Tanzania: Nini tatizo letu kama Taifa? Tunajikwamuaje?

wanasema kulindana pia ahadi hewa za viongozi navyo vinachangia kwa kiasi kikubwa kutoisha kwa matatizo yetu.

Tuna watu, ardhi, siasa safi, kwanini hatuendelei?

Osoro Nyawangah

TAKRIBAN miaka 45 sasa baada ya Jamhuri ya Tanzania kujitawala kutoka katika minyororo ya wakoloni, bado taifa hili lililojaliwa kuwa na akiba kubwa ya rasilimali nyingi na za kuvutia linaendelea kulia kilio cha umaskini uliokithiri miongoni wa jamii, licha ya kuwapo mikakati mingi ya kupambana na umaskini huo.

Katika mahojiano na baadhi ya wananchi, wapo ambao tayari wamekwisha kukata tamaa kuwa serikali yetu imeshindwa kabisa kupambana na umaskini na matokeo yake imeamua kuwaacha wananchi wapambane na adui huyo kwa mbinu na staili binafsi.

Lengo kuu la kupambana na wakoloni katika nchi nyingi za Kiafrika ilikuwa kuwawezesha wazawa kukamata hatamu za uongozi ili kuweza kuongeza kasi ya kujenga uchumi wa taifa ili wazawa waweze kufaidika na maliasili na rasilimali za taifa walizopewa na Mungu.

Mara baada ya kupata uhuru, Tanzania chini ya uongozi ‘shupavu’ wa Mwalimu Julius Nyerere, ilitangaza vita kabambe dhidi ya maadui watatu wakuu wa taifa hili ambao ni ujinga, maradhi na umaskini, maadui ambao hata leo hii hakuna dalili ya kuonyesha kuwapo na mafanikio ya kuwashinda.

Kumekuwapo maazimio mengi yaliyotangazwa na taifa kupitia Chama cha TANU na ASP, na baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambayo yalilenga kuleta msukumo na mbinu mpya za kupambana na maadui hao watatu ili kuwajengea wananchi wetu angalau ahueni ya maisha ili nao wafurahie matunda ya uhuru.

Azimio la Arusha, Azimio la Musoma, Azimio la Iringa, Azimio la Zanzibar na milolongo mingine ya maazimio yaliyolenga kwa dhati kulikwamua taifa hili ndani ya lindi la umaskini, maradhi na ujinga, hadi leo kuna watu wanaishi katika taifa hili wakiwa hawana fedha za kujinunulia hata mlo mmoja wa chakula kwa siku, hawajui kusoma na kuandika licha ya kuwapo utitiri wa shule za msingi za bure na wengine wengi wanapoteza maisha kutokana na maradhi yenye kinga na tiba.

Nyerere katika moja ya hotuba zake ambazo kwa kiasi kikubwa zilitoa dira ya uongozi wa taifa, aliwahi kusema ili taifa liendelee, linahitaji mambo makuu manne: Watu, ardhi siasa safi na uongozi bora.

Tanzania kama moja ya mataifa barani Afrika, tumejaliwa kuwa na watu wengi wenye nguvu na ari kubwa ya kufanya kazi, tuna ardhi kubwa na yenye rutuba nyingi ambayo hadi sasa kuna maeneo ambayo hayajawahi kulimwa na mtu yeyote licha ya kukanyagwa, kila baada ya miaka mitano tunaendesha uchaguzi wa kuwapata viongozi ‘bora’,

kutokana na uchaguzi huru na wa haki, kila mara na chama kinachoongoza taifa hili ni kile kile ambacho kila siku kinajinadi kwa kuwa na sera na siasa safi, je, falsafa hii ya Nyerere ina kasoro?

Mbona tuna vitu hivyo vyote ambavyo ni muhimu kwa taifa kuendelea lakini bado wananchi wetu wanaendelea kuimba wimbo usio na muitikiaji wa umaskini uliokithiri?

Mbona watu wetu wanaendelea kufa kutokana na maambukizi ya malaria, homa ya matumbo na utapiamlo? Kwa nini bado tuna asilimia kubwa ya wananchi wasiojua kusoma, kuhesabu na kuandika?

Hapa ndipo tunapata changamoto ya kutaka kujua kile kinachotukwaza katika kupiga hatua madhubuti za maendeleo. Licha ya kuwa na vitu hivyo muhimu, hapa ndipo inapofikia wakati tunataka kuuliza uhalali wa siasa na sera zinazotuongoza na uhalali wa viongozi tulionao.

Kwa mtazamo wangu, taifa hili haliwezi kuendelea endapo tutaendekeza uongozi wa kulindana katika nyanja mbalimbali za uongozi, hatutaendelea endapo tutaendekeza viongozi wanaoendeleza blabla na propaganda za siasa za umimi na kujitafutia umaarufu, nitatoa mifano.

Hivi karibuni katika kikao cha Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Magu, mhandisi wa maji alitoa taarifa ya utekelezaji wa mwaka ambapo alieleza jinsi alivyotumia mamilioni ya fedha kukarabati malambo na kuweka pampu za mikono kwenye visima katika vijiji mbalimbali, lakini wakati madiwani walipoanza kuhoji uhalali wa taarifa hiyo, ilibainika kuwa lambo moja la Lwangwe ambalo lilitajwa kuwa limekamilika kwa asilimi 80 halipo kabisa.

Pia ilibainika kuwa pampu zilizofungwa kwenye visima hivyo zilikuwa hazina ubora kiasi ambacho diwani mmoja alidai kuwa katika kijiji chake pampu iliyopo ina uwezo wa kujaza lita 60 tu za maji kwa siku. Hizi ndizo taarifa zinazotamalaki katika halmashauri zetu.

Taarifa ya Ofisa Kilimo/Mifugo pia haikuonyesha matumizi ya jumla ya sh 20,000,000 zilizotolewa kukarabati majosho manne wilayani hapo na pia ameshindwa kuandika taarifa ya jinsi alivyotumia fedha za awali katika miradi hiyo ili apewe kiasi kingine cha fedha.

Licha ya kuwapo dosari hizo za wazi ambazo zimerudisha nyuma maendeleo ya wananchi katika sehemu husika, bado viongozi wa halmashauri hiyo wameshindwa kuwachukulia hatua watendaji wa aina hiyo, kitu kinachojenga hisia kuwa nao ni washiriki katika uhalifu huo.

Haiwezekani mtendaji aandae taarifa ya mwaka na akasahau matumizi ya kiasi kikubwa cha fedha kama hicho, pia haiwezekani ikaandaliwa taarifa ya lambo ambalo halipo kabisa lakini watu hao wakaendelea kukalia nyadhifa zao, kuna kitu.

Takriban miezi mitatu iliyopita, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Juma Abubakar, alitoa ahadi ya ‘nguvu’ ya kuwapatia mchele magunia matano watoto yatima wanaolelewa katika Kituo cha Bethany Family baada ya kuguswa na hali yao na jinsi wanavyokosa upendo wa mama zao ambao hawapo tena.

Yeye kama mzazi alitoa ahadi hiyo ambayo iliamsha ari kubwa miongoni mwa jamii ya kuona umuhimu wa kuwasaidia watoto yatima na wale walio katika mazingira magumu ambao wanaongezeka kwa kasi ya ajabu kutokana na kuendelea kuenea kwa maambukizi ya UKIMWI, lakini hadi sasa bado watoto hao hawajapokea mchele huo!

Hizi ndizo ahadi za viongozi wa kisiasa ambazo badala ya kuchochea maendeleo ya jamii, zinatolewa kwa lengo la kujipatia umaarufu na baadaye hazitekelezwi.

Viongozi wa kituo hicho wamefuatilia hadi wamechoka na wamesema kuwa hawataki mgogoro na serikali.

Mfano mwingine ni ule wa uteuzi wa eneo la kujenga makao makuu ya wilaya ya mpya Rorya, mkoani Mara, ambapo madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wamependekeza kuwa makao hayo yawe kwenye Kijiji cha Utegi badala ya mji wa Shirati au Kijiji cha Randa, ambacho kipo katikati mwa jimbo hilo.

Kimsingi haya ni maamuzi ya kisiasa ambayo yanalenga kumjengea mtu mmoja au baadhi ya watu umaarufu binafsi bila ya kujali masilahi ya jamii husika katika eneo hilo, kwa sababu unapoamua kujenga makao ya wilaya kwenye eneo ambalo liko pembezoni mwa jimbo, hauwatakii mema wananchi watakaoathirika kwa umbali unauchochea.

Mimi ni mmoja wa wakazi wa jimbo hilo, nimefarijiwa sana na uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete, kwa wakazi wa jimbo hilo kupata wilaya, lakini uamuzi huo tayari umenyakuliwa na baadhi ya viongozi wenye uchu wa kunufaisha nia na dhamira zao binafsi na kusahau hali na umaskini unaowakabili wapiga kura wao kwa maslahi binafsi.

Kimsingi, Shirati si katikati ya jimbo hilo na kama mimi ningekuwa mmoja wa wapiga kura, ningeipigia Shirati kura kwa sababu kuu moja kuwa ina miundombinu yote muhimu kwa ajili ya kuwa makao makuu ya wilaya; ina mahakama, hospitali kubwa mbili, shule za sekondari tatu, bandari, uwanja wa ndege, ofisi za Uhamiaji, posta, mtandao wa maji ya bomba na kuna idadi kubwa ya watu na eneo kubwa la kujenga makao ya serikali.

Kwa mantiki hiyo inakipiku Kijiji cha Utegi ambacho najua kimepigiwa kura kutokana na sababu kuu moja kuwa Mbunge na Mwenyekiti wa halmashauri wanatoka katika eneo hilo, na hakina miundombinu.

Hivyo, kukijenga kijiji hicho kuwa makao makuu ya wilaya kutawagharimu sana wakazi wa jimbo hilo ambao hadi sasa wanakabiliwa na matatizo lukuki, ikiwamo umaskini uliokithiri kutokana na kukosa zao la biashara la uhakika.

Bado pamekuwapo mikakati mingi ya kuendeleza mazingira ya Ziwa Victoria kupitia miradi mbalimbali inayoingiza fedha kutoka kwa wafadhili au mikopo kutoka mashirika mbalimbali; kumekuwapo makongamano, semina na warsha nyingi zilizokwisha kufanyika kwa jina la hifadhi ya Ziwa Victoria lakini yako wapi matokeo?

Bado kuna uharibifu mkubwa wa mazingira unaendelea kandokando mwa ziwa hilo kwa kasi ya ajabu huku viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia hifadhi yake wakiendelea kuandika maombi mengine ya mikopo bila kujua kuwa kwa kufanya hivyo wanatuendelezea mzigo mkubwa wa madeni.

Ziwa hili limeendelea kuharibika kwa kasi ya ajabu kutokana na maamuzi ya kisiasa, samaki wamepungua na sasa kuna taarifa kuwa hewa ya oksijeni nayo imepungua kwa kiasi kikubwa na hivyo kuhatarisha uhai wa ziwa hilo.

Ili tuendelee tunahitaji uongozi bora na si bora uongozi, tunahitaji siasa safi na si siasa zenye kaulimbiu za ajabu kila kiongozi anapochaguliwa!

Tunahitaji viongozi wanaojali watu waliowachagua na si wale wababaishaji na wanaopiga propaganda.

Ukienda mkoani Kilimanjaro utaona jinsi kilimo cha kahawa kilivyosimamiwa na viongozi wa mkoa huo na kubadilisha maisha ya wanachi wa eneo hilo, utaona jinsi wananchi walivyojengewa uwezo wa kuwahoji viongozi wababaishaji.

Katika Kanda ya Ziwa, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini, mabonde ya nafaka, mbuga za wanyama na ziwa, hali ya wakazi wa eneo hili ambao kwa mujibu wa takwimu za Tume ya Uchaguzi ndio wapiga kura wakuu kwenye chaguzi za kitaifa, lakini eneo hili limeendelea

kuwa duni kiasi cha wakazi wake kushindwa kujinunulia hata kiti cha kukalia katika kaya.

Kwa nini tuendelee kuendekeza siasa ndogondogo za kibinafsi kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya? Je, kwa hali hii tutaweza kweli kuwatokomeza maadui hao?

osoropjn@yahoo.co.uk

Makala -Tuna watu, ardhi, siasa safi, kwanini hatuendelei?
 
Nadhani uzalendo ndio msingi mzuri mambo ya elimu hayajatutalia matatizo kwani kuhitimu na kuelimika ni vitu viwili tofauti wazee wetu hawakwenda shule lakini walipanga mipango madhubuti na jamii yote ilineemeka mwenye njaa alisaidiwa na mengi mazuri. Leo hii hao tunaowaita wasomi hata ustaarabu tu wa kuishi na jirani hawana, watoto wa wasomi wamekuwa kero kwa jamii utaona hapa elimu tunayopata hatusaidii ktk maisha yetu ya kila siku badala ya kuwa sehemu ya kutatua matatizo ya jamii wasomi wamekuwa sehemu ya kuleta matatizo kwa jamii yetu. mfano mtu kasomeshwa bure hadi chuo kikuu lakini akipewa kitengo cha elimu yuko radhi kupanga ada milioni moja kwa sekondari. kuna watu wako wizarani elimu lakini pia wanafungua shule mtaani na kuchaji kiasi hicho.pia vyeti vya uongo kuna watu wako nje kununua vyeti badala ya kusoma je hao ni wasomi ambao watasaidia
 
Mswahili, Hapo ninakubaliana na wewe kabisa!

Mtu akiwekwa katika Hospital ya serkali anaanza kufiri juu ya kuanzisha ya kwake!

akiwa wizara ya elimu anafikiria kuanzisha shule zake binafsi!

