Tanzania: Nchi ya kujenga na kubomoa!

Mghoshingwa

JF-Expert Member
Jul 9, 2011
305
73
Wama jf poleni kwa kazi za ujenzi wa taifa letu, taifa tunalo lijenga kwa nguvu huku wengine wanabomoa.
Wana jf nimekuja kwa mara ya kwanza kabisa ili tushirikiane pamoja na kubadilishana mawazo kuhusu mwenendo wa Taifa letu ambalo misingi yake mingi ya uadilifu imebomolewa kwa sababu ya rushwa, kukosekana kwa uwajibikaji, uadilifu pamoja na kukosekana kwa utekelezaji sahihi wa sera za maendeleo na mipango miji.
Kimsingi yapo mambo mengi hayaendi sawa katika Taifa letu, ila ninachotaka tubadilishane mawazo ni suala la MIUNDO MBINU hasa mfumo wa mawasiliano ya barabara na maji.
Wana Jf wenzangu naomba mnisaidie kujua jambo hili:
Je hivi mpango wa upanuz wa bara bara zetu ni wa ghafla ama ni mikakati ya makusudi? Nauliza hivi kwakuwa mara nyingi nashuhudia uharibifu wa miundo mbinu mingine pale muundo mbinu mwingine unapo anzishwa, kuboreshwa, ama n.k. Kwa mfano sasa hivi kuna ujenzi wa bara bara ya mwenge tegeta, ukipita bara bara hiyo utakuta mabomba yamekatwa na tractor zinazo tengeneza bara bara na maji yanamwagika hovyo., wakati mwaka jana mabomba hayo yalitandazwa kwa gharama kubwa tu, na wakauita mradi wa wachina.
Pia wakati mwingine utawakuta watu wanabomoa bara bara ya lami(wanachimba) ili kupitisha mabomba.
Je tuna chatisha mambo ama tatizo hasa ni nini?
 
ukifuatilia matukio ya mwaka huu mzima utafiri ni hadith ya nchi ya kusadikika maana mpaka mpangaji wa magogoni kuvikwa suti na mwekezaji
 
Back
Top Bottom