mteule
Senior Member
- Aug 2, 2007
- 149
- 252
Mkuu mimi sio mbishi lakini hapo kwa 95% naomba kubisha. Samahani. Ukiangalia mchango wa kisekta kwenye uchumi, kilimo, ambacho kinategemewa na zaidi ya asilimia 80 ya watanzania kinachangia takriban asilimia 25 ya pato la taifa( uchumi). Kumbuka pia shughuli za serikali ( public adimin) nazo zina mchango wake katika uchumi. Kwa talkwimu za mwaka 2010 shughuli za serikali zilichanigia takriban 20% ya pato la taifa. Kwa kuangalia hizi sekta mbili sioini jinsi ya kusema kwamba asimia 95 ya uchumi wa TZ uko mikononi mwa wageni. Ni kweli zipo sekta amabazo zinamilikiwa kwa kiasi kikubwa na wageni, lakini mchango wa sekta hizo kwenye uchumi ni mdogo. Mfano sekta ya madini pamoja na kukua kwa kasi sana inachangia asilimia 2.5 tu ya pato la taifa( 2010). Hoteli na migawa inachangia asilimia 2 tu ya pato lataifa. Mawasiliano( akina voda, airtel tigo, zantel n.k) yanachangia 3% ya pato la taifa, kwa mujibu wa takwimu za 2010. Yote katika yote, nafikiri si sahihi kusema kwamba 95% ya uchumi wa Tanzania uko mikononi mwa wageni.
Sawa mkuu naona figure zako ni kwa mujibu wa makabrasha yaliyotengenezwa na serikali ambayo imeingia mikataba feki inayosababishia hasara kubwa.
Mkuu ningependa uje na figure za kiasi cha fedha zinazopotea kutokana na ineffieciency ya
*ukusanyaji kodi
*mikataba ya kinyonyaji