Reli ya Kati - nimeshangaa juhudi zake hizo. Najiuliza TAZARA ilijengwaje wakati ule? Sasaa hivi TAZARA ingeweza pia kuwa na express hasa tukidandia utaalamu wa Wachina ambao waliijenga.. ingefungua pia barabara ya kwenda kusini zaidi..kama watu wanaweza kufika Mbeya mapema kuliko kwa njia ya basi well.. kwanini wapanda mabasi? barabara zingedumu zaidi n.k its all about leadership my dear friends.

Jitihada gani za Nyerere, yeye ndiye alyeuwa kila kitu Tanzania, usituchafuwe saa hizi.

Kwa mara ya kwanza tunaona treni ikipakia abiria mjini, kwa mara ya kwanza tunasikia treni ikiboreshwa. Nyerere alikuta treni toka Mjerumani, aliifanya nini badala ya kuiuwa na kuwa nyang'anyag'a.
 
Yes,kila linalofanywa leo ni kwa ajili ya maslahi ya matapeli wa Tanzania na nchi za magharibi wanaojiita wafadhali na hata wakati mwingine eti development partners,sio kwa ajili ya Watanzania.Ndipo tulipofika.Matapeli hawa wameteka kila nyanja.Wanafanya watakalo.Wao ndio wanaotengeneza wanasiasa,hawa wanaimba wimbo wao.No wonder hata raisi wa nchi nae analalamikia rushwa.Ipo kwa ajili ya mabwana zake,ni mfumo wa wakubwa, hana ubavu nayo.
Pitia bajeti ya miundombinu kama utaweza kuamini kuna uwekezaji wowote kwenye miundo mbinu kama reli. Iliyojaa ni siasa na haditihi tu hakuna chochote cha leo au miaka 10 ijayo. Inasikitisha
 
Jitihada gani za Nyerere, yeye ndiye alyeuwa kila kitu Tanzania, usituchafuwe saa hizi.

Kwa mara ya kwanza tunaona treni ikipakia abiria mjini, kwa mara ya kwanza tunasikia treni ikiboreshwa. Nyerere alikuta treni toka Mjerumani, aliifanya nini badala ya kuiuwa na kuwa nyang'anyag'a.
Aliimarisha reli aliyoacha Mjerumani, halafu akajenga nyingine. Awamu zote zilizofuata kwa pamoja hawajaweza kufanya uwekezaji aliofanya Nyerere.
Zomba angalia kumbu kumbu au kama huna basi omba tukupe.
 
Aliimarisha reli aliyoacha Mjerumani, halafu akajenga nyingine. Awamu zote zilizofuata kwa pamoja hawajaweza kufanya uwekezaji aliofanya Nyerere.
Zomba angalia kumbu kumbu au kama huna basi omba tukupe.

Nyerere hakujenga reli, aliyejenga mchina kwa kutaka shaba za Zambia, ustake kuchekesha watu.

Angeiimarisha hiyo reli ya kati si ungeiona inafanya kazi. Tuulize sisi tuliyoipanda wakati tunachukuwa uhuru hiyo treni ilikuwaje na miaka 10 baadae ilikuwaje, kwa ufupi; Nyang'anyang'a.
 
nyerere hakujenga reli, aliyejenga mchina kwa kutaka shaba za zambia, ustake kuchekesha watu.

Angeiimarisha hiyo reli ya kati si ungeiona inafanya kazi. Tuulize sisi tuliyoipanda wakati tunachukuwa uhuru hiyo treni ilikuwaje na miaka 10 baadae ilikuwaje, kwa ufupi; nyang'anyang'a.

pumba...vuuuu!
 
Nimesafiri sana na treni kwenda Tabora na Mwanza nilipokuwa mdogo yaani kama kuna usafiri bomba hakuna kama wa treni. Miaka ile haikutokea hata mara moja treni kulala njiani kwa tatizo lolote lile. Ukisafiri kwa daraja la kwanza/pili na hata la tatu ilikuwa ni raha ya aina yake kwanza kulikuwa na usafi wa hali ya juu. Maji kwenye mabehewa yote, vyoo visafi, mabehewa masafi, usiku mnalala kwa raha kabisa tena bila wasiwasi wowote wa kuibiwa au kukabwa. Hali ikaanza kubadilika taratibu kwa uchafu hasa daraja la tatu. Nauli ilikuwa inaongezeka karibu kila mwaka huku hali halisi na usafiri ikizidi kudorora kupita kiasi hata ile raha ya kusafiri na treni ikapotea. Pia kama ulivyosema Mkuu EMT kuna usalama mkubwa wa kusafiri na treni ukilinganisha kusafiri kwa mabasi. Mara zote nilizowahi kusafiri na treni haikutokea hata mara moja kuhofia ajali lakini kila nisafiripo na basi roho huwa mkononi ukifika uendako unashukuru Mungu.

Sijui kama usafiri wa treni nchini utarudia kuwa wa kiwango cha juu kama ilivyokuwa miaka ile maana wengi siku hizi hawana ustaarabu kabisa. Mtu anaweza kula ndizi au chungwa ndani ya treni akatupa ganda ndani ya behewa!!! Mtu anaweza kutema mate ndani ya behewa. MTu anaweza kumenya karanga ndani ya behewa na maganda akayatupa ndani ya behewa!!! Inasikitisha sana lakini ni kweli.


Na kama ni kweli watu 10 wanakufa kila siku kwa ajali za barabarani, then usafiri wa treni unaweza pia kupunguza hii idadi.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
Nyerere hakujenga reli, aliyejenga mchina kwa kutaka shaba za Zambia, ustake kuchekesha watu.

Angeiimarisha hiyo reli ya kati si ungeiona inafanya kazi. Tuulize sisi tuliyoipanda wakati tunachukuwa uhuru hiyo treni ilikuwaje na miaka 10 baadae ilikuwaje, kwa ufupi; Nyang'anyang'a.
Reli ya Tanga-Dar alijenga nani?
Nionyeshe reli iliyojengwa na Mwinyi, Mkapa na JK inayolingana na hiyo.

Ninasema kuwa mpaka Nyerere anaondoka madarakani reli zote zilikuwa zinafanya kazi.
Niambie reli ya kaskazini inapita behewa gani? Umetembelea ukaona reli ilivyo kichakani?

Narudia tena maana naona ulipanda treni za Congo, Nyerere akiondoka Madarakani reli ilikuwa inafanya kazi.
Unakumbuka ajali ya Kilosa ikitokea Nyerere hakuwa madarakani.
Narudia tena na tena maana uelewa wako unatia shaka sana, Nyerere akiondoka reli zote zinafanya kazi.OK?

Sasa endelea kubisha kadri uwezavyo, sina uwezo wa kukuzuia kuvua nguo hadharani. Ninachoweza kukuambia ni kuwa unavua nguo.

Zomba kuna maradhi mengi dunia lakini ya chuki ni hatari maana yanaathiri mfumo mzima wa fahamu.
Nionyeshe reli iliyojengwa na Mwinyi/Mkapa/ Kikwete kwa pamoja.
Kama huna jibu kaa kimya au endelea kuvua nguo mbele ya kadamnasi sina jinsi ya kukusadia tena
 
Reli ya Tanga-Dar alijenga nani?
Nionyeshe reli iliyojengwa na Mwinyi, Mkapa na JK inayolingana na hiyo.

Ninasema kuwa mpaka Nyerere anaondoka madarakani reli zote zilikuwa zinafanya kazi.
Niambie reli ya kaskazini inapita behewa gani? Umetembelea ukaona reli ilivyo kichakani?

Narudia tena maana naona ulipanda treni za Congo, Nyerere akiondoka Madarakani reli ilikuwa inafanya kazi.
Unakumbuka ajali ya Kilosa ikitokea Nyerere hakuwa madarakani.
Narudia tena na tena maana uelewa wako unatia shaka sana, Nyerere akiondoka reli zote zinafanya kazi.OK?

Sasa endelea kubisha kadri uwezavyo, sina uwezo wa kukuzuia kuvua nguo hadharani. Ninachoweza kukuambia ni kuwa unavua nguo.

Zomba kuna maradhi mengi dunia lakini ya chuki ni hatari maana yanaathiri mfumo mzima wa fahamu.
Nionyeshe reli iliyojengwa na Mwinyi/Mkapa/ Kikwete kwa pamoja.
Kama huna jibu kaa kimya au endelea kuvua nguo mbele ya kadamnasi sina jinsi ya kukusadia tena

Mkiambiwa mmejazwa Ubaguzi wa Ujinga mnakataa, kufanya kazi unakujuwa wewe au unasema tu? Ulisikia kabla ya ujio wake treni imezimika njiani inangoja diesel?
 
Mkiambiwa mmejazwa Ubaguzi wa Ujinga mnakataa, kufanya kazi unakujuwa wewe au unasema tu? Ulisikia kabla ya ujio wake treni imezimika njiani inangoja diesel?
Jibu swali muungwana! Ile reli ya Tanga-Dar nani aliijenga? Nionyeshe kipande cha reli kama ya Tanga-Dar kilichojengwa na Mwinyi/Mkapa/Kikwete.

Ubaguzi upo wapi katika swali? Jibu swali, lete hoja. Kama huna lete busara za ukimya.
Unapojinasibu umetumia reli baada ya uhuru wakati hujui ilijengwa lini na nani na kwanini, unawapa vijana nafasi ya kuvua hata nguo ya kujisetiri Yakhe!
 
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom