Tanzania kwakuibiwa na kudanganywa ni nzuri sana

Shine

JF-Expert Member
Feb 5, 2011
11,481
1,364
Tanzania ni nzuri sana: Umeme upo lakini hauwashwi,
Mafuta yapo lakini hayauzwi,
Mafisadi wapo lakini hawafungwi,
Rais mzembe lakini hajiuzulu,
Mahakama inauzwa ili kujenga Hotel,
Mhindi anatoa masaa 24 mafuta yapandishwe bei,
Tumebaki kudanganywa maisha bora kwa kila Mtanzania, yako wapi hayo maisha bora?
Vijijini maji safi hakuna,
Hospitali madawa hakuna,
Walimu hawalipwi mishahara!
Wakubwa wakiugua wanaenda kutibiwa nje,
Walala hoi wanabanana Muhimbili kitanda kimoja wagonjwa watatu,
Na ndio nchi pekee tunayotoa madini ya TANZANITE Duniani,
wameachiwa makaburu wanachukua buree sisi tunaachwa na mahandaki yasiyokuwa na mwisho! lakini tufanye je?
Kheri ya nusu shari kuliko shari kamili! Si tumeona yakiyotokea libya, Tunisia na kwingineko?

waTZ vijana tuamke kuinusuru nchi yetu kwakuchukua hatua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom