Tanzania ina matajiri, je Wameifanyia nini Tanzania?

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Nikiangalia kwa kweli Tanzania ina matajiri walio na uwezo pengine kuizidi serikali ,kuna nchi moja jina kapuni ni ndogo tu ,ila nchi yenyewe ni tajiri na ina matajiri ,kiongozi mkuu siku moja machale yalimcheza na kuwaita matajiri wote ,ambao wana makampuni makubwa sana ,ya ujenzi na hata viwanda na mali zinginezo katika mkutano huo suali la kwanza aliwauliza kutokana na utajiri walionao ambao wameupata wakiwa ndani ya nchi wameifanyia nini nchi yao ,huku kiongozi huyo mkuu akiwa na data kamili za kila tajiri na pia akielewa kwa kina ni akina nani wanafanya juhudi za kujitolea kwa ajili ya nchi yao na hata wale wasiotoa nao pia alikwisha kuwa na taarifa nao.

Alipata majawabu mengi na yote hakusema kitu ila aliwambia wawe tayari kuisaidia nchi yao ,ikiwemo kujenga mabarabara mahospitali na mashule ikiwemo nyumba za ibada. Kwa kweli matajiri waliitikia wito na hata wale waliokuwa na ubakhili waliondoa ubakhili wao na kusaidia kwa kutoa michango na wengine kujengea nyumba sehemu zile ambazo wana asili nazo ,kwa mfano kijiji alichotoka kina nyumba hamsini mbovu mbovu zilizochoka na za zamani basi ,hujenga idadi ya nyumba hizo na kuwagaiwa wale wenye nyumba mbovu na zile nyumba mbovu hupigwa greda na sehemu hiyo huweza kujengwa shule au zahanati na misaada ikiendelea kwa aina hiyo kwa nchi nzima na maendeleo yalizidi kiasi kila mtu ana nyumba ya kisasa na sehemu bora za kufurahia watoto.

Je hapa tz matajiri tulionao wameifanyia kitu gani Tanzania ?
 
Matajiri wengi wa tz ni kwa nje tu mjomba wengine usiku wanalala bafuni, chooni , kwenye mkeka yaani full mazingaumbe hela zao hazina baraka na masharti kibao
 
Matajiri wengi wa tz ni kwa nje tu mjomba wengine usiku wanalala bafuni, chooni , kwenye mkeka yaani full mazingaumbe hela zao hazina baraka na masharti kibao
Wa aina hiyo sio matajiri,matajiri wa kitanzania ni kama Rostam,Mwenye Azam,Mengi na wengine kama hao....mabilionea wa Arusha hawaingii kwenye hii list.I think am correct.
 
Nikiangalia kwa kweli Tanzania ina matajiri walio na uwezo pengine kuizidi serikali ,kuna nchi moja jina kapuni ni ndogo tu ,ila nchi yenyewe ni tajiri na ina matajiri ,kiongozi mkuu siku moja machale yalimcheza na kuwaita matajiri wote ,ambao wana makampuni makubwa sana ,ya ujenzi na hata viwanda na mali zinginezo katika mkutano huo suali la kwanza aliwauliza kutokana na utajiri walionao ambao wameupata wakiwa ndani ya nchi wameifanyia nini nchi yao ,huku kiongozi huyo mkuu akiwa na data kamili za kila tajiri na pia akielewa kwa kina ni akina nani wanafanya juhudi za kujitolea kwa ajili ya nchi yao na hata wale wasiotoa nao pia alikwisha kuwa na taarifa nao.

Alipata majawabu mengi na yote hakusema kitu ila aliwambia wawe tayari kuisaidia nchi yao ,ikiwemo kujenga mabarabara mahospitali na mashule ikiwemo nyumba za ibada. Kwa kweli matajiri waliitikia wito na hata wale waliokuwa na ubakhili waliondoa ubakhili wao na kusaidia kwa kutoa michango na wengine kujengea nyumba sehemu zile ambazo wana asili nazo ,kwa mfano kijiji alichotoka kina nyumba hamsini mbovu mbovu zilizochoka na za zamani basi ,hujenga idadi ya nyumba hizo na kuwagaiwa wale wenye nyumba mbovu na zile nyumba mbovu hupigwa greda na sehemu hiyo huweza kujengwa shule au zahanati na misaada ikiendelea kwa aina hiyo kwa nchi nzima na maendeleo yalizidi kiasi kila mtu ana nyumba ya kisasa na sehemu bora za kufurahia watoto.

Je hapa tz matajiri tulionao wameifanyia kitu gani Tanzania ?




Hapa Tz Wanapigwa vita sana na wanasiasa.
 
Si wanalipa kodi? What else do you want from them?. Nchi ibuni vyanzo kutoka kwa wenyenacho kisheria harafu serikali iwe serious na ukusanyaji na matumizi mazuri.........
Usipende kuwa na mipango ya kuoneana huruma.
 
Wanatumia utajiri wao kwa kuiba raslimali za taifa,kukwepa kodi, na kuwanyonya watanzania wenzao kwa kuwalipa mishahara kiduchu katika makampuni yao...
 
hongera IPP naona mmesoma na kupita hapa JF ,nawapongeza sana kwa juhudi hizo kwani hayo ndio matajiri wanavyofanya kuinua na kusaidia nchi zao.


[h=2]ITV yamwaga madawati shule ya msingi Tandale[/h]



Joyce-Mhavile-September6-2014.jpg
kurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio One, Joyce Mhavile, (Kulia), akipeana mikono na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Tandale ya jijini Dar es Salaam, huku Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mussa Natti, (Kushoto), akishuhudia wakati wa hafla ya kukabidhi madawati jijini jana. Katika kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwa vyombo hivyo vya habari vinavyomilikiwa na IPP Media, ITV/Radio One imetoa madawati 260 yenye thamani ya Shilingi milioni 50.Picha: Khalfan Said

Kituo cha Televisheni cha ITV/ Redio One, kimetoa msaada wa madawati 260 kwa Shule ya Msingi Tandale, jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 20 ya kuanzishwa kwake.

Kituo hicho ambacho kilianzishwa mwaka 1994 pamoja na shughuli mbalimbali inazozifanya, kimejikita kwenye elimu na kuamua kutatua tatizo la madawati shuleni hapo baada ya wanafunzi wake kuripotiwa kukaa chini.

Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Joyce Mhavile, akizungumza kwenye hafla hiyo jana alisema lengo ni kuweka mazingira mazuri ya kujifunza na baadaye kuwa taifa la watu wanaojiamini.

Kuhusu maji ambayo ni moja ya changamoto zilizotajwa kuwapo shuleni hapo, Mhavile aliahidi katika mipango wanayoipanga wataliangalia na hilo.

Aidha, alisema mbali ya madawati hayo, kituo chake kimetoa soda, maji na biskuti kwa wanafunzi hao ikiwa ni sehemu ya maadhimisho hayo.
 
Back
Top Bottom