Tanzania inaendelea na biashara haramu ya siraha?

Mongoiwe

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
524
263
Inashangaza Tanzania kujiita Kisiwa cha amani, nchi yenye utulivu, huku tukilalamikia kuongezeaka kwa vitendo vya Uharifu kuwa kunatokana na Idadi kubwa ya wakimbizi ambao wametokana na Nchi zenye mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, huku Tanzania hiyo ikiendelea na usafirishaji wa Siraha haramu katika nchi zinazopigana vita.

Katika hali isiyotazamiwa katikati ya Jiji la Mwanza kuna idadi ya vifaru 11 vya kijeshi vikiwa katika mabehewa ya Treni mali ya kampuni ya TRL eneo la 'Mwanza South', Inasemekana kuwa vipo hapo kugonjea kusafirishwa kwa Meli kuvuka kwenda nchini Sudani kupitia Uganda.

Haijafahamika Vifaru hivyo vimetokea wapi kupitia Reli ya kati, lakini duru za Kijeshi zimebainisha wazi kuwa huenda vikawa vimetokea katika Bandari ya Salama.

Kwa wanaokaa Jijini Mwanza maeneo ya Mkolani, Nyegezi, Buhongwa na hata Malimbe watakuwa wameviona vifaru hivi kwa vile vinaonekana kwa urahisi sana uwapo katika barabara ya Mwanza Shinyanga hata katika gari ingwa vimefunikwa kwa Maturubai.

Vifaru hivi vimeoneka hapo kuanzia Jumamosi mpaka jana Jumapili jioni na kwa sasa vinadaiwa vimepakiwa katika meli kusafirisha Usiku.

Iwapo ni kweli Vifaru hivi ambavyo vimeonekana hapa Mwanza vinasafirishwa kwenda nchini Sudani basi jambo hili litazidi kuingiza Tanzania katika kashfa ya biashara usafirishaji siraha haramu ama kudhihirisha repoti ya CCTI kuhusu Meremeta iliyoandaliwa na Mwanakijiji.
 
We're not sure who owned that tanks, may be M7 or south sudan, and not neccessarily belong to Tanzania. Tanzania is a gateway, neighbor countries used our port to transport their luggages include weapons. Last year, Burundi through TRL, transported many tanks, DRC and uganda are our clients too. Sisi tunahitaji michuzi si kitu kingine. Today Frence has sold a naval warship to Russia, why not TZ????
 
We're not sure who owned that tanks, may be M7 or south sudan, and not neccessarily belong to Tanzania. Tanzania is a gateway, neighbor countries used our port to transport their luggages include weapons. Last year, Burundi through TRL, transported many tanks, DRC and uganda are our clients too. Sisi tunahitaji michuzi si kitu kingine. Today Frence has sold a naval warship to Russia, why not TZ????

Hili taifa ni balaaaaaa
 
Hili taifa ni balaaaaaa

Tanzania yaingizwa katika kashfa nzito ya silaha DRC

  • YADAIWA KUWASAIDIA SILAHA WAASI DRC, MEMBE AWAKA, ATAKA IOMBWE RADHI
%5Cmembewaukweli.jpg
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe ambaye ameitaka UN kuiomba radhi Tanzania kutokana na tuhuma za kuhusika katika kusafiri silaha kwa waasi wa Congo

Na Jackson Odoyo

WAKATI Umoja wa Mataifa (UN) ukiitupia shutuma nzito Tanzania kuwa inasaidia kusafirisha silaha kwenda kikundi cha waasi nchini Congo, serikali imekanusha na kutaka iombwe radhi.

Ripoti iliyotolewa mwishoni mwa wiki na kikundi cha UN kilichokuwa nchini DRC kutathimini hali ya usalama, imeeleza kuwa Tanzania imekuwa ikisaidia silaha kikundi cha waasi wa nchi hiyo.

Kikundi hicho cha wataalamu wa UN kilichokuwa eneo la mashariki ya DRC kimeeleza kuwa kimeshindwa kuwapatanisha waasi hao kwa kuwa wanapata misaada na nchi jirani, ikiwemo Tanzania.

"Nyaraka zimedai kuwa rasilimali za madini zimeendelea kuhujumiwa na kwamba pia kuna ongezeko kubwa la vitendo vya ubakaji na mauaji ya raia," inasema taarifa hiyo iliyovujishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari duniani ambayo Baraza la Usalama la umoja huo limepanga kuijadili.

