Tanzania Nayo Kujenga 'China Town' ! - "A Blessing in Disguyise?!".

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,453
113,461
Wanabodi,

Hii nimeitoa kwa Mwandishi wa Waziri Mkuu.

Kwa: Whariri Wote;


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SERIKALI inakamilisha uanzishaji wa Kituo Maalum (China – Tanzania Logistic Centre) kwa ajili ya kuzipatia nchi za Afrika Mashariki na Kati bidhaa zenye ubora wa kiwango cha juu kutoka China badala ya wafanyabiashara wa nchi hizo kuzifuata huko.
Hayo yalitangazwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Cyril Chami wakati akimkaribisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuzindua Bodi mpya ya Mamlaka ya Maeneo Huru ya Uwekezaji (EPZA) jijini Dar es Salaam Jumanne iliyopita.
“Ili kuepukana na hatari ya kuupoteza mradi huu muhimu ambao tayari unanyemelewa na baadhi ya nchi hapa Afrika tunajitahidi kupata fedha hizi kutoka Bajeti ya serikali au kupata mkopo kutoka TIB (Tanzania Invstment Bank,” Dkt. Chami alisema.
Fedha zinazohitajika ni Sh. Bilioni 60 kulipia fidia ya kuwaondoa watu waliojenga kwenye makazi yasiyo rasmi eneo la ekari 60 Kurasini jijini Dar es Salaam, ambalo wawekezaji hao wanalipendelea badala ya eneo la Uwekezaji la Bagamoyo.
Mradi huo utakuwa wa awamu mbili – ya kwanza ni ujenzi wa kituo hicho na ya pili ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao, maeneo ya biashara, masoko ya kuhifadhi bidhaa mbalimbali, majumba ya maonyesho na mikutano na maofisi, huko Bagamoyo.
Dkt. Chami alisema makubaliano yaliyofikiwa na Serikali ya China ni kujenga kituo hicho kwa mfumo wa ubia ambapo Serikali ya China itatoa fedha zote za ujenzi wa miundombinu na mtaji wa kuanzia na Serikali ya Tanzania itatoa eneo la ujenzi.
Serikali ya China itawakilishwa na Ushirika wa Yiwu Pan-Africa International Investment Corporation na Serikali ya Tanzania itawakilishwa na Mamlaka ya EPZA.
Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, inaielekeza Wizaraya Viwanda na Biashara kuhamasisha uanzishwaji wa EPZ na Maeneo Maalum ya Uwekezaji (SEZ).
Katika miaka mitano iliyopita Bodi ya EPZA ilisajili Makampuni 63 yanayozalisha chini ya mfumo wa EPZ na kutengeneza ajira 14,000 za moja na 60,000 zisizo za moja kwa moja na Dola za Marekani Milioni 712 zimewekezwa na nyingine Milioni 390 zimeingizwa kutokana na mauzo ya bidhaa nje. (mwisho)Imetolewa na: Ofisi ya Waziri Mkuu, S.L.P. 3021, DAR ES SALAAMJumapili Machi 10, 2012

My Take:
Jee mradi huu ni ukombozi wa kweli kwa wafanya biashara wanaofuata bidhaa mbalimbali nchini China, hivyo kuzipatia humu humu nchini kwa urahisi, na kuliteka soko la Afrika Mashariki kwa mazagazaga yote?!.Jee ujio huu sio tuu utaleta zile cheap products na mazagazaga yote kutoka China kwa kuihamishia Ghwanzou hapo Kurasini, ambayo ni maarufu duniani kwa kufyatua fake na couterfate products?!. Japo at initio stage unaonyeshwa ni mradi wa ubia kati ya Tanzania na China, ukweli ni kuwa sisi baada ya kuwapa eneo, 100% investment ni ya Mchina japo kila kitakacho tengenezwa kitakuwa made in Tanzania with Chinese brand names kwenye kila kitu kitakachoundwa hapo! What will become with ile ndoto yetu ya Tanzania kufufua viwanda vyetu ili tutawale soko la Afrika Mashariki?. Jee ujio huu unaweza kuwa ndio kiashiria cha mwisho wa utawala wa Wahindi kwenye biashara zote?. Jee vile viwanda vyetu vidogo vigo na ulupuaji wetu, tutaweza kustahili ushindani na Mchina?. Tumemkaribisha wenyewe Mchina ili kutuletea neema, jee hii itakuwa ni neema ya kweli, au ni "A Blessing In Disguise?!.

