[Tanzania]Potential to produce 735 million barrels of oil

Alpha

JF-Expert Member
Aug 30, 2007
662
251
It's just a matter of time

Australia's Key Petroleum upbeat on Tanzania

DAR ES SALAAM, Feb 5 (Reuters) - Australia's Key Petroleum Ltd said on Thursday its West Songo Songo licence in Tanzania had the potential to produce 735 million barrels of oil or 1.3 trillion cubic feet of gas.

The West Songo Songo area is between the already-producing Songo Songo gas field and the east African country's coastline. Key Petroleum is also developing a nearby field at Nyuni.

"Exploration and development work is rapidly increasing the value of these areas which form a significant part of Key Petroleum's international asset portfolio," the company said in a statement.

"The geological work that our team has been undertaking has provided us with some highly prospective targets in the West Songo Songo licence area," said Managing Director Ken Russell.

"Although at an early stage of evaluation these results provide us with a greater level of confidence in our Tanzanian interest," he said.


Australia's Key Petroleum upbeat on Tanzania | Markets | Reuters
 
....gas kibao lakini hata umeme wenyewe hatuna,gold kibao lakini njaa ndio imeongezeka,sasa mafuta sijui yatasaidia nini?
 
....gas kibao lakini hata umeme wenyewe hatuna,gold kibao lakini njaa ndio imeongezeka,sasa mafuta sijui yatasaidia nini?

Yataongeza 'wachukuaji' wakati Watanzania wengi wakiendelea kulala hoi na kuamka taabani. Na mafisadi ndiyo watazidi kukenua gego mpaka gego maana wanawza kusaini mkataba wa Tanzania kupata 1% na iliyobaki ikachukuliwa na 'wachukuaji'.
 
Yataongeza 'wachukuaji' wakati Watanzania wengi wakiendelea kulala hoi na kuamka taabani. Na mafisadi ndiyo watazidi kukenua gego mpaka gego maana wanawza kusaini mkataba wa Tanzania kupata 1% na iliyobaki ikachukuliwa na 'wachukuaji'.

Siipendi kauli yako lakini habari ndo hiyo. NAdhanoi kwa hali iliyopo inabidi JK awe makini mno vinginevyo yanaweza yakaja ya Delta Niger watu kulipua mamboa ya mafuta.

Ni her JK akubali lawama kuliko fedhaya kuiweka nchi kwenye kamtego ka mabomu ya petroli.
 
Wakulu mimi naona JK hii biashara ya mafuta haiwezi atuachie tutakaempata mwingine maybe ataimudu. Kwasababu sera zake kuu zitakuwa kama za Obama ''Economic stimulus''. Hii nikwa sababu JK atakuwa ashaufikisha uchumi wa Tanzania unyayoni kwani sasa upo magotini.

Nimefurahishwa na kauli kuwa ''siwaseme Tanzania bara badala ya Tanzania'' ha ha ha hawa ndugu zetu Zenji wanatakiwa waache ubinafsi kama tumekubali muungano basi vyote vyetu sio kutenga vitu muhimu kutoingia kwenye muungano.
 
NAdhanoi kwa hali iliyopo inabidi JK awe makini mno vinginevyo yanaweza yakaja ya Delta Niger watu kulipua mamboa ya mafuta.

Ni her JK akubali lawama kuliko fedhaya kuiweka nchi kwenye kamtego ka mabomu ya petroli.