Ripoti hiyo pia imewatuhumu baadhi ya askari wa Congo kuvisaidia kwa silaha vikundi vya waasi wakilipwa mamilioni ya dola zilizopatikana kutoka kwenye migodi waliyovamia.

Taarifa hiyo imekuja wakati Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi 25 zinazosaidia mtandao wa kimataifa wa kulinda amani nchini Rwanda.

Hata hivyo, ripoti nyingine za taasisi za kimataifa zilizowahi kutolewa awali zimekuwa zikiituhumu Tanzania kuisaidia serikali ya Joseph Kabila kupambana na waasi wa nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe alisema juzi kuwa taarifa hiyo haina ukweli na kukitaka kikundi cha hicho kuiomba radhi Tanzania kwa tuhuma hizo zisizokuwa na msingi.

Alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Port of Paris- Trinidad na taarifa yake kusomwa na kituo cha televisheni cha TBC1 katika taarifa ya habari ya saa 1:00 asubuhi jana.

Alisema taarifa hiyo iliyotolewa na kikundi hicho si sahihi vinginevyo kithibitishe kwa kueleza silaha hizo zimetoka wapi na kugawiwa kwa nani kupitia njia gani.

"Tunaamini kwamba taarifa hiyo haikutolewa bure, lazima kuna kitu nyuma yake. Sasa tunataka waseme na kuthibitisha ukweli huo au watuombe radhi," alisisitiza Membe.

"Tungependa kutoa changamoto kwa kikundi hicho ambacho kinadai kutumwa na Umoja wa Mataifa kuthibitisha tuhuma ama kuomba radhi," alisema.

"Tunataka kiseme silaha hizo zimetoka wapi na kapewa nani, maana sisi katika majeshi yetu hatuna taarifa ya kutolewa silaha," alisema Membe.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi jana alisema hawezi kuzungumzia tuhuma hizo kwa sababu hajapata taarifa kamili kutoka UN.

"Siwezi kuzungmzia suala hilo leo kwa sababu taarifa hizo nimezisikia tu lakini taarifa kamili ya UN haijanifikia hivyo ni vigumu kusema chochote," alisema Dk Mwinyi na kuongeza:

"Taarifa ikinifikia nitaisoma na kesho (leo), nitaitolea tamko hivyo naomba tuvute subiri,"

Source: Mwananchi
 
hII HABARI IMENISTUA SANA JANA NILIPOISIKIA? iS IT TRUE?

Siyo wewe tu kwani hata mimi kwa mara ya kwanza nilipoona vile Vifaru nili Posti kuhoji iwapo Biashara hii (Meremeta) inaebndelea, na nilibahatika kuzungumza na waandishi kadhaa jijini Mwanza kuhusiana na jambo hilo ambao nao walinieleza kuwa walimtafuta waziri Hussen Mwinyi akawachenga kutoa majibu lakinbi kilichofanyika Vifaru hivyo viliamishwa siku hiyo na kuhifadhiwa katika yadi ya badari na kupakiwa melini to Uganda
 
SIO SIRAHA NI SILAHA.Kwa ujanja ujanja wa wabongo kitu hicho kinawezekana kabisa,kwa udhaifu wa viongozi wetu wajanja wachache wanaweza wakatumia kufanya dill na watawala wachache wenye uchu na pesa za kampen mwakani
 
Mod,

Same thread/topic as "Ripoti ya kuichafua Tanzania ni ya uzushi, uzandiki - Membe unayosema yana ukweli".

Mwanakijiji aliyasema haya kwenye ripoti yake ya Meremeta.Sijui tunapoelekea ila kuna siku hata hao majirani nao watatuchoka na kutugeuka.Hapo ndio utajua kupigwa kila upande.The so called "our friends" ndio hao hao watatugeuka na kutushambulia.By that time watakuwa wanamiliki nchi yetu vilivyo,ukianzia ardhi mpaka uchumi.

Mungu tusaidie Tanzania.Damu ya watu haimwagiki bure nchi za majirani - it will haunt us forever.
 
........................
Iwapo ni kweli Vifaru hivi ambavyo vimeonekana hapa Mwanza vinasafirishwa kwenda nchini Sudani basi jambo hili litazidi kuingiza Tanzania katika kashfa ya biashara usafirishaji siraha haramu ama kudhihirisha repoti ya CCTI kuhusu Meremeta iliyoandaliwa na Mwanakijiji.


Duuh Hiii ni kali kweli kweli si tuliambiwa Meremeta ni linahusu usalama wa taifaaa wajameni sasa imekuwaje huko Waziri Membe anajitetea sana kuwa twasingiziwaaaa??

Ni kashifa kubwa nani mbaya sana kwa Taifa kama kweli haya yanatendeka ndani ya nchi hii.

Kumbukeni tulikuwa mstari wa mbele kupigania uhuru kati na kusini mwa jangwa la sahara nchi zingine zijikomboe na kuwa Huru sasa twaanza onyesha mifano ya kupitisha siraha wenzetu wakauwane.

 
Mod,

Same thread/topic as "Ripoti ya kuichafua Tanzania ni ya uzushi, uzandiki - Membe unayosema yana ukweli".

Mwanakijiji aliyasema haya kwenye ripoti yake ya Meremeta.Sijui tunapoelekea ila kuna siku hata hao majirani nao watatuchoka na kutugeuka.Hapo ndio utajua kupigwa kila upande.The so called "our friends" ndio hao hao watatugeuka na kutushambulia.By that time watakuwa wanamiliki nchi yetu vilivyo,ukianzia ardhi mpaka uchumi.

Mungu tusaidie Tanzania.Damu ya watu haimwagiki bure nchi za majirani - it will haunt us forever.
nabata ushungu kwa hayo uliyosema kwani tushazungukwa tayari,iliyobaki tungoje kipigo,hii E.A.C ni tayari tuna maadui kila upande,hivyo vifaru ni vya mu7,na vijana wake wa kazi kagame na nkunda wale wote washatumika sana kwenye jeshi la museveni,hata elimu ya upiganaji msituni ya kagame kaipatia marekani lakini akitokea uganda kama ofisa wa jeshi la m7,sasa leo hao ndio wameungana na kujifanya wanataka kuwa jirani zetu,hiyo federation haina mwisho mzuri mi nakwambia tutakujalia na kusaga meno badae,nkunda alikua ni pandikizi la m7 na kagame,kagame katokea kwa mu7 na kufanya coup rwanda,sasa leo watashindwa kuja leta watu wao hapa T.Z?kama ilitokea jamaa wakapigania migingo island ambacho ni kisiwa sawa tu na bongoyo,sijui itakuwaje wakianza kupigania hizi mnaita rasilimali zenu,hao si watu,mda utasema
 
Duuh Hiii ni kali kweli kweli si tuliambiwa Meremeta ni linahusu usalama wa taifaaa wajameni sasa imekuwaje huko Waziri Membe anajitetea sana kuwa twasingiziwaaaa??

Ni kashifa kubwa nani mbaya sana kwa Taifa kama kweli haya yanatendeka ndani ya nchi hii.

Kumbukeni tulikuwa mstari wa mbele kupigania uhuru kati na kusini mwa jangwa la sahara nchi zingine zijikomboe na kuwa Huru sasa twaanza onyesha mifano ya kupitisha siraha wenzetu wakauwane.

Nimefanikiwa kupata Report hiyo na hapa naweka Summary:

Letter dated 9 November 2009 from the Group of Experts on the Democratic Republic of the
Congo addressed to the Chairman of the Security Council Committee established pursuant
to resolution 1533 (2004)
The members of the Group of Experts on the Democratic Republic of the Congo have the honour to transmit
herewith the final report of the Group prepared in accordance with paragraph 8 of Security Council resolution
1857 (2008).
(Signed) Dinesh Mahtani
(Signed) Raymond
Debelle
(Signed) Mouctar Kokouma Diallo
(Signed) Christian B.
Dietrich
(Signed) Claudio Gramizzi
Final report of the Group of
Experts on the Democratic Republic of the Congo
re-established pursuant to resolution 1857
(2008)
[Original: English]

Summary
This report concludes that military operations against the FDLR have failed to dismantle the organization’s
political and military structures on the ground in eastern DRC. The increasing rate of FDLR combatant
defections and the FDLR temporary removal from many of its bases are only a partial success considering
that the armed group has regrouped in a number of locations in the Kivus, and continues to recruit new
fighters. This report shows that the FDLR continues to benefit from residual but significant support from top
commanders of the FARDC, particularly those officers in the 10th military region (South Kivu), and has sealed
strategic alliances with other armed groups in both North and South Kivu . External support networks, both
regional and international, have been used by FDLR in the field to counteract the effects of Kimia II, for
instance networks in Burundi and Tanzania . The Group has also documented that the FDLR has a far
reaching international diaspora network involved in the day-to-day running of the movement; the coordination
of military and arms trafficking activities and the management of financial activities. This report presents two case studies on the involvement of individuals linked to faith-based organizations.
The Group investigated the FDLR’s ongoing exploitation of natural resources in the Kivus, notably gold and cassiterite reserves which the Group calculates continue to deliver millions of dollars in direct financing into FDLR coffers. This report illustrates how FDLR gold networks are intertwined tightly with trading networks operating within Uganda and Burundi as well as the UAE. The Group also documents that a number of minerals exporting houses, some of whom were named in the Group’s previous report in 2008, continue to trade with the FDLR.
This report shows that end buyers for this cassiterite include the Malaysia Smelting Corporation and the Thailand Smelting and Refining Company, held by Amalgamated Metals Corporation, a UK entity.
The report analyzes the integration of non-state armed groups into the FARDC through the rapid integration in January 2009; as well as prior and during the FARDC/RDF joint operation Umoja Wetu and Kimia II. In this context, the CNDP officer class, in particular General Bosco Ntaganda, has continued to retain heavy weapons acquired during its period of rebellion in spite of its official integration into the FARDC and still
controls revenue generating activities and parallel local administrations. The Group also presents documentary evidence showing that Gen Ntaganda continues to act as Kimia II deputy operational commander.
CNDP military officers deployed as part of FARDC Kimia II operations have profited from their deployment in mineral rich areas, notably at the Bisie mine in Walikale, North Kivu, and in the territory of Kalehe , in South Kivu . In both these areas, the FARDC commanding officers on the ground are ex-CNDP officers. The Group
includes evidence in the report showing direct involvement of CNDP military officials in the supply of minerals​
to a number of exporting houses in North and South Kivu , some of which also supply the same international companies mentioned above.
The Group has monitored compliance with paragraph 5 of resolution 1807 (2008), by which the Security Council decided that all states shall notify the Sanctions Committee in advance regarding the shipment of arms and related material for the DRC or any provision of assistance, advice or training related to military
activities, especially given the Group’s findings on the continued diversion of FARDC military equipment to non-governmental armed groups, notably the FDLR. The Group has conclusively documented irregular deliveries of arms to the DRC from the Democratic People’s Republic of Korea and the Sudan as well as deliveries of trucks and aircraft that have been used by the FARDC. This report also documents the failure of a number of States to notify the Sanctions Committee of training they provided to the FARDC.
The Group also reports on violations of human rights committed in contravention of subparagraphs 4 (d), (e) and (f) of resolution 1857 (2008): This report concludes that the FARDC and non-governmental armed groups continue to perpetrate human rights abuses, and in the context of Kimia II operations, in contravention of international humanitarian law. The FARDC and the FDLR have been involved in significant killings of civilians and other abuses from March to October 2009 causing additional waves of displacement of several hundred thousand civilians. The findings of this report underline the need for the urgent establishment of a vetting mechanism as well as the strengthening of accountability and justice system in the DRC. A list of FARDC
commanders currently deployed in the Kimia II operation, with an established record of human rights abuses is annexed to this report:


Kwa kusoma Ripoti Kamili fungua Attachment hapa chini:
 

Attachments

  • Group of Experts Report DRC (Nov.2009).pdf
    530 KB · Views: 104
kuna report zinatolea kwa ajili ya kuweka high tension kwa nchi kama hii report imeiweka tanzania katika high tension kwa kusudio la kuifanya tanzania ichukuwe more action katika vita hivi kwa mtazamo wangu wanaona Tanzania wanaweza kufanya vita hivyo vikaisha mara moja kwa msaada wa Tanzania.
 
We're not sure who owned that tanks, may be M7 or south sudan, and not neccessarily belong to Tanzania. Tanzania is a gateway, neighbor countries used our port to transport their luggages include weapons. Last year, Burundi through TRL, transported many tanks, DRC and uganda are our clients too. Sisi tunahitaji michuzi si kitu kingine. Today Frence has sold a naval warship to Russia, why not TZ????
Kweli mkuu watu wengine wanakurupuka
 
kuna report zinatolea kwa ajili ya kuweka high tension kwa nchi kama hii report imeiweka tanzania katika high tension kwa kusudio la kuifanya tanzania ichukuwe more action katika vita hivi kwa mtazamo wangu wanaona Tanzania wanaweza kufanya vita hivyo vikaisha mara moja kwa msaada wa Tanzania.
You was right
 
Back
Top Bottom