Wakiwa wahasibu wa wilaya au Halamashauri wanafikiria kujuizia masoko, maghulio yote! na hii mentality ililetwa sana na BWM!
 
Mzee Es said:
Mzee JK, ni kiongozi naturally I mean hiyo lazima tumpe credit yake wheree it is due, anao uwezo wa kuongoza yaani yeye kuwa mbele na wengine wakafuata nyuma,

ila swali ni kwamba anao uwezo wakuongoza katika haya mazingara ya leo ambayo ni very complicated?

One thing for sure ni kuwa sio msomi, yaani JK sio intellectual,

Halafu viongozi wakuu wa nchi yetu wanasisitiza kuwa eti Tanzania bado ni nchi ya ujmaaa na kujitegemea mpaka kesho, wanasema kama anayetaka kutafsiri tofauti ni RUKHSA, lakini as far as CCM is concerned bado ni siasa ile ile ya ujamaa!

Heshima yako Mzee,

Unaweza kutusaidia kutuonyesha ukweli kwamba JK ni kiongozi "naturally"?Angalau mfano mmoja tu utatosha.Nadhani angekuwa kiongozi naturally as you suggested asingetuletea cabinet ya watu 60 ambao takriban nusu yao wana CV zenye walakini.Na ile ya kusema kuwa majina ya wala rushwa anayo ila anawapa muda wabadilike is definitely not a character of a natural-born leader.

Halafu,kama kweli yeye ni leader by nature,kwanini kuwe na hofu ya kuongoza katika "mazingira ya leo ambayo ni very complicated" (hujafafanua).Nadhani JK ana mvuto flani ambao ni rare,lakini hata hivyo mvuto huo was groomed for about a decade tangu Mwalimu amwekee mizengwe in favour of Ben Mkapa in 1995.We all know,Bongo fedha can make an ugly person look like Brad Pitt.

And I dont think JK isnt intelligent,because it takes more than intelligence to concort such a winning strategy as exhibited in the last Election.
 
Salamu zenu waheshimiwa, na baada ya wiki nzito, mawazo yangu yametulia kiasi na kuweza kuendelea kutoa mchango katika mada mbalimbali hapa. Mengi yamesemwa na kuyarudia itakuwa ni kupoteza muda. Lengo langu hata hivyo nataka niliangalie swali la mada "Nini tatizo (matatizo) letu kama Taifa?" kwa kuliangalie toka upande tofauti.

Hadi hivi sasa inaonekana kuwa tatizo la Tanzania si moja bali ni mkusanyiko wa matatizo kadhaa ambayo ni Elimu, Uongozi, na Uzalendo. Hata hivyo kwa maoni yangu vitu hivyo havitaji hasa tatizo la Watanzania ni nini. Baada ya kufikiri kwa kina nikipita hoja za watu wengi humo, nimefikia mahali ambapo nimejikuta nikikiri ingawa kwa kigugumizi tatizo letu kama Taifa hasa ni nini.

Tatizo ambalo tulilonalo, ni tatizo ambalo pia linakabiri nchi nyingi za Kiafrika na zile zingine za dunia ya tatu. Nchi chache za dunia ya tatu zilizoweza kulishinda tatizo hilo ndizo leo hii zimeanza kujijenga na kuonesha mafanikio makubwa ya kiuchumi na kimaslahi ya raia wao. Ni tatizo hilo Wachina, Wahindi, Wamalaysia, Wa Indonesia na Wa Korea Kusini wamelishinda na leo wapo ambapo wapo. Na sisi kama tunataka kweli kuleta neema kwa wananchi wetu ni lazima tulikabili tatizo hilo.

Tatizo ninalolizungumzia siyo elimu, hata hivyo linajionesha katika elimu yetu. Tazizo hilo siyo uongozi, ingawa linajionesha katika uongozi wetu. Na tatizo hilo siyo uzalendo ingawa linatukodolea macho kwenye uzalendo wetu. Hatutaweza kujenga jamii ya kisasa, yenye mafanikio na ya kiafrika hadi pale tutakapoamua kulikabili tatizo hilo kwa mbinu za makusudi na za dhati. Hapo ndipo Tanzania ile tuiotayo itakapodhihirika.

Tatizo hilo nini basi? Nikitumia neno moja, tatizo letu kama taifa ni KUTOKUJIAMINI (lack of self confidence). Watanzania hatujiamini kuwa sisi

a. Tunaweza kufanya mambo makubwa na siyo madogo madogo
b. Tunastahili mambo mazuri na siyo mabaya na mabovu bovu
c. Tunapaswa kufanya mambo ya haki na kisheria na siyo ya kupindapinda.

a. Kutokujiamini kufanya mambo makubwa.
Waswahili walisema msemo huu wenye maana kubwa, "Ukiona vyaelea vimeundwa". Watanzania tunaangalia Marekani, Ulaya na Asia, tunapigwa na butwaa na kushangaa jinsi gani wenzetu wamepiga hatua kubwa ya maendeleo na mafanikio. Badala ya kufikiri kuwa hivyo vyote "vimeundwa" na wanadamu tunadhania hivyo "vimeshushwa" na muumba! Marekani haikutoka mbinguni, wala Ulaya haikunenwa ikawa! Kuna watu waliojitoa mhanga kuijenga Marekani ya leo na kuiunda Ulaya tunayoifurahia. Hata Japani haikutolewa njozini!

Kuna watu wa nchi hizo waliojiamini kuwa wao wanaweza kufanya mabadiliko na wakati mwingine kuweka rehani mali na maisha yao ili kufanikisha lengo lao. Miaka michache baada ya uhuru, Watanzania tulianza kujiamini na kusema na sisi "tunaweza" tukaanza kujenga shule, barabara, hospitali n.k lakini baada ya muda si mrefu, tumejikuta tukirudi nyuma na kuanza kuomba msaada wa wazungu kutuendeshea mashirika yetu, idara zetu, na hata kutupa mawazo ya nini kifanyike. Tumefikia mahali kuwa hatujiamini kiasi cha kwamba kuna maporomoko ya maji huko Iringa ambayo kama yangegeuzwa bwawa basi tatizo la umeme wa Mtera lingepungua kama siyo kutoweka kabisa! Waliofahamu jambo hilo hawakujiamini kuwa wangeweza kuleta tofauti kama wangelipigia kelele jambo hilo. Leo wanamsubiri Waziri Mkuu kuwaambia kuwa wanaweza!

Kutokujiamini huku kunadumaza ubunifu na kuzorotesha mawazo mapya. Kama nilivyosema mahali kwingine, watu wenye hisia za namna hawako tayari kusikiliza watanzania wenzao wakitoa mapendekezo ya mambo mazuri ya kufanywa kwani hatuwaamini kuwa wanaweza kuwa na mawazo mazuri. Cha kuudhi ni kuwa wazo hilo hilo likitolewa na Mr. John Smith wa NGO fulani, basi tunakuwa wa kwanza kulikumbatia na kujiuliza “kwanini hatukufikiri hivyo mwanzoni?”!

Hadi pale tutakapoweza kujiamini kuwa na sisi tunaweza "kuiunda" Tanzania yetu basi tutaendelea kudumaa na kuendelea kukodolea vilivyoundwa na wenzetu. Tutaendelea kuimba nyimbo za kusifia vilivyoundwa na wenzetu!

b. Kutojiamini tunastahili mambo mazuri
Hili linaoonekana sana kutokana na tabia ya Watanzania kuzoea vitu vibovu na visivyofanya kazi. Mtaa ukiwa na taa zinazoangaza kila kona, watoto (wakati mwingine hata watu wazima) wataanza kuzitungua!! Mfereji unapojengwa wa kupitisha maji machafu sisi tunaugeuza dampo na mahali pa watoto kuchezea! Juzi juzi mmeona picha ya wanafunzi wa chuo kikuu wakiwa wamekaa sakafuni wakisikiliza mhadhara. Tunaliona hilo na kucheka, kwani ni la kawaida. Kwa sababu hatujiamini ya kuwa tunastahili vitu vizuri na vyenye kurahisisha maisha yetu basi tunaendelea kuviendeleza vitu vibovu na vilivyopitwa na wakati. Ajali ya hivi karibuni ya huko Kibaha ni mfano dhahiri. Dereva anakwenda kasi na hajali sheria za usalama barabarani, watu tunakaa kimya hadi ajali inapotokea.

Hili pia laweza kusema pale ambapo ofisi fulani inatakiwa kufanya jambo fulani kwa wananchi, lakini kwa vile wananchi wamekubali kuwa ofisi hiyo haijawahi kufanya jambo zuri basi watu wanakubali hali halisi (status quo) badala ya kupinga na kutaka kitu chema. Ni mara ngapi umeenda hospitali au kwenye ofisi ya serikali ukajipanga foleni na kabla ya zamu yako kufika mtu mwingine ambaye anajuana na yule wa kwenye kaunta anakupita na kuhudumiwa kwanza? Wewe unabakia kuguna? Tumezoea kupatiwa na kutendewa vibaya kiasi cha kwamba tunapopatiwa na kutendewa vizuri tunasema “kipofu kaona mwezi”! Hilo linatushangaza, na tunapiga magoti kushukuru kudra za Mwenyezi Mungu.

Ni hadi pale basi tunapoweza kuamini kuwa na sisi tunastahili huduma nzuri, mahali pazuri pa kusomea na kufanya kazi, maisha mazuri, hapo ndipo tutaweza kutaka mabadiliko na kusababisha mabadiliko!

c. Kutojiamini kuwa tunapaswa kufanya mambo ya haki na ya kisheria.
Kama kuna kitu kinachotudumaza kufanya mabadiliko ya kweli na kujiletea (sijasema kuletewa) maendeleo ya dhati ni uduni wa kutokujiamini kuwa tunapaswa kufanya mambo ya haki na kisheria. Watanzania (kwa ujumla wetu) tumezoea kupinda sheria au kujifanya kana kwamba sheria hazipo. Tumezoea kuzunguka sheria kiasi cha kwamba kufuata sheria na wajibu kinakuwa ni kitu cha ajabu. Sheria inakataza jambo fulani na taratibu zilizopo zinafafanua nini hakiwezi kufanyika. Cha kushangaza ni kuwa anatokea mtu ambaye kwa makusudi anaamua kufanya jambo kinyume na sheria au taratibu zilizopo. Badala ya kusimama na kumkemea na hata kumchukulia hatua tunakubali kuwa hivyo ndivyo ilivyo na ya kuwa “Mkuu kasema” basi linafanyika.

Fedha zimetolewa kutekeleza mradi fulani, wakuu wa kitengo au idara hiyo badala ya kutekeleza yale yaliyomo kwenye pendekezo la mradi huo wanaanza kufikiria ni jinsi gani pesa zile zitapishwa kwenye makampuni ya marafiki zao au ndugu zao ambapo watakatiwa kitu kidogo. Watu wanaliona lakini mtu anaogopa kusema kwani ataonekana “si mwenzetu” na nafasi yake kazini inakuwa hatarini kwani hadi hivi sasa hatuna ulinzi kwa “mpiga kengele ya tahadhari” Ni kwa sababu hiyo basi, vitu hivi vya kupinda sheria vinaendelea na kila mwaka Mkaguzi Mkuu wa serikali anakuja na taarifa akisema kuwa “idara fulani imepoteza shilingi bilioni hizi na hizi na hazijulikani zilivyotumika”. Watu tunang’aka lakini then, tunasema “watanzania hao” na tunaacha mambo jinsi yalivyo!

Unawezaje kujenga taifa lenye maendeleo wakati badala ya watu kujenga wanajitahidi kubomoa? Mtu kateuliwa uwaziri cha kwanza anajaribu kufikiri ni jinsi gani atajinufaisha na kuwanufaisha watu wa karibu yake, ili siku akiondoka awe na pa kufikia? Tutawezaje kujenga Taifa la kisasa kama sheria zilizopo zinapindwa na kuvunjwa hadharani na watu wakubwa, lakini ni wadogo ndio wanaokamatwa? Vyama vingapi vya ushirika vilivyokufa, makampuni mangapi ya umma yaliyofilisika, na idara ngapi ambazo zimeshindwa kufuata bajeti zao na vigogo wao bado wanadunda kwenye mfumo bila ya kukutwa na lolote (with impunity)?

Ndugu zangu, ni hadi pale watoto wa Tanzania watakapojenga moyo wa kujiamini hapo ndipo wataanza kuonesha jinsi gani wameelimika na siyo kupata elimu, wamekuwa wazalendo na siyo wajiitao wazalendo, na wamehamasika kiuongozi badala ya kuvisha migololo na kushikishwa ngao za kijadi kuashiria kuwa ni viongozi!

Swali kwenu, ni jinsi gani tunaweza kujenga jamii ya watu wanaojiamini? Binafsi ni mapendekezo kadhaa lakini kwa sasa nasubiri mawazo yenu.

Kwa sababu nimeandika kwa kirefu, nawapatia kiungo hapa ambapo unaweza kudownload hoja yangu hapo juu kama faili la pdf na uichapishe na kujisomea katika muda wako.
 

Attachments

  • kutokujiamini.pdf
    9.5 KB · Views: 98
Mwanakijiji,
Nikiazima msemo au kaulimbiu ya kampuni fulani ya simu hapa Bongo siku zilizopita, "Now You Are Talking!"

Nashukuru pia kwa kuweka ambatisho ambalo baadhi yetu tunaweza kufanya rejea.

Kama nilivyowahi kuchangia huko nyuma kwenye mada hii, ni kweli tunahitaji "dozi" ya vitu mbalimbali vikiwemo ELIMU na UZALENDO na KUJIAMINI, nawe umesema hivyo. Baada ya kujiuliza tena na tena, naona kwamba, ili tuweze KUJIAMINI huko tunakokutaka, basi tunahitaji ELIMU na UZALENDO! Kwa maana nyingine, KUJIAMINI ni matokeo ya Elimu na Uzalendo. Tuhakikishe kuwa watu wetu wanakuwa na elimu itakayowafanya wajiamini kuwa wanaweza...

Lakini ajabu ni kwamba, ili watu hao (viongozi?) waweze kuwapatia watu wetu (wananchi) elimu hiyo inabidi wawe wazalendo kwanza, ili kuweza kujali mustakabali wa taifa letu! Kiasi fulani inakuwa hadithi ya kuku na yai, nani aanze au alianza! Na si ajabu hakuna mwananchi au kiongozi ANAYEJIAMINI kuwa haya yanawezekana, hivyo tutasubiri Bush au Benki ya Dunia, ndiyo waje watuwezeshe! Naona kizunguzungu!!

Lakini tuendelee kujadili.
 
BARUA YA WAZI KWA MSAJIRI WA VYAMA

Watanzania Tutatue Tatizo letu Kubwa Kwanza – Halafu Tutajenga Demokrasia na Uchumi Kirahisi

Ndg Msajiri,

Tanzania ni nchi nzuri. Watu wake ni wema na wakarimu. Tanzania yaweza kugeuka na kuwa Taifa lenye nguvu ya uchumi kuliko Taifa lolote kama tutazingatia hili.

Namna pekee ya kupata mabadiliko ya kweli ya kisiasa na kiuchumi Tanzania ni kwa wewe, Msajiri wa Vyama vya Siasa nchini kukifuta chama cha Mapinduzi.

Sababu ni hizi:
Chama cha Mapinduzi kimejivisha madaraka makubwa sana. Amini usiamini chama hiki kina nguvu kuliko Bunge, Serikali, Mahakama au chombo kingine chochote hapa nchini.

Chama hiki kina uwezo wa kuvunja sheria yoyote ya nchi bila kufanywa lolote na yeyote. Kina uwezo wa kuvunja sheria ya nchi halafu kikaliagiza jeshi la polisi na mahakama nini cha kufanya!
Viongozi wake wanaweza kukaa miaka 5 bila kufanya lolote la maendeleo kwa taifa, halafu wakati wa uchaguzi wakamwagiza mtu au taasisi yeyote ikipe chama fedha na mtu huyo akashinda uongozi tena.

Chama hiki pia kimetambua kuwa namna ya kuendeleza ufisadi ni kuhakikisha kwamba watanzania wanaendelea kuwa maskini siku zote ili wawe waoga na wasiwe na hoja. Ukiwapa sh. 10,000 au 100,000 umepata uongozi bila maswali!

Umaskini wa watanzania sio swala la hali ya nchi au hali ya hewa. Ni wale wanaojiona wajanja wachache sana wamepanga hivyo!

Chama hiki pia kinatisha. Wanachama wake ambao wangeweza kuwa viongozi wazuri (na kinao wengie kimewaficha) wanagwaya kukohoa (kusema ukweli kwenye matatizo) au kutoka kwenye chama hiki. Kupata uongozi Tanzania sio kwa sifa za utendaji bali ni kwa jinsi unavyoweza kutii wakubwa hata kwa jambo ambalo ni kinyume kabisa na maadili au hekima za kawaida za binadamu.

Kimelifanya jambo la kutoka kwenye chama kama kosa la ki-ugaidi. Hivyo wengi hawathubutu!
Lakini kina wanachama ambao wanaweza kuwa viongozi wazuri sana na watendaji wazuri sana kama nchi yetu ingekuwa na uhuru na demokrasia ya kweli. Lakini watu hawa wamezidiwa nguvu na Chama hiki.

Chama hiki kimekuwa ni taasisi iliyo mbele kuvunja sheria za nchi kuliko mtu au taasisi yeyote nyingine.

Namna ya kuleta mabadiliko ya kweli ni kukifuta chama hiki kwa sababu ya ufisadi na uvunjaji wa sheria za nchi uliokithiri ili wanachama wake watawanyike kwenye vyama mbali mbali na kuwe na balance ya nguvu za kufanya maamuzi za kisiasa.

Kwa matendo yake chama hiki hakina tofauti na mtu anayeanzisha chama kwa sababu za ugaidi au ufisadi - HASTAHILI. CCM HAISTAHILI pia. TUIWEKE KWENYE JUMBA LA MAKUMBUSHO kwa kumbukumbu na historia yetu watanzania. Sasa hivi hamna lolote jipya ndani ya CCM.

Kumbuka silaha yao kubwa ni wingi wao. Na hatari moja ya "demokrasia" ndio hiyo: kura nyingi ndio ushindi. Wendawazimu wakiweza kujiunga kwa wingi wakawa wanafanya maamuzi yao ya kiuchizi-uchizi (ukiwahoji machizi hao watakwambia kwamba ni demokrasia ndiyo inatumika), nchi hiyo ina hatari mpaka litokee kundi jingine litakolokuwa kubwa zaidi na lenye nguvu za kisiasa.
Kwa Tanzania kundi jingine ni vigumu kujiandaa na kuizidi nguvu CCM kwani CCM wataingiza mamluki wao na muda si mrefu mnaanza kuulizana "nani kajamba", "nani kajamaba" bila kupata jibu.

Kumbuka Chama hiki kina uwezo wa kuiagiza mahakama au polisi kitu chochote kile, kwa hiyo hamna pa kwenda. Ni kama vile kuwa kinyume na CCM ni sawa na kuwa dola. Vyombo hivi ndio ambavyo vingetusaidia kujenga uswa na haki na demokrasia ya kweli (kama ipo). Kama hatuwezi kupata hayo yote kwa sababu ya kuwepo fisadi CCM kwa nini tusitatue tatizo letu kubwa kwanza - kufuta CCM halafu tujenge taifa.

TUMECHOKA - TUNAHITAJI MABADILIKO YA KWELI!
 
Ndg Advisor

Punguza HASIRA kwanza duuhh

.....kama nimekuelewa vizuri, unamaana tatizo ni CCM na ubabe wake, na unapendekeza hiki chama kifutwe

Kwa msajili wa vyama kuna vigezo vya kufauta ili chama kifutwe....just do ya H/W......list hivyo vigezo...then compare with CCM actions kama ni kinyume/sawa na hivyo vigezo then we will be able tu judge kuwa kifutwe au kama kuna adhabu yeyote kipewe kutokana na ubabe wake.

