Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Kuna mzee mstaafu nilikutana naye alinieleza mambo ya ajabu ya namna ya kuinua mauzo ya bidhaa za Tanzania.
Aliniambia kuwa Kuna kiwanda Tanzania kilikuwa kinajulikana kama LIGHT SOURCE kilikuwa kinatengeneza taa (Bulbs) kikiwa pale kule Pugu ROAD Dar es salaam mkono wa kulia kama unaenda Airport karibu na D.T.DOBIE.Kabla ya kufilisika kilifikia mahali kikawa hakina hela kabisa kiasi cha kushindwa kulipa mishahara na pesa za likizo za wafanyakazi wake.
Uongozi wa kiwanda ukasoma sheria za kazi na kodi wakaona mahali pameandikwa payments benefits can be in cash or in kind
Wakati ule bulb zilikuwa zimejazana kwenye bohari ya kiwanda zikiwa haziuziki kutokana na soko huria na ushindani.Basi ikawa mfanyakazi ukiomba likizo ilikuwa hulipwi mshahara hela taslimu bali unapigiwa pesa yako inayolingana na hela ya Likizo halafu unapewa mabox ya balbu zinazolingana na hela ya likizo ukauze uende zako likizo huko kijijini kwenu.
Mzee huyo akashauri kuwa Ili kuongeza soko la bidhaa zetu zinazozalishwa ndani ni vyema wafanyakazi wa serikali Tanzania wawe wapewe vitu vinavyozalishwa Tanzania wakauze ili wapate hiyo mishahara na marurupu yao badala ya kuwapa hela Taslimu.Akasema kitu kama hicho kitakasaidia kupanua soko la bidhaa zetu na watu watapenda kuziuza na kuzitumia maana watu watapigana kufa na kupona ili wauze wapate chao.Pia itasaidia kupata ufumbuzi wa wa wafanyakazi wanaolalamikia serikali kuwa mishahara ni midogo haitoshi kwa kuwa kila mmoja itakuwa ni juhudi yake tu ukiongea vizuri ukapata bei kubwa zaidi unapouza kile cha juu ni halali yako.
Fikiria Raisi Kikwete mwisho wa Mwezi umefika halafu anapewa mananasi yaliyokosa soko Kijijini kwao Msata akayauze huko kwenye safari zake anazoenda nje mara kwa mara ili apate posho za safari na mshahara wake si uchumi ungeinuka?
Habari ndo hiyo.
Wadau mnasemaje?
Aliniambia kuwa Kuna kiwanda Tanzania kilikuwa kinajulikana kama LIGHT SOURCE kilikuwa kinatengeneza taa (Bulbs) kikiwa pale kule Pugu ROAD Dar es salaam mkono wa kulia kama unaenda Airport karibu na D.T.DOBIE.Kabla ya kufilisika kilifikia mahali kikawa hakina hela kabisa kiasi cha kushindwa kulipa mishahara na pesa za likizo za wafanyakazi wake.
Uongozi wa kiwanda ukasoma sheria za kazi na kodi wakaona mahali pameandikwa payments benefits can be in cash or in kind
Wakati ule bulb zilikuwa zimejazana kwenye bohari ya kiwanda zikiwa haziuziki kutokana na soko huria na ushindani.Basi ikawa mfanyakazi ukiomba likizo ilikuwa hulipwi mshahara hela taslimu bali unapigiwa pesa yako inayolingana na hela ya Likizo halafu unapewa mabox ya balbu zinazolingana na hela ya likizo ukauze uende zako likizo huko kijijini kwenu.
Mzee huyo akashauri kuwa Ili kuongeza soko la bidhaa zetu zinazozalishwa ndani ni vyema wafanyakazi wa serikali Tanzania wawe wapewe vitu vinavyozalishwa Tanzania wakauze ili wapate hiyo mishahara na marurupu yao badala ya kuwapa hela Taslimu.Akasema kitu kama hicho kitakasaidia kupanua soko la bidhaa zetu na watu watapenda kuziuza na kuzitumia maana watu watapigana kufa na kupona ili wauze wapate chao.Pia itasaidia kupata ufumbuzi wa wa wafanyakazi wanaolalamikia serikali kuwa mishahara ni midogo haitoshi kwa kuwa kila mmoja itakuwa ni juhudi yake tu ukiongea vizuri ukapata bei kubwa zaidi unapouza kile cha juu ni halali yako.
Fikiria Raisi Kikwete mwisho wa Mwezi umefika halafu anapewa mananasi yaliyokosa soko Kijijini kwao Msata akayauze huko kwenye safari zake anazoenda nje mara kwa mara ili apate posho za safari na mshahara wake si uchumi ungeinuka?
Habari ndo hiyo.
Wadau mnasemaje?