ibrah, tukitaka tufaid hayo mafuta kama watz tusimwamin mtu yeyote. kuanzia president mpaka mtu wa chini kabisa. huko nyuma tulishawaamin sana lakin wametufanya na wanatufanya ndivyo sivyo. wengine kwa kutojua (wanaingia mikataba kama mongungo wa msovero - chifu) au kwa tamaa zao (kwa kuchukua au kutegemea rushwa).
tusiwaamin kwa vip?
tusimwamin mtu yeyote kwa kulikabidhi suala lote kwa mtu mmoja au mamlaka moja. kwamfano tukisema rais awe ndo mwamuz wa mwisho katka suala hili, anaweza kutuuza. leo tuna kikwete ambaye tunaamin sio fisad (japo mafisad labda wanamdrive), kesho itakuwaje? tuna uhakika wa kuwa na presidaa kama yeye? vip akitokea kuwa fisad?
mambo kama haya ni ya kuyaweka katka mikono ya watu wengi. kitu kama bunge. na kila kitu kiwe waz.
kumhonga kikwete au rais si vigumu kwa multinational companies. kuhonga kundi la watu wengi ambao wanaweza kubadilishwa na wanaoongozwa na taratibu imara zilizowekwa ni vigumu
 
mi naona wakishatuthibitishia tu, tusiharakishe tukae chini tujipange!! JK si wa kumkabidhi hii kazi, kashindwa na wezi walioiba hadharani, wataanza kupachika vitu vyao. Tujadiliane tuwe na mtu mwenye kutetea hii nchi si hawa wababaishaji.
 
Msondo Ngoma.....Mambo hadharani......Lazima mikataba iwekwe wazi, uficho wa makubaliano kati ya serikali na wachukuaji (sio wawekezaji) ndio unawanufaisha mafisadi na 10% zao. ....Sasa mambo hadharani....mambo msondo ngoma....
 
Well, Kuna anayefahamu mkataba kati ya Serikali na hii Kampuni ya "Australia's Key Petroleum Ltd." unasemaje? Kama Reuters walivyomnukuu kiongozi wa hii kampuni, inaonesha walishakabidhiwa kila kitu. Na nadhani, Serikali huwa haiwalipi/ haina uwezo wa kuyalipa haya makampuni yanayofanya "oil/mineral prospecting". So, huwa yanafanya hiyo kazi "at their own risk" or else, in anticipation of lucrative deal when they strike oil. I doubt if the Government own more than 10% of the whole deal.

I stand to be corrected!
 
Hata yakiwa kidogo yakwetu, na hata kama yatakuwa ujazo wa kinibu basi tutagawana tujipake.
 
Hawa nao! Kwa nini wasiseme Tanzania bara badala ya Tanzania?
Fundi wacha utani Bwana. Wewe ni msomi na unajua siku zote Unapotaja Tanzania Unamaana Tanzania Bara. Kwa hiyo ndiyo maana na sisi tunashadidia Zanzibar kumaanaisha Visiwa vyetu viwili pale tunapotaka kujieleza bila ya kuwamo Bara. Fanya reference si kuna Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( ambayo ndio Bara au Tanganyika -ukitaka) na kuna Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Two entities- hakuna ya tatu hapo. Fundi -analysis isikupige chenga Ndugu yangu- tena wakati huu.
 

Jk ndio kiongozi peke mpaka kufikia leo aliweza kuimarisha na kuitangaza TANZANIA katika ulimwengu na ndio leo hii tumeanza kufaidi matunda ya uongozi wake nikiongozi wa kupigiwa mfano katika bara hii la afrika kwa juhudi zake hata kufikia nchi za west wamemuona kuwa ni kiungo muhimu baina yao na nchi nyingine za kiafrika uwezo wake ni mkbwa katika kukabiliana na ugumu wa uongozi tusisahau sio muda mrefu alipongezwa kwa jinsi alivyo lishuhulikia maswali ya wizi wa EPA uwezo wa kushuhulikia mafuta anao tena mkubwa
 
Good news...but with greedy people like mafisadi, mafuta hayatakuwa na msaada sana. Tuzidi kuomba mungu mambo yabadilike haraka.
Mungu Ibariki Tanzania
 

I think you all need to hold your horses!! That paragraph is very misleading.
There is 'potential', and there is barrels of oil OR cubic feet of gas. Meaning they are not sure. You can not have a press release that is misleading like that. And since we know songosongo produces gas. Then y'all need to chill until its clear what they are actually saying.

