Tanzania ni Mali ya nani?

kwa kuwa umesema Tanzania ni mali...........Basi ni mali ya kuokota ambayo aliyeipoteza bado hajajua kuwa ameipoteza......ngoja siku akitambua......
 
Nchi ni nchi, na mali ni mali. Kusema nchi ni mali huo ni ujinga tena wa wazi wazi. Kama nchi ni mali haya itumie basi Tanzania. Mie nakupa Tanzania yote yako chukuwa wewe, pata wewe, haya umeshakuwa na mali. Hata wewe binafsi yako sio mali, haya jiuze basi kama wewe mali.


Huna hoja, una viroja.

hawa ni wale wanaoambiwa kuwa Dhahabu iliyopo kahama,almasi iliyopo Mwadui,kahawa iliyopo kagera, korosho zilizopo mtwara, mbuga za wanyama zote na pesa zilizopo hazina/ BOT ni mali yetu wanaitikia kuwa ni kweli zao......Chako ni kile ulichonacho na unauwezo wa kukitolea maamuzi....


MY WORD IS MY BOND...
 
tumuulize mkulu wa kaya hili swala anaweza kutupa ufafanuzi...may be anaweza...
 
Wakuu,
Tunapoendelea kujiweka sawa kwa ajili ya mambo ya kitaifa yaliyoko mbele yetu, hususan mchakato wa kuandikwa kwa katika mpya, naomba kuuliza swali. Nahisi pamoja na mambo mengine, katiba mpya itatakiwa kuwa na ibara inayolitaja taifa letu Tanzania. Katika kufikiria hayo nimepata swali ambalo pengine laweza kuonekana jepesi lakini kumbe gumu. Hivi; Tanzania ni mali ya nani? Naomba mtazamo wenu kisha tujadiliane
Ni mali yetu sote mkuu ila ndo hivyo, sijui dunia inataka kufikia kiama?
 
hawa ni wale wanaoambiwa kuwa Dhahabu iliyopo kahama,almasi iliyopo Mwadui,kahawa iliyopo kagera, korosho zilizopo mtwara, mbuga za wanyama zote na pesa zilizopo hazina/ BOT ni mali yetu wanaitikia kuwa ni kweli zao......Chako ni kile ulichonacho na unauwezo wa kukitolea maamuzi....


MY WORD IS MY BOND...

Hao au nyie mnaouliza Tanzania mali ya nani?

Mali huwezi kuipata kw kukaa na kuuliza eti nchi na mali ya nani? huo ni upunguani wa hali ya juu. Wewe unaeojioan kuwa una mali, mbona huna? ungekuwa na mali ungejuwa mali ni nini na usingefikiria kuwa nchi ni mali.

Huo ujanja umeupata lini hata leo ujidai Tanzania ni mali ya nani? nani alikuambia Tanzania mali? Mali iko huko magharabi.

Nyie ni mapunguani msiojuwa mali ni nini. Hiyo tanzania kaa uitazame jina tu. Kama unataka kujua Tanzania mali ya nani basi ni ya Muhindi wa Tanga aliyoipa jina Tanzania. Haya unalo?

Dr.Jakaya Mrisho Kikwete = Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Mohamed Gharib Bilal = Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Ali Mohamed Shein = Rais Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar.

Hao wote ni Raia wa Tanzania. Wewe na mimi ni Raia wa Tanzania.

Mali iko wapi hapo? usituletee akili za mbege saa hizi.
 

Mkuu Somji Juma, heshima yako.
Nakubaliana na jibu lako, nchi yetu ni mali ya Mungu. Hata maandiko matakatifu yanasema hivyo. Kwa Mfano; Zaburi 24:1 inasema, nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana.
Sasa kwa kuwa ni mali ya Mungu, sisi tuitwao watanzania si wenye mali bali ni mawakili tu. Katika Uwakili wetu huo, tunapaswa kuitunza Tanzania ili iwe na uendelevu kwa maslahi ya kizazi kilichopo sasa na vizazi vitakavyokuja baada yetu. Tunao wajibu wa kuyatunza kwa uangalifu mkubwa mazingira ya Tanzania. Tunayo haki ya kutumia maliasili zilizopo nchini, lakini katika namna ambayo si ya ufujaji, bali tukijua kwamba kuna kesho na kuna mwenye mali hii.
Aidha, wenye uwakili juu ya Tanzania ni watanzania kwa kuzaliwa kwao au kwa kupewa uraia kisheria. Hivyo wageni hawana mamlaka juu ya utajiri wa nchi hii. Wao walipewa uwakili katika nchi zao.
Katika uwakili wetu huo, tunao wajibu pia wa kuwadhibiti wanaofanya ufisadi juu ya nchi hii na waovu wote waliotajwa na wachangiaji katika uzi huu.
 
Tanzania ni mali ya Watanzania wote.
Swali: je, Mtanzania ni nani?
Jibu: Mtanzania ni yule mwenye maisha bora hadi sasa. Hii ni kwa sababu kila aliye Mtanzania ali ahidiwa maisha bora. Kwa maana hiyo kama huna maisha bora hadi leo hii basi wewe sio Mtanzania na Tanzania utaiona ngumu. Tanzania in wenyewe...na wenyewe ndio Watanzania.
 
Tanzania ni mali ya Watanzania wote.
Swali: je, Mtanzania ni nani?
Jibu: Mtanzania ni yule mwenye maisha bora hadi sasa. Hii ni kwa sababu kila aliye Mtanzania ali ahidiwa maisha bora. Kwa maana hiyo kama huna maisha bora hadi leo hii basi wewe sio Mtanzania na Tanzania utaiona ngumu. Tanzania in wenyewe...na wenyewe ndio Watanzania.

Maisha bora kuyangoja JF? Sahau. Hapa tuwachieni sisi semi retired, vijana mkachakarike at least 14 hours every day. Hii ni kwa vijana wote wa miaka 18 mpaka 50. Nakuhakikishia ukijituma inavyotakiwa hutolalamika maisha magumu.

Nimetembea sana duniani, ni nchi chache sana zenye fursa za kujiwezesha haraka haraka kama tulizonazo Tanzania kwa sasa. Amini usiamini huo ndio ukweli. Lakini ikiwa kutwa kucha unajificha kwenye mtandao hutoziona maisha yako.
 
Maisha bora kuyangoja JF? Sahau. Hapa tuwachieni sisi semi retired, vijana mkachakarike at least 14 hours every day. Hii ni kwa vijana wote wa miaka 18 mpaka 50. Nakuhakikishia ukijituma inavyotakiwa hutolalamika maisha magumu.
Nimetembea sana duniani, ni nchi chache sana zenye fursa za kujiwezesha haraka haraka kama tulizonazo Tanzania kwa sasa. Amini usiamini huo ndio ukweli. Lakini ikiwa kutwa kucha unajificha kwenye mtandao hutoziona maisha yako.


Ndugu majibu yako ni mazuri,

Lakini kama unajituma kisha maisha yenyewe ni magumu, mfumuko wa bei unaumiza kila siku ni heri ya jana. Lakini kuna wengine wanatumia madaraka yao kujinufaisha ndio hao wanasababisha maisha yawe magumu. Sidhani kama kuna mtu anayeishi pasipo kufanya kazi.

ALIYESHIBA HAMJUI MWENYE NJAA

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Mkurugenzi wa Sekta Binafsi Tanzania, Bw. Louis Accaro alipata kusema hivi;
"We've also changed the land laws. In the past, land in Tanzania could not be bought because it was the property of the state. But now, investors can have title to the land; the land is leased to them for a certain number of years, usually for 99 years, and can be sold freely"
 
Maisha bora kuyangoja JF? Sahau. Hapa tuwachieni sisi semi retired, vijana mkachakarike at least 14 hours every day. Hii ni kwa vijana wote wa miaka 18 mpaka 50. Nakuhakikishia ukijituma inavyotakiwa hutolalamika maisha magumu.

Nimetembea sana duniani, ni nchi chache sana zenye fursa za kujiwezesha haraka haraka kama tulizonazo Tanzania kwa sasa. Amini usiamini huo ndio ukweli. Lakini ikiwa kutwa kucha unajificha kwenye mtandao hutoziona maisha yako.
JF ni sehemu ya kuchakarika. Huwa sipati msukumo wa kuchakarika ninapokuwa mpofu wa habari/taarifa. Taarifa kwangu ni chachu ya kunichakarisha...nikitoka JF huwa naingia kitaa kama mbogo mjeruhiwa. Lakini sijasema kama mimi ni Mtanzania au la! pengine ninge enea katika ujumbe wako moja kwa moja.
 
Duuh!!!!!!!!!!

Inauma sana kwa watz kukosa utaifa namna hii, hii ndo sababu kubwa kwa Tz kukosa mwenyewe. Lakini tutafika tu, watatafutana wenyewe mwishowe wataiacha Tz kwa watanzania, Tanzania is greater than Tanzanians!!!!
 
Hao au nyie mnaouliza Tanzania mali ya nani?


Mali huwezi kuipata kw kukaa na kuuliza eti nchi na mali ya nani? huo ni upunguani wa hali ya juu. Wewe unaeojioan kuwa una mali, mbona huna? ungekuwa na mali ungejuwa mali ni nini na usingefikiria kuwa nchi ni mali.

Huo ujanja umeupata lini hata leo ujidai Tanzania ni mali ya nani? nani alikuambia Tanzania mali? Mali iko huko magharabi.

Nyie ni mapunguani msiojuwa mali ni nini. Hiyo tanzania kaa uitazame jina tu. Kama unataka kujua Tanzania mali ya nani basi ni ya Muhindi wa Tanga aliyoipa jina Tanzania. Haya unalo?

Dr.Jakaya Mrisho Kikwete = Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Mohamed Gharib Bilal = Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Ali Mohamed Shein = Rais Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar.

Hao wote ni Raia wa Tanzania. Wewe na mimi ni Raia wa Tanzania.

Mali iko wapi hapo? usituletee akili za mbege saa hizi.


wewe Zomba hivi huwa unasoma kweli kwa umakini uzi utolewao kujua ni uzi upi unakusapoti au kukupinga......hata hivyo mawazo yako siyo hasi.....punguza jaziba ...toka ndani ya Duara uone kilichopo ndani ya hilo Duara...


MY WORD IS MY BOND......
 
Back
Top Bottom