Tanzania kama hatuna rais vile

K007

Member
Jan 30, 2011
52
3
Kiukweli binafsi sioni cha maana alichofanya muongoza nchi wetu(rais) tangu atinge ikulu zaidi ya kuonesha udhaifu katika utendaji wake.

Nnavyojua mimi ni kwamba kiongozi lazima awe na vifu fulani adimu ambavyo hata wanaoongozwa wanaona kabisa bila huyu kiongozi jambo fulani haliwezi kwenda vizuri.

Lakini kwa Tanzania sasa hivi kila mtu anaendesha maisha yake binafsi kuanzia ngazi ya familia hadi taifa bila kumtegemea rais wetu wa nchi, hii inaonesha wazi kwamba hivi sasa kila Mtanzania ni RAIS binafsi anayejiongoza katika kuendesha maisha yake ya kila siku.
 
Hayo ndiyo matokeao ya kuchagua viongozi kwa ushabiki wa kijinga. Hakuwa na rekodi nzuri hata kwenye uwaziri. Mpaka anaondoka madarakani atakuwa ameacha pumba tupu.
 
The same to me ndugu yangu ukiniuliza ni kitu gani kizuri kitanifanya nimkumbuke kikwete kama rais wangu kiukweli sina jibu mpaka kesho.
 
Utapata tu kitu cha kumkumbuka maana wote wametuachia kumbu kumbu mbali mbali.Nyerere watu walivaa magunia,huoni sukari sabuni wala mkate hata sigara.Mwinyi ye alikuwa ruksa kila kitu hela zikahamia kwa raia.Mkapa mikataba mibovu yote ya madini na uozo wa ufisadi wa RICHMOND NA EPA,na Kikwete utapata tu la kuweka kumbu kumbu usijali.
 
kweli kabisa hakuna lamuhimu lakujivunia kwake au kumkumbuka kwa jambo lamaana!! Nakumbuka kipindi cha uhai wa Mlm.Nyerere (94/95) walipendekeza mtu wakugombea urais,baadhi wakamchagua kikwete ila Nyerere akakataa akasema huyu bado mdogo (mtoto)! Wengi walijua utoto wake upo kwenye umri kumbe LA (sivyo),Mwalimu Nyerere aliona mbali! Utoto wake upo kwenye mambo ya starehe zaidi, hana mawazo yakimaendeleo,hayupo serious na maisha ya majority!! Na wengi tulijua nimtu wawatu atafanya mambo for watu ila ikawa kinyume chake!! Tanzanian TUAMKE TUSIJEFANYA KOSA KWENYE CHAGUZI ZIJAZO,Ona inavyotu-cost,vijana wasasa wanasema inakula kwetu..
 
kheee yani unasema huoni alichaofanya kikwete au?haya ngoja nikupe haya uwe nayo kama kumbukumbu:-kuleta bajaj za kubeba wajawazito,kucheka na wahujumu uchumi,kwenda nje ya nchi kama anaenda kwao bgamoyo,kutojitambua kama raisi,kutoa kauli au hotuba za kukera na kutia hasira na kubwa zaidi mkumbuke kwa kuwa handsome na gud dancer wa kiduku na bongo flavour....ooh!!nimekumbuka,na hii ni RAIS WA KWANZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI MWENYE DOCTORATE.
 
Everytime this guy is delivering a speech he is always stammering .....i ask myself...why? could it be that he isnt sure of what is saying or what? Kama ile ya jana hazina.....eeeh...eeh...eh nyiiingi na na kuchezeshachezesha mikono hizi zote ni dalili za kutokuwa na uhakika wa jambo unalolisema au kutokujiamini...kutokujiamini pia ni result za self conciousness
 
Kiukweli binafsi sioni cha maana alichofanya muongoza nchi wetu(rais) tangu atinge ikulu zaidi ya kuonesha udhaifu katika utendaji wake.

Nnavyojua mimi ni kwamba kiongozi lazima awe na vifu fulani adimu ambavyo hata wanaoongozwa wanaona kabisa bila huyu kiongozi jambo fulani haliwezi kwenda vizuri.

Lakini kwa Tanzania sasa hivi kila mtu anaendesha maisha yake binafsi kuanzia ngazi ya familia hadi taifa bila kumtegemea rais wetu wa nchi, hii inaonesha wazi kwamba hivi sasa kila Mtanzania ni RAIS binafsi anayejiongoza katika kuendesha maisha yake ya kila siku.

Mkuu hayo ni kweli kabisa. Mheshimiwa kaenda likizo labda bado anasherehekea ushindi pale magogoni na nje. Kiuhalisia ningependa raisi ambaye anatofautisha mabadiliko na maendeleo. Mabadiliko si lazima yawe maendeleo inavyoonekana serikali inakazania mabadiiko kuliko maendeleo. Pia wananchi nadhani tunalo jukumu sasa la kudai vyote kwa maslahi ya taifa zima.
 
naona kwenye jopo la wanaokwenda kumuona gadafi wamemwacha! ndo maana anaenda kutembea kwenye wizara kutoa maelekezo badala ya kutoa ufumbuzi!!
 
Nafikiri hili ni langu moyoni lakini kumbe wengi tu linawagusa, ni kweli nchi haina kiongozi shujaa ambaye siku anahutubia taifa watu wote wanakimbilia kwenye Luninga - Lakini imefikia wakati akitokea kwenye Luninga zetu watu wanabadilisha channel kwa kusema "Toa usanii huo" hivi usalama wa taifa hawamwambii kuhusu mambo haya ya uswazi kwenye TV za jumuia?
 
Sijawahi mtia JK machoni zaidi ya kwnye TV. Sijui siku nikimuona itakuwaje, nisijepandwa na hasira na kumtemea mate au kurusha kiatu.

Jamaa anachezea nchi kama vile taasisi yake binafsi.:hatari:
 
Huyu jamaa anaaenda nje kama anaenda Bwagamoyo-Chalinze. Jamaa kwa mfano Mashetembelea Marekani mara nyingi kuliko alivyotembelea kule kwetu Shycom! Sasa je Huyu tumuite rais wa TZ au Raisi wa Mambo ya Nje???
 
mm pia sion jipya alilofanya, anazunguka tu katika nchi mbalimbali, nina waswas hata japan ataenda kutoa pole, kwa kweli mi naona kama hii nchi haina rais kwa sasa, kila mtu anajiongoza peke yake
 
Back
Top Bottom