Hawajasema wamequote percent gani inachimbika. Hiyo figure ni 10,50 au 90% (i.e P90,P50,P10)?
Kama ni mafuta, hiyo ni kama 10 to 15years of production, game over. Kama ni gas, haina faida kama hakuna soko la kutosheleza. Gesi haina faida kama huna soko locally, maana ni mtindo wa kusafirisha kwa mabomba.

Pia, kuhusu comission ya serikali, ni kweli hawa wanaingia na risk zao. Kampuni chache zinafungwa na kuja upya, maana una-explore weee, ukiishiwa unanunuliwa au unakuja upya heheee. Hata hawa jamaa walitumia jina jingine muda uliopita.
 
Hawa nao! Kwa nini wasiseme Tanzania bara badala ya Tanzania?

Hakuna haja ya kufanya hivyo kwani inajulikana wazi kuwa Tanzania ni Tanganyika na Zanzibar ni Zanzibar. Hebu angaliamajina kama TFF, TIPPER, TRA, TPC, TABA, BMT na nyenginezo na kwa upande mwengine ZFA,ZAPHA, ZRA, BAZA, BMZ na kadhalika.
Ni ukweli unaotambulika kuwa kimasilahi Tanzania ina maana tanganyika na Zanzibar ni sehemu tofauti na hiyo "Tanzania"
Angalau kwa hili la mafuta ya Songo Songo hakuna malumbano kwani katiba iko wazi kuwa maliasili ya Bara ni mali ya Bara lakini ya Zanzibar bado mgogoro kwani na wao wanataka wawe kama kaka zao, eti nao wamiliki raslimali yao. Hawajijui kuwa wao ni Bwana mdogo chao lazima kilindwe na kaka.
 
Yataongeza 'wachukuaji' wakati Watanzania wengi wakiendelea kulala hoi na kuamka taabani. Na mafisadi ndiyo watazidi kukenua gego mpaka gego maana wanawza kusaini mkataba wa Tanzania kupata 1% na iliyobaki ikachukuliwa na 'wachukuaji'.

Hakuna tofauti kwani tukiyaacha hayatusaidia kitu lakini wakifaidika Mafisadi watawajengea majumba watoto wao na vimada wao nasi walalahoi tutatia macho nuru. Pia vibarua wajaa jasho watabangaiza kwenye miradi ya visaluni na tamaa haitaishia hapo hivyo wataanza kujenga viwanda hivyo ajira kwa wajaa jasho. Siku zinasogea kwani hakuna muelekeo kuwa wananchi watawashinda mafisadi.
 
Wakulu mimi naona JK hii biashara ya mafuta haiwezi atuachie tutakaempata mwingine maybe ataimudu. Kwasababu sera zake kuu zitakuwa kama za Obama ''Economic stimulus''. Hii nikwa sababu JK atakuwa ashaufikisha uchumi wa Tanzania unyayoni kwani sasa upo magotini.

Nimefurahishwa na kauli kuwa ''siwaseme Tanzania bara badala ya Tanzania'' ha ha ha hawa ndugu zetu Zenji wanatakiwa waache ubinafsi kama tumekubali muungano basi vyote vyetu sio kutenga vitu muhimu kutoingia kwenye muungano.

Wakishaondowa gesi, dhahabu, almasi na tanzanite. Hivi wastutake muhali ni vya kwetu peke yetu, AU SIVYO WAKULU?
 
Well, Kuna anayefahamu mkataba kati ya Serikali na hii Kampuni ya "Australia's Key Petroleum Ltd." unasemaje? Kama Reuters walivyomnukuu kiongozi wa hii kampuni, inaonesha walishakabidhiwa kila kitu. Na nadhani, Serikali huwa haiwalipi/ haina uwezo wa kuyalipa haya makampuni yanayofanya "oil/mineral prospecting". So, huwa yanafanya hiyo kazi "at their own risk" or else, in anticipation of lucrative deal when they strike oil. I doubt if the Government own more than 10% of the whole deal.

I stand to be corrected!

I remember once you suggested (of course not to mainlanders)that oil might not benefit the owners and that they should stop recovering it, do you still beleave that suggestion can apply in this case,sir?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom