Tanzania President Dr Magufuli is a new Field marshal in Afrika!

TumainiEl

JF-Expert Member
Jan 13, 2010
6,188
11,219
Nimeamua kuanza na kichwa cha habari chenye ujumbe rais wetu awezakuwa rais mpya ktk africa mwenye cheo cha field marshal.

Kwanini nasema hivyo? Sababu zakusema hivyo zinatokana na uhalisia wa hali ya sasa ktk taifa letu ambalo hapo awali ilikuwa wenye nacho wanaitunishia serikal, viongoz walikuwa wana bebwa na wana nchi na sio wana nchi wanabebwa na viongoz wao. Taifa ambalo kila mwenye nafasi alikula kwa ofisi yake na hakuna alie weza ulizwa au nyooshewa kidole na tume za maadili au rais.

Muungano wetu ulitiwa vidole na kukejeliwa na wapinzani. Ama kwa hakika hakuna alie thubutu kuwaambia watu wa zenji msicheze na muungano tutawabomoa. Rais wetu Magufuli ambaye ndie amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya Tz ametumia nafasi yake kama Rais kusimamia ukweli nakuwagusa mapapa wote ndani ya serikali jambo ambalo hapo mwanzo halikuwa jambo rahisi na wa Tz wote tunaona mabadiliko makubwa ambayo hata Rwanda ambaye ndio anaonekana kuwa na mafanikio makubwa kwenye serikal yake anaanza kuiga kwetu.

Ila ukiacha hayo yote nimeandika, kubwa lililo nifanya kuanza uzi huu ni baada yakufuwatilia vyombo vya habari na mitandao toka jana mpaka leo uchaguzi Znz umemalizika salama pasipo hata risas kurushwa au mabomu. Field Marshal Dk Magufuli ameibuka mshindi na uwenda chama chetu ccm kikanyakuwa dola kwa ushindi wa kishindo. Ndio maana nadirik kusema Magufuli is a new field marshal of Africa.
 
Safi sana bora umeona mapema kuwa Magu ndiye Filed Marshall mpya wa Africa. Naye anajiunga na wenzie waliokuwa na cheo kama hicho kina Idd Amin Dada, Gadafi, Bokassa, Hassan Hibre, Mengistu Haile Marium n.k....lets wait time will reveal his darkest side
 
Subiri wanakuja...ntarudi badae wakishatoka kwenye mech ya man u
 
Hivi ni zipi sifa za dikteta ili akitokea tuweze kumfahamu? Naomba mwenye ujuzi kidogo atudadavulie na sio kwa kumtaja mtu au kiongozi fulani. Mimi naomba tupewe sifa ili kila mtu afanye judgement mwenyewe!!!
 
Mimi ninaamini ni mapema mno kumsifia sana rais wa nchi hii. Ninaamini baada ya miaka mitatu tokea kuchaguliwa kwake ndipo tutakuwa na picha kamili kama tumeula au tumeliwa. Kwa sasa ngoja niwe mtazamaji zaidi.
 
Angalau siku tutakapomuona mzee wa vijisenti amepandishwa kizimbani ndipo tutaanza kuwa na imani na ulichosema.
 
Back
Top Bottom