CPU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 3,863
- 686
CHAMA cha Wahandisi Washauri Tanzania (ACET), kimesema kuwa idadi ya wanawake wahandisi Tanzania ni ndogo ukilinganisha na nchi nyingine kwani mpaka sasa wahandisi waliopo ni wanne. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa ACET, Mwesigwa Kamulali, alisema pamoja na idadi hiyo ndogo amewataka wanawake wenye taaluma ya hiyo kujiunga na chama hicho ili kuweza kushirikiana na kutoa huduma katika jamii.
Tungependa kuwa na wahandisi wengi wanawake kama tulivyo sisi wanaume, tukiangalia idadi ya wahandisi wanne haitoshelezi kabisa kutoa huduma za ushauri wa kihandisi kwa ufanisi, alisema Kamulali. Alisema Chama cha Acet awali kilikuwa na wanachama tisa lakini mpaka sasa kina wanachama hai 94 ambao ni sawa na asilimia 47 ya wazalendo wahandisi washauri. Katika hilo, alisema chama hicho kinatarajia kufanya Jubilei ya kutimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwake Januari 27 mwaka huu.
Alisema katika Jubilei hiyo wanatarajia kuwa na wajumbe 200 na wageni kutoka nje 14 ambao watatoka Afrika ya Kusini, Botswana, Zambia, Kenya, Uganda , Sudan, Nigeria na Tunisia. Kamulali alisema katika maadhimisho hayo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda.