TANZANIA Mpya inakuja

AMANIPARTY

Member
Jun 2, 2011
15
7
WATANZANIA tunao mtaji ambao ni hazina Ndani ya nchi yetu katika mambo makuu matatu:

1. Lugha: Watanzania Tuna Hazina ya Lugha ya Kishwahili ambayo sio chimbuko la kabila mojawapo ndani ya Nchi yetu. Mateso Tuliyoyapata kwenye Biashara kandamivu ya Utumwa, Mchanganyiko wa zaidi ya lugha za makabila 360 ndani ya nchi yetu, pamoja na jitiada binafsi za waasisi wa Taifa Letu akiwemo Marehemu Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, zimeleta matunda ya kuwa na Lugha hii. Majirani zetu Kenya na Uganda hawana bahati hii.. Mataifa mfano Japan, China, Korea wote hawana bahati hii, wao wanatumia Lugha ya kabila Moja tu ambalo ndilo lilikuwa asisi la ufalme wa nchi zao na likapewa hadhi ya kuwa Lugha ya mataifa yao na kupoteza kabisa Lugha nyingine na kuziondoa kwenye tasnia ya mawasiliano kiasi kwamba baada ya miongo kadhaa lugha hizo za makabila mengine zikapotea Duniani. Marekani haina bahati hii, wanatumia Lugha ya Kabila la Malkia wa uingereza ambayo wameibadilisha kidogo tu matamshi yake. CHAMA CHA AMANI(CCA) kinamini Kishwahili Chetu kikiheshimiwa na kupewa stahiki yake kama Lugha ya Taifa HURU, kinaweza kutumika kama Lugha si ya mawasiliano tu bali pia Lugha ya biashara, michezo/fani na Elimu.

2. Akili na Uelewa: Watanzania wana Akili na Uelewa wa hali ya juu sana nadhani kuliko Taifa lolote Ulimwenguni. Akili na Upeo wa uelewa huu bado umelazwa. Watanzania bado hawajapata mtu wa kuwaamsha na kuwaambia waanze kutumia akili na uelewa walionao. CHAMA CHA AMANI(CCA)tunamini kwamba akili za watanzania zikiamshwa na kuamrishwa kuanza kufikiri tunaweza kuwa na Taifa lililoendelea kwenye Uvumbuzi na teknolojia ya hali ya Juu sana ulimwenguni na hivyo Watanzania tukawa sio soko la kujaribia teknolojia na bidha za wenzetu. Watanzania wenyewe tutabuni na kutengeneza Viwanda vitavyozalisha bidhaa zinazotufaa kwa matumizi yetu kwanza kabla ya kupeleka mgao kwa majrani zetu. Nchi haiwezi kuwepo ikiwa inatumia bidhaa, technolojia na elimu ya nchi nyingine.

3.Uhuru: Tunaamini kwamba Binadamu wote ni zao la Imani. Mpaka sasa hakuna sayansi wala nchi wala serikali yoyote iliyofanikiwa kufafanua asili ya mwanadamu. Hivyo wote bado tunaamini mwanadamu ni Zao la Imani. kama ni Hivyo basi hakuna mwanadamu mwenye amri kubwa zaidi juu ya mwenzake. Hakuna Taifa lenye mipaka yake na serikali yake linaloweza kuingilia matakwa na kutunisha misuli yake kwenye taifa Jingine. CHAMA CHA AMANI (CCA) Tunamini Hilo, Kwa Hivyo Tuna kila sababu ya kuidai Tanzania HURU. Mataifa yanayojiita yenyewe makubwa.. basi kwa Ukubwa wao uwe pia ukubwa wa uelewa wao, watuelewa Hivyo na kuheshimu Uhuru wa Taifa Hili kama majarida ya Umoja wao yanavyofafanua. Hatutaki Ukloni mamboleo, hatutaki kpangia nini na lini tufanye nini, Tunapohitaji kuchagua viongozi wetu tuacheni tutumie rasilimali na uwezo tulionao sio kupewa msaada na pesa kwenye kila kitu. Tunahitaji kumiliki migodi na rasilimali zote za inchi yetu, ni zetu, tuachieni tufanye kile tunachodhani ni sahihi ndani ya mipaka yetu, hatuhitaji mtufundishie Jeshi letu nani wa kumpiga na wapi pa kumpiga, Tuacheni tujijue wenyewe, kwani Nie nani aliwafundisha? kiasi kwamba mjipe kuwa walimu wa wengine. Hatuhitaji silaha zenu, tunahitaji Kutengeneza na kutumia za kwetu kwa mbinu za kwetu pia. Toka lini mtu akamuuzia adui yake silaha yenye uwezo wa kumpiga yeye mwenyewe? haiwezekani.. Daima mnatuuzia silaha hafifu zinazotugombanisha na kuuana sisi kwa sisi. INATOSHA. Sisi ndio tunapaswa kutoa misaada sio kupewa misaada. Tanzania Mpya Inakuja.. Mimi wewe na sisi Tutaiwezesha. AMANI DAIMA!

Asanteni
 
Hiyo no.2 mkuu naitilia shaka make kama kweli ndivyo basi haya matatzo tunayoyapigia kelele kila siku yangeishaisha ...sasa tusaidie kama akili tunayo tatzo letu ni nini?

Yawezekana tuna akili ila uelewa wetu ni mdogo ama sivyo kinyume chake.
 
Nachelea kuchangia, kwa sababu sijaona jambo jipya katika hii mistari takriban 27 iliyowekwa katika hii thread.
 
WATANZANIA tunao mtaji ambao ni hazina Ndani ya nchi yetu katika mambo makuu matatu:

1. Lugha: Watanzania Tuna Hazina ya Lugha ya Kishwahili ambayo sio chimbuko la kabila mojawapo ndani ya Nchi yetu. Mateso Tuliyoyapata kwenye Biashara kandamivu ya Utumwa, Mchanganyiko wa zaidi ya lugha za makabila 360 ndani ya nchi yetu, pamoja na jitiada binafsi za waasisi wa Taifa Letu akiwemo Marehemu Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, zimeleta matunda ya kuwa na Lugha hii. Majirani zetu Kenya na Uganda hawana bahati hii.. Mataifa mfano Japan, China, Korea wote hawana bahati hii, wao wanatumia Lugha ya kabila Moja tu ambalo ndilo lilikuwa asisi la ufalme wa nchi zao na likapewa hadhi ya kuwa Lugha ya mataifa yao na kupoteza kabisa Lugha nyingine na kuziondoa kwenye tasnia ya mawasiliano kiasi kwamba baada ya miongo kadhaa lugha hizo za makabila mengine zikapotea Duniani. Marekani haina bahati hii, wanatumia Lugha ya Kabila la Malkia wa uingereza ambayo wameibadilisha kidogo tu matamshi yake. CHAMA CHA AMANI(CCA) kinamini Kishwahili Chetu kikiheshimiwa na kupewa stahiki yake kama Lugha ya Taifa HURU, kinaweza kutumika kama Lugha si ya mawasiliano tu bali pia Lugha ya biashara, michezo/fani na Elimu.

2. Akili na Uelewa: Watanzania wana Akili na Uelewa wa hali ya juu sana nadhani kuliko Taifa lolote Ulimwenguni. Akili na Upeo wa uelewa huu bado umelazwa. Watanzania bado hawajapata mtu wa kuwaamsha na kuwaambia waanze kutumia akili na uelewa walionao. CHAMA CHA AMANI(CCA)tunamini kwamba akili za watanzania zikiamshwa na kuamrishwa kuanza kufikiri tunaweza kuwa na Taifa lililoendelea kwenye Uvumbuzi na teknolojia ya hali ya Juu sana ulimwenguni na hivyo Watanzania tukawa sio soko la kujaribia teknolojia na bidha za wenzetu. Watanzania wenyewe tutabuni na kutengeneza Viwanda vitavyozalisha bidhaa zinazotufaa kwa matumizi yetu kwanza kabla ya kupeleka mgao kwa majrani zetu. Nchi haiwezi kuwepo ikiwa inatumia bidhaa, technolojia na elimu ya nchi nyingine.