...otherwise tuendelee "Kumkoma Nyani giladi"
 
jamani hili suala kila nikikaa linaninyima raha sana tena sana


nikitaafuta speech za kenya huwa napata nyingi ziwe za kenyatta au za kina raila na kibaki na za kampeni na hata za session la bunge lao tena kwa urahisi


ila tatizo kwetu kila nikijaribu kutafuta za tanzania ni chache mno sana kiasi cha kusema hamna si za hayati karume wala nyerere na wala si za hivi karibuni nnashindwa kujua.


tatizo liko wapi nnnaamini kuna speech nyingi ziko mikononi mwa watu ziwe za wazee wetu na hadi za sasa ila sizioni kwenye internet nnashindwa kujua tatizo liko wapi ?


jee tatizo ni protocol au kuwa tuko nyuma ya technolojia au kulikoni?

na nnaomba kutoa wito kwa wana mahiri wa kitanzania ktk elimu hii tusaidianeni kama ni tatizo technolojia kujinyanyua aibu jamani


kwa leo ni hayo tu
 
Jana jioni kulikuwa na foleni moja ya ajabu sana pale kwenye junction ya Africana (Mbezi Beach). Foleni ambayo ilisababisha magari kufungana kila kona, na watu kuamua kutembea kwa miguu maili kibao.

Binafsi, nilikuwa nakwenda kuhudhuria harusi ya binamu. Nikajikuta nimekwama kwenye hiyo foleni kwa masaa 2, mpaka nilipohamua kuahirisha kwenda na kupaki kwenye kijipabu mpaka hiyo karaha ya foleni itoweke.

Tatizo lilikuwa kwenye hiyo junction. Kwamba, magari yanayotoka mjini, yanayotoka Tegeta, na yanayotoka Africana yamefungana kutokana na kila dereva kujifanya mwenye haraka na ujuaji usiokuwa na msingi.

Sasa najiuliza, huu uchache wa barabara unasababishwa na nini hasa? Ukosefu wa fedha za kujenga hizi barabara, ukosefu wa wataalam wa ujenzi, uzembe wa wahusika, au nini hasa?

Je ujenzi wa ile barabara ya nyuma kuanzia kawe mpaka barabara ya Africana ulilenga watumiaji wanaokwenda mbele ya Mbezi Beach? Kwa sababu kilichotokea ni kwamba, magari kadhaa (yanayokwenda mbele ya Mbezi Beach) yamekuwa yanatumia ile barabara ili kutokea kwenye junction ya africana na Bagamoyo road. Matokeo yake pale kwenye junction pamekuwa na vurugu mno. Yaani Barabara ya Africana ghafla imekuwa bize bila ya wahusika kufanya mabadiliko yoyote kwenye ile junction. Na kuongezea matatizo, pale pale kwenye junction kuna kituo cha teksi, vibajaji, daladala, pamoja na vigenge kibao. Kwa hiyo sio tu magari, bali hata watu wamelundikana hapo. Sasa kama huo sio uzembe wa wahusika, tuite nini?

Kwa nini ile barabara ya nyuma (sijui inaitwaje) isingeendelea angalau mpaka ikakutana na barabara ya Kunduchi. Kuongeza ufanisi zaidi, kwa nini isingeendelea mpaka Tegeta, Boko, na mpaka Bunju kama inawezekana? Kwa sababu Tegeta imetanuka mno, na sasa hivi ina wakazi kibao. Kwa hiyo, ingerahisisha sana matatizo ya msongamano kama wakazi wa Tegeta na mbele wangekuwa na angalau na uchaguzi wa barabara ipi kutumia.

Khaa hii nchi inachosha sasa...........grrrrrrrrrr!!!!
 
Ni kweli kabisa viongozi na serikali yetu ni ya kidini ni wafuasi wazuri sana wa dini hii ,dini yao sio UIISLAM wala UKIKRISTU, yenyewe na viongozi wake ni wafuasi wazuri wa dini ya JUJU(vibuyu).

Tanzania haindelei kwa sababu viongozi na wa wananchi walio wengi wanafuata imani hii.
Tangu lini SHETANI anapenda maisha bora yako??
Hawa viongozi wetu ni ma BOX tu lakini maamuzi makubwa na makuu yanafanywa na ma JUJU(mashetani yao eg vibuyu,majini,mapembe,vifaru),Haya MASHETANI ndio matowa uamuzi mazito ya nchi kuna maendeleo hapo??

Hakika nawaambieni maendeleo ya watanzania hayatafika kama hiki kizazi cha SANGOMA kitaendelea kushikilia hatamu.
Hata hao maalbino wanauliwa na haohao viongozi wa juu wa serikali kama isingekuwa hivyo hilo tatizo lisingekuwa janga.
 
Nani atatuambia ukweli kuhusu CCM?

Lula wa Ndali-Mwananzela Aprili 1, 2009
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

JUKUMU la kiongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kukijenga na kukilinda chama ni kubwa. Athari katika chama za kiongozi kutenda maovu, au kutotimiza wajibu, ni kubwa kiasi kwamba maadili yake yakitetereka chama kitavurugika; na nchi itakwenda mrama. – Kanuni za Maadili ya CCM 2002.

Tunaweza kumung’unya maneno tukipenda; tunaweza tukasita kusema tunachokijua ni ukweli; tunaweza kuona aibu kusimama na kutamka tunachokijua; wakati mwingine tunaweza kuhofia watatufikiriaje kina “fulani” kwa sababu ya kusema kitu fulani. Hata hivyo kuna wakati ambao baada ya kupima gharama yote, baada ya kuangalia mambo yote mbadala, ukweli lazima usemwe, na usemwe pasipo utata wowote.

Nilipoandika wiki iliyopita kuhusu “CCM hii si ile ile ya Nyerere” sikujua kuwa siku hiyo hiyo mzee John Malecela, mmoja wa wakongwe wa CCM angeitisha mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia kile ambacho kwa kiasi fulani kilikuwa somo langu wiki ile. Baada ya kumsikiliza na kusikia ujumbe uliomo katika maneno yake, nimefikia hatima moja tu, hatima ambayo sina budi kuiweka hadharani na kuiita kwa jina lake sahihi.

Kwamba, kama chama cha Republican cha Marekani kilivyoonekana kuwa ni adui wa maslahi ya Wamarekani wengi, kiasi cha kusababisha nyota mpya kuibuka ndani ya chama cha Demokrati na hatimaye kuinyang’anya Republican hatamu za uongozi ndivyo hivyo hivyo naamini wakati umefika kwa Watanzania kuukubali ukweli ambao wamekuwa wakiuangalia miaka nenda miaka rudi.

Tanzania haistahili kuwa ilipo sasa. Hakuna sababu yoyote ya kuelezea kwanini tupo hapa tulipo. Miaka michache tu huko nyuma Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete aliulizwa swali ambalo lingeweza kuwa na majibu mengi ya uongo na kweli kuhusu kwanini Tanzania ni maskini. Katika jibu lake ambalo lilionesha ukweli wa utata huu wa umasikini wetu, Rais Kikwete alisema kuwa “hata mimi sijui kwanini Tanzania ni masikini.”
Taifa linapokuwa na Rais ambaye hajui kwanini Tanzania ni masikini basi matatizo yetu yanaonekana ni makubwa zaidi kuliko tunavyodhani.

Ninaamini kabisa kuwa tatizo la Tanzania na umasikini wa Tanzania umetokana, umechangiwa na kuendelezwa na utawala wa CCM.

Kwanza ni kwa sababu ndicho chama pekee ambacho kimeshika madaraka ya nchi tangu Uhuru, hivyo, kimantiki ni kuwa kama kuna maendeleo yoyote ambayo tunayaona, sifa ni lazima ziende kwa CCM. Barabara, hospitali, magari ya kifahari, majengo n.k ambavyo tunaambiwa ni “maendeleo” vinahusiana kwa kiasi kikubwa na utawala wa CCM. Kama “maendeleo” tunayoyaona yanahusishwa na CCM basi hatuwezi kukana ukweli mwingine kuwa umasikini tunaouona pia unahusiana na utawala wa CCM.

Pili, hata hivyo, ni kwa sababu CCM ndiyo chama ambacho kimeunda sera na kuzitekeleza sera hizo katika taifa letu. Hivyo kutofanikiwa kwa sera mbalimbali za CCM ndiko kulikosababisha haya tunayoyaona leo.

Mara nyingi kwenye majukwaa yao wamekuwa wakinadi “sera” zao kwa wananchi na inaonekana kwa kiasi kikubwa wananchi wanazikubali. Tatizo ni kuwa sera hizi nyingi ni sera ambazo utekelezaji wake hauendani na ukweli halisi wa nchi yetu.

Zimebakia kuwa ni sera za kiakili na kisomi lakini zisizoamsha ndani ya wananchi hamu ya kuzitekeleza kwa kiwango cha juu kinachowezekana. Tatizo lake kubwa si katika sera kama sera bali katika watekelezaji na wasimamizi wa sera hizo.

Ndani ya CCM kitaifa hakuna kiongozi mwenye mvuto wa kuamsha taifa kuelekea ukuu na makubwa.

Baadhi ya watu (mimi mmojawapo) tuliamini kabisa kuwa kwa kumchagua Kikwete Tanzania itakuwa imepata ile cheche itakayowasha moto wa mabadiliko ya kitaifa. Leo hii mbele ya macho yake yanafanyika madudu ambayo hata nikianza kuyaandika na kusimulia kizazi kijacho haiwezi kuaminiwa.


Watu kama Malecela wanaitisha waandishi wa habari tukitumaini wana cha “maana” cha kuzungumzia kumbe wanataka kuzungumzia “malumbano” ambayo hata wahusika wake hathubutu kuwataja kwa majina!

Nilitarajia mzee Malecela angesema mawili matatu kuhusu kukerwa kwake na yaliyotokea Benki Kuu, hakusema! Nilitarajia wakati rushwa ya rada ilivyogundulika angekuwa wa kwanza kupaza sauti hakufanya hivyo; nilitarajia mzee wetu angekuwa wa kwanza kukemea na kutaka Meremeta ifunuliwe hajafanya hivyo; wazee wengine wa CCM nao wanazungumza kutoka mbali na hakuna anayetaka kusema ukweli vile ulivyo.


Matatizo ya Tanzania kisiasa na kiuchumi yametokana moja kwa moja na sera na utekelezaji mbovu wa sera za CCM. Hatuwezi kutenganisha tunayoyaona leo kutoka katika utawala wa chama pekee chenye kutawala nchi hii.

Hata yale madogo ambayo wanapenda tuwaimbie sifa ukiyaangalia kwa karibu utaona kuwa kiwango chake cha ubora nacho ni finyu na kidogo. CCM ndiyo matatizo yetu, na hatutaweza kujenga taifa la kisasa lenye mafanikio na nafasi za mafanikio kwa kila mtu bila ya kuindoa CCM madarakani au kuipunguzia nguvu yake na hivyo kuinoa katika utawala.


Hatuwezi kupiga hatua ya maana ya maendeleo na tutaendelea kushangaa Rwanda, Burundi, Uganda, Msumbiji na Zimbabwe zikijiweka sawa kiuchumi na watu wake wakaanza kunufaika huku sisi tunaendelea kuimba “umoja, amani, utulivu na mshikamano” wa walioshiba huku wenye njaa wakiwaangalia.

Hatuwezi kamwe kujenga taifa la kisasa ambalo kilimo chake ni cha kisasa, elimu yake ni ya kisasa kwa kadiri ya kwamba watawala walioko madarakani wanaona vitu kama hivyo ni vya kuja pole pole.

Hatuwezi kupiga hatua ya haraka ya maendeleo makubwa kama ya baadhi ya nchi za Kusini mwa Asia tusipoamua kuwa na viongozi wenye maono ya mbali, utendaji wa karibu na uthubutu usio na mipaka.


Mpaka pale tutakapoamua kukataa CCM na mambo yake yote, ahadi zake na mlolongo wa watawala wake wanaoamini kuwa wao ni zawadi ya Mungu kwa Tanzania, ndipo hapo tutaweza kweli kujipa nafasi ya kufanikiwa.

Kwa maneno mengine, hadi tutakapoamua kwa makusudi kuondoa kizuizi cha mafanikio yetu, basi tutaendelea kurembuliana macho na ufisadi, kucheza twist na wezi na kula mchanyato wa ulaghai miaka nenda rudi huku wenyewe tukiamini kuwa “tunaendelea”.


CCM ndilo tatizo, na tukijua hilo na kulikubalii ndipo tutajikuta dhamira zetu zinatusukuma kuhakikisha kuwa nguvu yake inapunguzwa sana mwaka huu na baadaye 2010.

Na sisi tunaweza!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,

Huwezi kuponya ugonjwa mpaka kwanza ukubali ugonjwa upo. Na huwezi kuponya ugonjwa kwa kushughulikia dalili za ugonjwa peke yake. Kuponya ugonjwa ni kuushughulikia na kuuondoa ugonjwa wenyewe kabisa.

Ili kuundoa ugonjwa huu panahitajika jitihada za makusudi za kuuelimisha ummah, hasa vijijini. Sisi kama JF tutafanya nini katika kipindi hiki tulichonacho mpaka kufikia uchaguzi 2010 ili kufanikisha hili suala la kuundoa ugonjwa huu?
 
Mkuu,

Huwezi kuponya ugonjwa mpaka kwanza ukubali ugonjwa upo. Na huwezi kuponya ugonjwa kwa kushughulikia dalili za ugonjwa peke yake. Kuponya ugonjwa ni kuushughulikia na kuuondoa ugonjwa wenyewe kabisa.

Ili kuundoa ugonjwa huu panahitajika jitihada za makusudi za kuuelimisha ummah, hasa vijijini. Sisi kama JF tutafanya nini katika kipindi hiki tulichonacho mpaka kufikia uchaguzi 2010 ili kufanikisha hili suala la kuundoa ugonjwa huu?

Naamini kuwa hapa JF panaweza kuwa chimbuko la mabadiliko yanayohitajika katika kuleta ufumbuzi wa matatizo ya Taifa letu. Ugonjwa tulionao tunaujua, ni ugonjwa mbaya, unaoweza kurithishwa vizazi vyetu kwa muda mrefu kama hatua za haraka hazitachukuliwa kuuponya.

