EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Kampuni ya Reli Tanzania (Tanzania Railway Ltd) imekubali kuilipa kampuni ya International Finance Corp kiasi cha dola za Kimarekani milioni saba ili kufuta deni inalodaiwa kabla ya kubinafsihwa tena na serikali.
Tanzania Railway Ltd iliingia deni hilo baada ya kuingia katika mkataba wa miaka 25 na ile kampuni ya Rites Ltd ya India. Hata hivyo mkataba huo ulivunjwa mwaka 2009. International Finance Corp ilikuwa imepanga kuikopesha Tanzania Railway Ltd dola za Kimarekani milioni 44 ili kuisadia kampuni hiyo ya reli kuboresha shughuli zake za usafiri wa reli Tanzania.
International Finance Corp ilikuwa tayari imeshaikopesha Tanzania Railway Ltd dola milioni 14. Tanzania Railway Ltd tayari imeshalipa dola milioni 7. Fedha hizi zililipwa Septemba 2010. Rites Ltd walitafutwa kwa njia ya simu kwenye makao makuu ya ofisi zao lakini hakuna aliyepokea simu.
Serikali ya Tanzania imepanga kuwekeza kiasi cha shilling trillioni 2 kwa miaka mitano ijayo kuboresha usafiri wa reli.
Tanzania Railway Ltd iliingia deni hilo baada ya kuingia katika mkataba wa miaka 25 na ile kampuni ya Rites Ltd ya India. Hata hivyo mkataba huo ulivunjwa mwaka 2009. International Finance Corp ilikuwa imepanga kuikopesha Tanzania Railway Ltd dola za Kimarekani milioni 44 ili kuisadia kampuni hiyo ya reli kuboresha shughuli zake za usafiri wa reli Tanzania.
International Finance Corp ilikuwa tayari imeshaikopesha Tanzania Railway Ltd dola milioni 14. Tanzania Railway Ltd tayari imeshalipa dola milioni 7. Fedha hizi zililipwa Septemba 2010. Rites Ltd walitafutwa kwa njia ya simu kwenye makao makuu ya ofisi zao lakini hakuna aliyepokea simu.
Serikali ya Tanzania imepanga kuwekeza kiasi cha shilling trillioni 2 kwa miaka mitano ijayo kuboresha usafiri wa reli.