X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,809
Tanzania ina umwa, inaumwa homa kali
Taabani yaangamia, watu hawatafakali
Wenye nacho wanavuma, wakifaidi mali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Ina madonda ya utumwa, ufisadi na majangili
Na vikwazo vya uduma, vyote vinatuhadhili
Maradhi yanayochoma, tupo kama tumbili
Madawa na usalama, vyote kwetu ni ghali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Roho zetu zinauma, hali zetu ni dhalili
Viwanda bora vya umma, tumevitupa mbali
Wanatunyonya wazima, na tumeshika makali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Wako wapi walio wema, viongozi maadili
Tunalia lia mama, wanauza zetu mali
Twanyonya wetu uzima, tumekuwa kandambili
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Twaburuzwa kama uma, usokuwa na makali
Tunachinjwa kama nyama, twaliwa kama ugali
Hatuna mbele wala nyuma, tupo dhofu hali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Tusikubali kusimama, wala tusitulie tuli
Mafisadi wapo nyuma, tupigane tusikubali
Wapo kwenye nema wanatuona hatuna akili
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Bora tupate lawama, kuliko hii hali
Amkeni wana wema, tuondowe udhalili
Kusiwepo kusimama, tuondoe muhali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Taabani yaangamia, watu hawatafakali
Wenye nacho wanavuma, wakifaidi mali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Ina madonda ya utumwa, ufisadi na majangili
Na vikwazo vya uduma, vyote vinatuhadhili
Maradhi yanayochoma, tupo kama tumbili
Madawa na usalama, vyote kwetu ni ghali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Roho zetu zinauma, hali zetu ni dhalili
Viwanda bora vya umma, tumevitupa mbali
Wanatunyonya wazima, na tumeshika makali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Wako wapi walio wema, viongozi maadili
Tunalia lia mama, wanauza zetu mali
Twanyonya wetu uzima, tumekuwa kandambili
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Twaburuzwa kama uma, usokuwa na makali
Tunachinjwa kama nyama, twaliwa kama ugali
Hatuna mbele wala nyuma, tupo dhofu hali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Tusikubali kusimama, wala tusitulie tuli
Mafisadi wapo nyuma, tupigane tusikubali
Wapo kwenye nema wanatuona hatuna akili
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama
Bora tupate lawama, kuliko hii hali
Amkeni wana wema, tuondowe udhalili
Kusiwepo kusimama, tuondoe muhali
Tanzania ina umwa jahazi lenda mrama