Ugonjwa huu ni ugonjwa wa aibu japokuwa una dawa. Dawa ninayoiona ni moja tu, nayo ni kushinikiza mabadiliko ya lazima kufanyika katika uongozi wa juu wa nchi kupitia sanduku la kura. Nashauri waandishi wote wa habari wenye mapenzi mema na nchi hii, waanze sasa jitihada za makusudi za kuelimisha umma juu ya nini umma unachotakiwa kufanya (kama ilivyokuwa 2005) ili tupate viongozi mbadala wenye nia, uwezo na ujuzi wa nini kinachohitajika kuikomboa nchi hii kabla haijaanguka kabisa.

Waandishi na wana-media wengine wote watusaidie kufikisha ujumbe unaofaa kwa watu wote ili uchaguzi ujao utusaidie kupata viongozi bora. Viongozi waliopo sasa wameshindwa kutimiza malengo tuliyoamini wangeweza kuyatimiza.

Nchi hii inahitaji juhudi za pamoja kabla haijaangamia.
 
Sina uhakika kama kweli watanzania tunajua umaskini wetu umetokana na CCM.Ebu fikiria namna gani baada ya miaka 40 ya uhuru lakini kuna watanzania hawana uhakika hata wa wakupata shilingi 100 kwa siku.mbaya zaidi tunaambiwa uchumi unakua kwa asilimia takribani 6 au 7.

Mimi najiuliza,ukuaji huu unamhusu nani,kwa kiasi gani,ki vipi,lini na wapi.Maajabu mengine,ni watanzania hawa ambao wanaipa ccm,chama ambacho kimewafanya mwaskina wa kupindukia.naleta kwenu watalaamu tujadli sote.

Naitwa Benjamin mtweve niko udsm nasoma history na political science.
 
Ur lucky that Pundit isn't available!Lol....He could have done some kifimbocheza style in here.
 
Sina uhakika kama kweli watanzania tunajua umaskini wetu umetokana na CCM.Ebu fikiria namna gani baada ya miaka 40 ya uhuru lakini kuna watanzania hawana uhakika hata wa wakupata shilingi 100 kwa siku.mbaya zaidi tunaambiwa uchumi unakua kwa asilimia takribani 6 au 7.

Mimi najiuliza,ukuaji huu unamhusu nani,kwa kiasi gani,ki vipi,lini na wapi.Maajabu mengine,ni watanzania hawa ambao wanaipa ccm,chama ambacho kimewafanya mwaskina wa kupindukia.naleta kwenu watalaamu tujadli sote.

Naitwa Benjamin mtweve niko udsm nasoma history na political science.

Benjamin mtweve,

Wewe unadhani mchawi ni CCM!

Malawi, Kenya, Zambia je leo wameendelea baada ya kuwapiga chini wapinzani miaka 10-20 sasa upinzani ndo upo madarakani?

Umesoma Kitabu cha aliyekuwa Mkuu wa Anti-corruption kenya over.. Now it is our time to eat?

Kwa maoni yangu..mchawi Tz siyo CCM?

Ni sisi wenyewe wananchi!

Je Mwakyembe au Killango je hawa hawako CCM?
 
I will tell you.

Umasikini wetu ni PLANNED POVERTY.
Ruling class imekuwa inasimamia kuhakikisha kwamba majority wanabaki kwenye hali duni ya umasikini ili wao kuweza kuendelea kutawala.
Wametumia THEORY YA ABRAHAM MASLOW ,YA HIERACHY OF NEEDS kufanikisha hilo.

The theory states:Huwezi kuenda kwenye mahitaji ya juu wakati yale ya msingi hayajawa satisfied.

Hivyo tunamka asubuhi mimi na wewe tunahangaikia school fees za watoto,chakula cha familia kwani mshahara hautoshi ,mavazi pale karume sokoni, tena ya mtumba.

Kwa jinsi hiyo huwezi kuanza kufikiria uwezekano wa kugombea udiwani.

So,tatizo letu ni TABAKA TAWALA.So, the so-called sera,vision 2025 na mengineyo yanayofanana na hayo yanatengezwa kwa kufuata theory ya Maslow.

Naelekea Ilala Boma nawahi mitumba ya asubuhi.Baadaye.
 
Jamani,

Great points zimetolewa, na great debate hii. Mimi nina mawazo tofauti.

TUNAKOSA ELIMU. PERIOD!

Tanzania kwa sasa hata CCM ikisimamisha kichaa kugombea urais anapata. WHY?. Sehemu zilizokuwa na shule toka zamani kama Kagera na Kilimanjaro, ndio tumeona wanapata angalau ubunge wapinzani. WHY?.

Elimu ni pana. Basic elimu ya secondary ni muhimu kwa kila Mtanzania, Lakini waelimishwe pia kuhusu Self awareness, Uraia, uzalendo etc.
Kungekuwa na somo shuleni (lipo uraia kwa sasa) linaloonyesha mabaya ya kutolipa kodi, mabaya ya kuchukua rushwa etc.

Wananchi waliopo sasa (asilimia 80% kwa mtazamo wangu) hawawezi kupembua lipi ni lipi. Ili tuendelee tunahitaji wananchi wenye mtazamo na uzalendo. Huwezi kuwa na mtazamo au uzalendo kama huna elimu angalau ya kati.

Leo unaenda kwa babu ambaye hata darasa la kwanza hakwenda, kisha unaanza kumuelezea sera ya majimbo, ataelewa nini?, au unamweleza kukua kwa uchumi, per capita income imekuwa blah blah!! what?!?, anachohitaji kumuambia utaijengea kijiji chake hospitali, shule, kuleta maji. Basi hapo umepata kura!!!, wanasiasa ni waongo, hivyo easily anadanganya anapata kura.

Kwahiyo hawa wananchi tukiwaelimisha basi ujue CCM tuna kazi ya ziada. Kwa maana wataweza kufanya Logical reasoning etc.

Bandugu nimeongelea Elimu katika narrow mind sasa naomba uelezee hiyo hiyo elimu kwa kusomesha nje vijana kwa ajili ya utaalaamu.
Elimu ya kusomesha nje itakuza uchumi haraka, elimu ya kati itasaidia wananchi kuamka na kuchagua viongozi bora.

Mi nalia na ELIMU.

FD
Haki ELimu wamefanya kazi nzuri sana,serikali imewaingilia kwa vitisho na vyombo vya habari,lakini walikuwa wanawaelimisha wananchi kujua haki zao za msingi na pia kuwafanya watendaji serikalini tuliwapa dhamana kuiendesha nchi yetu kuwajibika.
cha msingi sio Elimu ya darasani tu,bali ni kuwa na NGO nyingi za mfano wa Haki elimu ili kuelimisha nchi,kwa sasa tuna NGO nyingi za Ukimwi ,watoto yatima etc zote ziko kiulaji lakini tukiwa na asasi za kuelimisha jamii juu ya siasa bora na uongozi bora, nchi yetu ingekuwa mbali sana.
 
Back
Top Bottom