Tanzania Inakwenda Wapi? Chanjo kwa watoto hazipatikani, kodi zetu zinaenda wapi?

Pole sana ndugu yangu. CCM wamekandamiza Bilioni mbili na ushehe leo tu! Ndio Maisha Bora hayo ya Captain wa mafisadi.
 
Poleni sana Watanzania Kwa yanayowapata.Nadhani kama Kikwete anahitaji kumwajibisha mtu basi hili lina ushahidi achukue hatua maana hahitaji tume hapa.
Ndugu wana JF Kitu cha kwanza kufanyika ni kwamba kuhakikisha vyombo vyote vya habari Tz vinashika bango hili suala na hata kutoandika yaliyojiri Dodoma. Pili kumshinikiza mkuu wa kaya Kumwajibisha waziri, naibu wake, katibu mkuu, Boharia wa madawa na wengine wanaohusika na utoaji taarifa, utoaji maamuzi kwenye wizara husika.

Tutaendelea kuchezea Maisha ya watu hadi lini? Si ajabu waziri kaacha kufanya kazi ofisini na kukimbizana na kampeni za chama bila kujali maisha ya watu yaliyo hatarini. It is time for action.
Wana JF tunaoweza wa kushawishi maggazeti na vyombo vya habari pamoja na kuweka propaganda za kuhakikisha mtu walau mmoja anawajibishwa. Take action Nowwwwwww

Nawakilisha
 
Poleni sana, nyinyi mtakaa kujadili kuhusu chanjo wenzenu hela zote wanamaliza katika kikao cha kamati kuu ya CCM. Uliza wametumia kiasi gani kufanya hicho kikao chao cha kuchagua wajumbe wa NEC na zimetoka wapi kama sio hizo hizo za walipa kodi.
 
jamani, jana nilipata mshituko wa ajabu, nilikwenda pharmacy moja nikakutana na akina mama wawili wanatafuta gloves eti wametumwa na zahanati ya "KIWANJA MPAKA" iliyoko soko matola Mbeya kuwa wakatafute hivyo vifaa kwa ajili ya ndugu yao anaetarajia kujifungua. Kwa bahati mbaya katika duka hilo gloves zilikuwa zimekwisha wakachanganyikiwa- walikuwa hawajui waende wapi saa tatu na nusu usiku. Hii haingii akilini? Gloves za shilingi mia mbili hazipo?
 
jamani, jana nilipata mshituko wa ajabu, nilikwenda pharmacy moja nikakutana na akina mama wawili wanatafuta gloves eti wametumwa na zahanati ya "KIWANJA MPAKA" iliyoko soko matola Mbeya kuwa wakatafute hivyo vifaa kwa ajili ya ndugu yao anaetarajia kujifungua. Kwa bahati mbaya katika duka hilo gloves zilikuwa zimekwisha wakachanganyikiwa- walikuwa hawajui waende wapi saa tatu na nusu usiku. Hii haingii akilini? Gloves za shilingi mia mbili hazipo?

..ndio tanzania hiyo!

..ila,ahadi ya maisha bora kwa kila mtu ni challenge kubwa si mchezo!

..huwa najiuliza,je?are we up to it?sababu longolongo nyingi!
 
Pole sana ndugu yangu. CCM wamekandamiza Bilioni mbili na ushehe leo tu! Ndio Maisha Bora hayo ya Captain wa mafisadi.

Harafu eti wanakaa kwenye vikao vyao vya ccm na kuanza kuwakilisha mafanikio waliyoyafanya (huku wakiponda pesa za walipa kodi), mafanikio gani hayo iwapo wizara ya Afya inashindwa kushughulikia suala muhimu kama la chanjo kwa watoto, je wanajua watoto watapata mazara gani kwa kukosa huduma muhimu kama chanjo????? sisi yetu macho tu,MPAKA HAPO JESHI LITAKAPO AMUA KUCHUKUA NCHI YAO.
 
Mimi pia ni muhanga wa tatizo hilo. maaskini kabinti kangu kana miezi miwili chanjo kamepata juzi maana zilifika alhamisi. Domokaya kacheki hospital. Wamaiba pesa hata za chanjo kufanyia kampeni za chama. ama kweli hata laana za vichanga hivi washazipata. halafu utawasikia kila kukicha eti wana prevent mortality rate kwa under five years. Non sense.
 
Back
Top Bottom