Welcome to "New China Town Kurasini!,

Pasco.
 
Waje tu, itakuwa poa. I enjoyed China Town in Kuala Lumpur, Malaysia, everything was very cheap!
 
Kama ni mradi wa ukubwa unaodhania bwana Pasco usingekaa katika eneo dogo kabisa la hekari 60, hapa tunataka kugeuzwa kichaka cha kuuzia bidhaa feki za China kwenda nchi za kiafrika. Kwa kuwa akili ya CCM sio ya kujitegemea wanachokifanya sasa ni kupata manufactured products badala ya kujipanga kufanya manufacturing. Kwa mfano Pamba inayozalishwa Tanzania ingeweza kutengeneza nguo hapa hapa lakini inaenda China wanaongeza thamani na kurudisha nguo kwa bei kubwa. Huyo Chami alitakiwa kuongelea kujenga viwanda vyetu na sio kuwa madalali wa bidhaa za kichina
 
Hii issue si ilikuja pale kamata kamata za Wachina wa Kariakoo ilipotokea ndipo ubalozi wao na serikali wakaelewana ijengwe center yao ya mauzo ambapo itakuwa duty free zone. Wafanya biashara wakinunuwa mali watalipia ushuru na kuchukuwa mizigo yao. Center hiyo pia itawauzia wateja wa nchi za jirani zote maana watapata kwa bei nafuu.
 
Pasco, China is seeking global dominance and with that markets to dump their products. All this money being pumped to country like ours in the name of development is mere rhetoric, fake and cosmetic pretence so to exploite us. Let us be not deceived, no country can spend money on foreign territory without any perceived future return .
The mainstream of our country economy is agriculture - thats where majority of our folks make out their living. If we are not careful this sector will further be exploited with entry of China in global competency. As someone observed in this forum, the solution to our poverty is not aid or handouts ,but access to markets like china ,US etc, where we can markets our goods .
 
bado ni ngumu kumzuia machinga kwenda china kuleta mzigo wake autakae yeye
 
Ni jambo zuri wajenge tu,Dubai wanayo pia,hawa jamaa wamepiga hatua kubwa sana kwa sasa,wanatoa vitu original na vyenye ubora sana,na pia wanatoa vitu feki na copy,muhimu kwa serikali kuchukua hatua na shirika la viwango kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nizile za kiwango cha dunia,nchi za mashariki ya kati karibu zote zinatumia sana bidhaa za china,na bidhaa original kabisa,nina Nokia n900 nilinunua 1 ya nchi ya Gulf ni made in china,nilipewa waranty ya mwaka 1 mpaka sasa natumia ni mwezi wa 10,haijawahi kunisumbua,muhimu serikali kuhakiki bidhaa,kila la kheri china town
 
Tumeshindwa kuviendesha tu viwanda alivyotujengea Mwalimu ndo sembuse tujenge vipya sasa hivi? viongozi wetu wanafikiria kwa kutumia masaburi akili zao ni juu ya kuwa tegemezi na omba omba tu waache wachina walio serious na maendeleo waje kuuza bidhaa zao hapa tumeshindwa kabisa kujiendesha na siku akitokea mwekezaji tukambinafsishia serikali ntafurahi sana.Shida yangu ni kuwa wachina wakiwa mahali wanakaba hadi penati yaani hadi kazi ya kufagia wanafanya wenyewe hawataki masihara
 
wanabodi,

hii nimeitoa kwa mwandishi wa waziri mkuu.

Kwa: Whariri wote;


taarifa kwa vyombo vya habari

serikali inakamilisha uanzishaji wa kituo maalum (china – tanzania logistic centre) kwa ajili ya kuzipatia nchi za afrika mashariki na kati bidhaa zenye ubora wa kiwango cha juu kutoka china badala ya wafanyabiashara wa nchi hizo kuzifuata huko.
Hayo yalitangazwa na waziri wa viwanda na biashara, dkt. Cyril chami wakati akimkaribisha waziri mkuu mizengo pinda kuzindua bodi mpya ya mamlaka ya maeneo huru ya uwekezaji (epza) jijini dar es salaam jumanne iliyopita.
"ili kuepukana na hatari ya kuupoteza mradi huu muhimu ambao tayari unanyemelewa na baadhi ya nchi hapa afrika tunajitahidi kupata fedha hizi kutoka bajeti ya serikali au kupata mkopo kutoka tib (tanzania invstment bank," dkt. Chami alisema.
Fedha zinazohitajika ni sh. Bilioni 60 kulipia fidia ya kuwaondoa watu waliojenga kwenye makazi yasiyo rasmi eneo la ekari 60 kurasini jijini dar es salaam, ambalo wawekezaji hao wanalipendelea badala ya eneo la uwekezaji la bagamoyo.
Mradi huo utakuwa wa awamu mbili – ya kwanza ni ujenzi wa kituo hicho na ya pili ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao, maeneo ya biashara, masoko ya kuhifadhi bidhaa mbalimbali, majumba ya maonyesho na mikutano na maofisi, huko bagamoyo.
Dkt. Chami alisema makubaliano yaliyofikiwa na serikali ya china ni kujenga kituo hicho kwa mfumo wa ubia ambapo serikali ya china itatoa fedha zote za ujenzi wa miundombinu na mtaji wa kuanzia na serikali ya tanzania itatoa eneo la ujenzi.
Serikali ya china itawakilishwa na ushirika wa yiwu pan-africa international investment corporation na serikali ya tanzania itawakilishwa na mamlaka ya epza.
Ilani ya uchaguzi ya ccm ya mwaka 2010, inaielekeza wizaraya viwanda na biashara kuhamasisha uanzishwaji wa epz na maeneo maalum ya uwekezaji (sez).
Katika miaka mitano iliyopita bodi ya epza ilisajili makampuni 63 yanayozalisha chini ya mfumo wa epz na kutengeneza ajira 14,000 za moja na 60,000 zisizo za moja kwa moja na dola za marekani milioni 712 zimewekezwa na nyingine milioni 390 zimeingizwa kutokana na mauzo ya bidhaa nje. (mwisho)imetolewa na: ofisi ya waziri mkuu, s.l.p. 3021, dar es salaamjumapili machi 10, 2012

my take:
Jee mradi huu ni ukombozi wa kweli kwa wafanya biashara wanaofuata bidhaa mbalimbali nchini china, hivyo kuzipatia humu humu nchini kwa urahisi, na kuliteka soko la afrika mashariki kwa mazagazaga yote?!.jee ujio huu sio tuu utaleta zile cheap products na mazagazaga yote kutoka china kwa kuihamishia ghwanzou hapo kurasini, ambayo ni maarufu duniani kwa kufyatua fake na couterfate products?!. Japo at initio stage unaonyeshwa ni mradi wa ubia kati ya tanzania na china, ukweli ni kuwa sisi baada ya kuwapa eneo, 100% investment ni ya mchina japo kila kitakacho tengenezwa kitakuwa made in tanzania with chinese brand names kwenye kila kitu kitakachoundwa hapo! What will become with ile ndoto yetu ya tanzania kufufua viwanda vyetu ili tutawale soko la afrika mashariki?. Jee ujio huu unaweza kuwa ndio kiashiria cha mwisho wa utawala wa wahindi kwenye biashara zote?. Jee vile viwanda vyetu vidogo vigo na ulupuaji wetu, tutaweza kustahili ushindani na mchina?. Tumemkaribisha wenyewe mchina ili kutuletea neema, jee hii itakuwa ni neema ya kweli, au ni "a blessing in disguise?!.

Welcome to "new china town kurasini!,

pasco.
mkuu pasco, i agree with your obesrvation, hii ni ile hadithi ya mwarabu na ngamia kwenye hema.
 
China towns zipo nchi nyingi sana asia, euro na america, sifa yake kubwa ni kuendesha uzalishaji wa bidhaa feki, uuzaji wa madawa ya kulevya, ukahaba. Huko utakuta iphone fake, beer fake, saa fake, nguo fake, viatu, perfume fake ect mpaka fedha fake wanatengeneza kwa siri. Nilichokiona kwa wenzetu ni kwamba wanavimonitor sana vijiji hivi sasa kwa hapa kwetu na rushwa ndio tumeumia.

upande wa uchumi: hapa ndio tumeua soko la bidhaa za ndani na viwanda vidogo vidogo na pia hawa jamaa ni mabingwa wa kukwepa kodi. Wizara isitudanganye kuhusu china town, nenda popote duniani china town ni eneo maalum na lipo kisheria kwa uuzaji wa fake products na huwa hakuna wafanyabiashara wakubwa hata siku moja wote ni wadogo wadogo na hii ndio nature ya china town.
 
kuna tetesi nilizipata kwa jamaa mmoja wa west anasema lengo la kuweka vijiji hivi kila nchi ni kuwa na secret military base ya china kama ilivyo kwa amerika
 
Tumeshindwa kuviendesha tu viwanda alivyotujengea Mwalimu ndo sembuse tujenge vipya sasa hivi? viongozi wetu wanafikiria kwa kutumia masaburi akili zao ni juu ya kuwa tegemezi na omba omba tu waache wachina walio serious na maendeleo waje kuuza bidhaa zao hapa tumeshindwa kabisa kujiendesha na siku akitokea mwekezaji tukambinafsishia serikali ntafurahi sana.Shida yangu ni kuwa wachina wakiwa mahali wanakaba hadi penati yaani hadi kazi ya kufagia wanafanya wenyewe hawataki masihara

Kweli kabisa, si alivyojenga tu hata alivyotaifisha tulishindwa kuviendesha.
 
Nakumbuka banda la mchina pale kidongo-chekundu 60s. Ni nani analikumbuka hilo?
 
Wenzetu wanawakaribisha waChina wakiwa na jicho la ziada,sisi na ulimbukeni wetu tunawabeba kama walivyo na kuwaachia wafanye watakalo.Na hili la China town ndio linahitimisha kifo cha tuviwanda tuchache tulivyobahatika ku-survive.
 
Wenzetu wanawakaribisha waChina wakiwa na jicho la ziada,sisi na ulimbukeni wetu tunawabeba kama walivyo na kuwaachia wafanye watakalo.Na hili la China town ndio linahitimisha kifo cha tuviwanda tuchache tulivyobahatika ku-survive.

Hiyo ndio njia pekee ya kuzidisha kiwango, kama unaweza kushindana nao utaweza tu, kama huwezi bora ununue kwao tu. "If you can't beat them, join them"!
 
Hii itakuwa International Machinga Complex(IMC) ambayao itafeli kama ile ya locals kwa sababu ya kutumika kisiasa

AMM.JPG
 
In nutshell, miradi ya namna hii ni ya kibwege na haina tofauti yoyote na ile ya mababu zetu akina Sultan Mangungu wa Msovero Sultanate. Ubwege wa viongozi wetu ni wa kurithi. Haiwezekani wewe badala ya kuangalia jinsi ya kutanua exports zako na masoko ya bidhaa zako, ukashirikiana na adui wako wa kibiashara kumsaidia kuuza bidhaa zake..#toostupid
 
Back
Top Bottom