3.Uhuru: Tunaamini kwamba Binadamu wote ni zao la Imani. Mpaka sasa hakuna sayansi wala nchi wala serikali yoyote iliyofanikiwa kufafanua asili ya mwanadamu. Hivyo wote bado tunaamini mwanadamu ni Zao la Imani. kama ni Hivyo basi hakuna mwanadamu mwenye amri kubwa zaidi juu ya mwenzake. Hakuna Taifa lenye mipaka yake na serikali yake linaloweza kuingilia matakwa na kutunisha misuli yake kwenye taifa Jingine. CHAMA CHA AMANI (CCA) Tunamini Hilo, Kwa Hivyo Tuna kila sababu ya kuidai Tanzania HURU. Mataifa yanayojiita yenyewe makubwa.. basi kwa Ukubwa wao uwe pia ukubwa wa uelewa wao, watuelewa Hivyo na kuheshimu Uhuru wa Taifa Hili kama majarida ya Umoja wao yanavyofafanua. Hatutaki Ukloni mamboleo, hatutaki kpangia nini na lini tufanye nini, Tunapohitaji kuchagua viongozi wetu tuacheni tutumie rasilimali na uwezo tulionao sio kupewa msaada na pesa kwenye kila kitu. Tunahitaji kumiliki migodi na rasilimali zote za inchi yetu, ni zetu, tuachieni tufanye kile tunachodhani ni sahihi ndani ya mipaka yetu, hatuhitaji mtufundishie Jeshi letu nani wa kumpiga na wapi pa kumpiga, Tuacheni tujijue wenyewe, kwani Nie nani aliwafundisha? kiasi kwamba mjipe kuwa walimu wa wengine. Hatuhitaji silaha zenu, tunahitaji Kutengeneza na kutumia za kwetu kwa mbinu za kwetu pia. Toka lini mtu akamuuzia adui yake silaha yenye uwezo wa kumpiga yeye mwenyewe? haiwezekani.. Daima mnatuuzia silaha hafifu zinazotugombanisha na kuuana sisi kwa sisi. INATOSHA. Sisi ndio tunapaswa kutoa misaada sio kupewa misaada. Tanzania Mpya Inakuja.. Mimi wewe na sisi Tutaiwezesha. AMANI DAIMA!

Asanteni

Hiyo no.2 mkuu naitilia shaka make kama kweli ndivyo basi haya matatzo tunayoyapigia kelele kila siku yangeishaisha ...sasa tusaidie kama akili tunayo tatzo letu ni nini?

Yawezekana tuna akili ila uelewa wetu ni mdogo ama sivyo kinyume chake.

Tunaposema watanzania Akili na Uelewa wetu bado Umelazwa, tuna maanisha nini..
Akili ni uwezo ambao binadamu yeyote anao, ambao watanzania Tunao zaidi. Ili mtu aweze kuitumia akili yake barabara lazima kuwepo na nyenzo. Unafikiria kwanza kisha unapewa nyezo ili kile ulichokifikiria ukiweke kwenye uhalisia wake. Na hakuna nyenzo ambayo ni bure, kila nyenzo in gharama zake. Hivyo lazima Taifa liwe tayari kuwapatia watu wake nyezo (pasipo kuwatoza gharama) ili kile wanachokifikiria na kukiwaza kwenye asili ya mawazo yao wajaribu kikiweka kwenye uhalisia. Hii ndio maana ya Idea Generation. nchi inapownyima wananchi wake nyezo hii muhimu ni kuzilaza akili zao kwa nguvu. ama wanajua ama hawajui. Si Umma wa watanzania wote ambao utajikita kwenye kufanya tafiti na vumbuzi hizi ila wapo wananchi ambao wamekasmiwa uwezo huo na Mwenyezi Mungu ni lazima wathaminiwe na kupewa wigo wa kufanya kile wanachokifikiri bila kuwahukumu. Mataifa Yote tunayoyaita yameendelea imagine mpaka leo wanatumia mawazo binafsi ya wananchi wao waliotangulia mfano Nelcon, Isaac newton, Kary Max na wengineo. hao waliweza.. sisi tutashindwaje kuweza? Tunaweza. Si mawazo Yote yatakuwa yenye maana na msingi ila kati ya kumi lazima moja litakuwepo lenye mnufaa. CCA tunaamini kwamba Akili ambazo hazijachafuliwa na elimu za Kigeni zina wigo mzuri wa kufikiria. na wazo moja zuri laweza kuwa ukombozi kwa Taifa na Mataifa. Embu ona Utumwa huu. Mtu aliyesoma sana elimu ya mtu mwingine, tukimanisha kwamba mtu akisoma sana na kujitahidi kuelewa mawazo ya mtu mwingine anaitwa msomi. Unapewa na shahada kadhaa kwamba wewe ni msomi, Dr, prop na mengineyo. Lakini yote uliyoyajaza kwenye ubongo ni mawazo ya mtu mwingine.. unaitwa msomi.. na unapewa heshima kwenye jamii. Ni Misingi wa utumwa ambao lazima Tuugundue na kuanza jitihada za kujitenga nazo. Vijana wetu masomoni na Vyuoni wananyanyaswa kwe kumezeshwa mawazo ya watu wengine wa mataifa ambayo hata haijulikani hasa asili yao. Hatupingi Elimu ila sasa lazima Tuchambue kizuri tukichukue na kuwaachia vingine ili nasi tutengeneze chetu.
Amani Daima!!
 
Nachelea kuchangia, kwa sababu sijaona jambo jipya katika hii mistari takriban 27 iliyowekwa katika hii thread.

Chama Hiki jukumu lake si Dogo.. tunajua hili na Tunathubutu kwa hili.. Kuhakikisha watanzania wanafunguka na kupata uelewa na kujijua wao ni akina nani na nini tunatakiwa sasa tufanye. Kumwamsha mtu mmoja na kumwonyesha stahili yake ni kazi ngumu na ugumu zaidi ni pale inapogharimu kuamsha Taifa Zima. Lakini TUTAWEZA.. Na kama hatutaweza basi ni kipimo tosha kwetu kwamba hatuna wito kwa Hili.

Amani Daima
 
Mkuu huoni kwamba ingekuwa bora mkaungana nyie wote na wapinzani wengine ili kwanza common enemy atoke na afilisiwe hapo ndio muanze kila mtu kwenda kivyake..?

Umoja ni Nguvu
 
Hiki CCA ni CCJ iliyojivua gamba? Tafuteni jina jingine acheni kutumia utabiri wa Shehe Yahaya mfuga majini kuwa chama kitakachokuwa na nguvu kitaitwa CCK au CCN! Achaneni na mawazo ya kimagamba magamba! CDM ndo chama letu!
 
Hiki CCA ni CCJ iliyojivua gamba? Tafuteni jina jingine acheni kutumia utabiri wa Shehe Yahaya mfuga majini kuwa chama kitakachokuwa na nguvu kitaitwa CCK au CCN! Achaneni na mawazo ya kimagamba magamba! CDM ndo chama letu!

Mbona pro-cdm mna matatizo aisee agh

Vyama vingi vipo kwasababu kuna watu hata ufanyeje hawawezi kuwa chadema ndio uhuru huo

Bravo cca..mwaga sera
 
Hiki CCA ni CCJ iliyojivua gamba? Tafuteni jina jingine acheni kutumia utabiri wa Shehe Yahaya mfuga majini kuwa chama kitakachokuwa na nguvu kitaitwa CCK au CCN! Achaneni na mawazo ya kimagamba magamba! CDM ndo chama letu!

Kama hii ndio CCJ basi nakiunga mkono nitaunga mkono upinzani wowote ndani ya CCM kwani hii itasaidia kuleta mapinduzi Tanzania
 
Kama hii ndio CCJ basi nakiunga mkono nitaunga mkono upinzani wowote ndani ya CCM kwani hii itasaidia kuleta mapinduzi Tanzania

Uzuri moja ccm tunapanga agenda vyama vingine wanatekeleza ikiwemo chadema..

Mtaimba nyimbo zetu ..for coming years (not less 20)
 
Hicho chama ni cha siasa au ni kama saccos? Nadhani hatuna haja ya kuwa na mushrooming political parties,PEOPLES POWER yatutosha.okeeee?
 
Uzuri moja ccm tunapanga agenda vyama vingine wanatekeleza ikiwemo chadema..

Mtaimba nyimbo zetu ..for coming years (not less 20)

Mkuu mimi sishabikii vyama kama timu za mpira..., nimeshaona kwa ufisadi uliopo Tanzania na watu walafi na majambazi nchi haitafanikiwa bila kuwa na upinzani wa kweli na wenye nguvu..., na ni vigumu kuwa na upinzani wa kweli wakati chama kimoja kimejichukulia mali nyingi ambazo ni za wananchi (vitega uchumi) na wanatumia ubavu huo kuendelea kuwa madarakani

In short CCM ni kama kupe na ningesema hivyo hivyo kwa chama chochote ambacho kingekuwa pale ambapo CCM ipo (Power Corrupts)
 
Mkuu mimi sishabikii vyama kama timu za mpira..., nimeshaona kwa ufisadi uliopo Tanzania na watu walafi na majambazi nchi haitafanikiwa bila kuwa na upinzani wa kweli na wenye nguvu..., na ni vigumu kuwa na upinzani wa kweli wakati chama kimoja kimejichukulia mali nyingi ambazo ni za wananchi (vitega uchumi) na wanatumia ubavu huo kuendelea kuwa madarakani

In short CCM ni kama kupe na ningesema hivyo hivyo kwa chama chochote ambacho kingekuwa pale ambapo CCM ipo (Power Corrupts)

Unasahau tu unachoshabikia sasa hivi kiko corrupts kabla ya kuingia madarakani..as a matter of fact wanacheza agenda ya ccm..
 
Unasahau tu unachoshabikia sasa hivi kiko corrupts kabla ya kuingia madarakani..as a matter of fact wanacheza agenda ya ccm..
Mimi sishabikii chama chochote.., ila ni bora kuwe na vyama vingi vyenye nguvu sawa ingawa vyote vikiwa corrupt ila vitachungana na kuangaliana ili viingie kwenye utawala.., mfano mzuri sasa ni Bungeni yaani ni NDIO mtindo mmoja hata kama ikiwa ni Pumba
 
Mkuu huoni kwamba ingekuwa bora mkaungana nyie wote na wapinzani wengine ili kwanza common enemy atoke na afilisiwe hapo ndio muanze kila mtu kwenda kivyake..?

Umoja ni Nguvu

Ni kweli Ndio Maana mpaka sasa Nguvu na Nia Zetu tumezielekeza Upinzani. ingawa tunakiri wazi kwamba Tunatofautiana kwenye Itikadi na Mitazamo. Ila Kwanza Tumejizatiti Kuhakikisha Chama Kilichopo madarakani kwanza Kinaondoka Madarakani
 
Hiki CCA ni CCJ iliyojivua gamba? Tafuteni jina jingine acheni kutumia utabiri wa Shehe Yahaya mfuga majini kuwa chama kitakachokuwa na nguvu kitaitwa CCK au CCN! Achaneni na mawazo ya kimagamba magamba! CDM ndo chama letu!

Usiwe mwepesi sana wa kutabiri au kubashiri kisha ukahukumu.. Daima uwe mzalendo.. wewe ni muhimu sana ndani ya jamii yetu.. usijidharau, kitakuwa ni chama kipya, hakina Doa wala harufu ya Chama tawala. wala hakitatahitaji chombo chakavu chochote kama malighafi yake.
 
Hicho chama ni cha siasa au ni kama saccos? Nadhani hatuna haja ya kuwa na mushrooming political parties,PEOPLES POWER yatutosha.okeeee?

Ushabiki ni kitu kizuri na Hatari sana.. Hasa pale ushabiki wa Siasa unapofananishwa na ushabiki wa mpira. Tukumbuke kwenye uchaguzi wa 2005, asilimia kubwa ya watanzania hawakuichagua CCM bali walimchagua Kikwete, ambao haohao leo hii amegeuka kuwa chungu kwao. Ni hatari kushabikia Chama au mtu pasipo kuangalia sera na katiba yao. Ndio maana tunasema watanzania wengi tusiwe wavivu wa kufikiria. na mtu huwezi kufikiria kabla ya kusoma. pitia sera na katiba ya chama husika kisha ujiridhishe na kukichagua. Tusijekichagua chama kabla ya kusoma sera na katiba yao kisha mbele ya safari tukawa maadui wakubwa wa chama hicho.
 
Ushabiki ni kitu kizuri na Hatari sana.. Hasa pale ushabiki wa Siasa unapofananishwa na ushabiki wa mpira. Tukumbuke kwenye uchaguzi wa 2005, asilimia kubwa ya watanzania hawakuichagua CCM bali walimchagua Kikwete, ambao haohao leo hii amegeuka kuwa chungu kwao. Ni hatari kushabikia Chama au mtu pasipo kuangalia sera na katiba yao. Ndio maana tunasema watanzania wengi tusiwe wavivu wa kufikiria. na mtu huwezi kufikiria kabla ya kusoma. pitia sera na katiba ya chama husika kisha ujiridhishe na kukichagua. Tusijekichagua chama kabla ya kusoma sera na katiba yao kisha mbele ya safari tukawa maadui wakubwa wa chama hicho.

Hatuchagui sera (hiyo ya kila chama ni nzuri kwasababu ni marketing tool)

Tunachagua mtu makini na muungwana mpenda haki..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom