Tanzania ijifunze toka Tunisia; Wananchi wakizidiwa watawala hutimuliwa

Suala siyo chama cha replace,ila ni mabadiliko yatakayobadili hali hii mbaya ya maisha!


Lazima kuwe na sera na mikakati baada ya mabadiliko sio kuleta mabadiliko baade hakuna dira, mikakati na strategy kwa nza ya ku-replace maisha ya sasa
 
Wana JF nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana kile kilichokuwa kinajiri kwenye nchi ya jamaa zetu wa kule Kaskazini mwa Afrika yaani TUNISIA. Jina la TUNISIA linafanana kwa namna jina la Tanzania lilivokaa yaani TANZANIA. Zote zinaanza na "T" na kumalizia''A''
SIfamojawapo ya marais wa nchi zote mbili ni WAISLAMU.



Tunisia imekumbwa na mgogoro wa kisiasa ULIOSABABISHWA NA MAANDAMANO YA WANANCHI WAKILAMIMIKIA MAMBO MUHIMU YA MAISHA yakiwa ni pamoja na:
  1. Kupanda kwa gharama za Maisha.
  2. Ukosefu wa Ajira.
  3. Rushwa na Ufisadi uliokithiri mipaka.
Baada ya Wa-Tunisia kuanzisha maandamano kupinga hali hizo tatu muhimu,KAMA KAWAIDA YA UTAWALA DHALIMU POLISI WALIANZA KUZUIA MAANDAMANO KWA NGUVU IKIWEMO KUTUMIA RISASI ZA MOTO iliyopelekea watu karibia 200 kupoteza maisha.

Baada ya mauaji Rais ZINE el BEN aliamua kumfukuza kazi Waziri wa Mambo ya ndani. Bado haikusaidia kitu maandamano yakawa yako palepale,Rais akaamua kulihutubia Taifa kwa njia ya TV akiahidi kupunguza gharama za vitu na kuongeza ajira,bado Watunisia hawakumwelewa. Jana Ijumaa 15/01/2011 Zine Ben Ali AKAAMUA KUMWAGA MANYANGA, NCHI IMEMSHINDA NA HAITWALIKI.

Rais huyu ameitawala Tunisia kwa zaidi ya miongo 2(23 years). Jana amekimbia nchi maana imemshinda. Huyu Rais ana tuhumiwa kuwa MARA TU BAADA YA KUINGIA MADARAKANI ALIANZISHA SERA YA UGENISHAJI(UBINAFSISHAJI) na akaanza kuyauza Mkampuni na Mashirika ya Umma kwa kasi ya ajabu HUKU YEYE MWENYEWE AKIMTUMIA MKEWE KUJINUFAISHA NA UGENISHAJI HUO.

LESSON: Haya matukio ya Tunisia yana shabihiana kabisa na KILE KINACHOENDELEA HAPA kwetu Tanzania. Kwamba Watawala wetu hawa CCM wanatakiwa haya Matukio ya Tunisia wayachukulie kwa umakini mkubwa. Kwani kilichotokea TUNISIA CHAWEZA PIA KIKATOKEA HAPA TZ KIRAHISI KABISA NA CCM WAKAMWAGA MANYANGA.

Hali zote zilizosababisha Rais wa Tunisia hata hapa TANZANIA zipo na ziko wazi kabisa. Kwa hiyo ni swala la muda tu. MUDA UTAKAPOFIKA POLISI WATAFANYA MADUDU YAO KAMA WALIVOFANYA ARUSHA. HAPO NDIPO NCHI NZIMA ITAKAPOWAKA MOTO. Hakuna kifaru wala RISASI itazuia UMMA UKIAMUA KUING'OA SERIKALI KWA MAANDAMANO.

Kwa hiyo CCM kaeni mkao wa kula. Vuguvugu limeshaanza. Kikwete get prepared for the IKULU EXIT unless you change the situation.



Hali ya Ufisadi bado inazidi kuitesa na kuinyanyasa CCM na serikali yake. Huo ndiyo ukweli.
  1. SERIKALI YA CCM TAYARI MMESHAUA HUKO ARUSHA.
  2. PESA YA KUILIPA DOWANS(RICHMOND) INATAYARISHWA.
  3. EWURA TAYARI WAMESHAPANDISHA UMEME BAADA YA KUWAPA BARAKA ZAKO.
  4. PETROL/DIESEL IMEKUWA IKIPANDA KILA SIKU.
  5. THAMANI YA SHILINGI INAZIDI KUPOROMOKA NA HUJACHUKUA HATUA YOYOTE.
  6. MIGOMO VYUO VIKUU IMEANZA KUTIKISA NCHI UDOM,UDSM na kwingineko.
Hizi zote ni dalili mbaya sana kwa serikali iliyoko mamlakani. Kwa hiyo nasema CCM get prepared,the time is nigh! SOMO LIMESHATOLEWA NA WANANCHI WA TUNISIA. Who will be next??

Umejitahidi kuandika ila nilipo bold ni sawa ni kama vile umejenga nyumba nzuri sana halau ukachukua kinyesi na kuipaka kwa kuwa tu umekosa rangi inayofanana na kinyesi madukani ambayo ulikuwa unaitaka.

Tanzania a'int Tunisia and what happened in Tunisia will never happen in Tanzania in our lives time. We Tanzanians had been socialised to live in hardship and accept that hardship which make us directing our hardships to god (whom we cannot rally against) intead of policians.

By the way watch out they'll call you hate monger and violence incitor
 
Lazima kuwe na sera na mikakati baada ya mabadiliko sio kuleta mabadiliko baade hakuna dira, mikakati na strategy kwa nza ya ku-replace maisha ya sasa

kama Serikali hii iliyopo itasalimu amri, basi itakuja take-care gvt, mpaka pale katiba mpya na miundo mipya in place...pengine tutapata GNU.
kwa sasa replacement ni CUF na CHADEMA...Lakini tunaweza kuunda gvt ya technokrats, ifanye kazi kwa mwaka au 2 kureform system iliyopo, kwani hii ya leo inaonekana ina-fail, mkuu!
 
Kama ccm na aina ya viongozi wake kama makamba wametawala, ni dhahiri CDM wanaweza kufanya vizuri zaidi.What so special na ccm mpaka mtoa maada aone hakuna chama mbadala? Ni hayo madudu ya dowans na hizo tabu za maisha?Problem with most of Tanzanians are very cheap! Can be simply bought by cheap ccm propagandas like CDM ni chama cha kikristo! Enyi watanzania ni nani aliyewaroga hata msizione shida na dhuluma mnazofanyiwa na wachache miongoni mwenu? Hivi suala la wachache kunufaika na wengi kutomudu hata mlo wa siku moja kuna suala la udini hapo? Kiongozi kuwa mkristo au muislamu inakusaidia nini wewe binafsi kimaisha? Kama tumefikia hatua ya kushindwa hata kujua kwamba hizi ni propagandas za kijinga za ccm na wachache wanafaidika kiuchumi basi tunahitaji wawekezaji wa mawazo kwani tuna upungufu mkubwa katika kufikiri!
 
Tanzania a'int Tunisia and what happened in Tunisia will never happen in Tanzania in our lives time. We Tanzanians had been socialised to live in hardship and accept that hardship which make us directing our hardships to god (whom we cannot rally against) intead of policians.

By the way watch out they'll call you hate monger and violence incitor[/QUOTE]


I'm not sure whether you have considered the act of man and human acts when one is affected by frustrating factors. No society is hostile and violent by nature. If the political system goes on frustrating people there will come a time when the people you thiink have been socialised and tamed to accept hardships will say "enough is enough". Remember all the fights against oppressions in the world (slavery, racism ...) didn't start right from the beginning; it is only when people couldn't bear it any more that there was a revolt. Where the present system is taking us, if there is no immediate change, not long from now Tanzania will no longer be the long known "kisiwa cha amani". Conditions for peace are getting less and less and most of our leaders are working for their bellies at the expence of suffering and frustrated people. You will be still alive to see Tanzanians change from lambs we are today to hyenas claiming our share of the kill. This day has come.
 
Hivi mnajua kilichotokea Tunisia au mnapiga makelele tu nasie twataka ? Yaani hiyo habari yote hapo juu itawauza kwa bei rahisi kabisa maana hakuna cha kweli kilichoandikwa na ambacho kiliwasha moto wa mabadiliko ya Tunisia na kilichotokea.

Ndugu zanguni kilichojiri Tunisia ambacho hakikuelezwa hapo ni kisa kidogo sana na ambacho hapa kwetu imekuwa ni tukio la kawaida,kama umewahi kusikia hawa jamaa zetu wamachinga wauzao bidhaa zao bila ya kuwa kibali au sehemu maalum ya kufanyia biashala zao,mgambo au asikari wa tunisia walimwagia jamaa mbogamboga zake zikiwemo nyanya na bidhaa zingine wakimtuhumu kuwa akiuza bila ya kibali (machinga kwa hapa kwetu) ,jamaa alichezea kisago kitakatifu cha mgambo hao ila baada ya kumaliza ,jamaa alijiwasha moto na kufariki ,hapo ndipo cheche zilipoanza na habari zake kuenea kama moto wa nyasi huku zikiwapandisha wananchi mori wa kuisakama serikali na hadi hapa tulipofikia raisi ameshakimbia nchi na jamaa wanasema haitoshi wale waliomzunguka wote nao waondoke. Mnayaweza ? Hivi Kikwete aliwafukuza watu huko vijijini si mliwapokea kwa zulia jekundu au si kweli ? Wacheni longolongo zenu.
ndio tusiowataka nyinyi na mitazamo yenu kwani nani hajui kimetokea nini tunisia
 
wana JF na watanzania kwa ujumla nina wazo ambalo naweza kusema kuwa tuatakuwa tumetatua matatizo mengi sana katika nchi yetu hii.

Mimi binafsi nimependa sana walichofanya watunisia ..... Hivi sisi hatuwezi fanya kitu kinachofanana na hicho? Maana Nchi hii siielewi kabisa kama vile hakuna Raisi au Waziri wa mambo ya ndani.
Mambo yanafanykia kienyeji sana kila mtu anatoa tamko wenye nchi wamekaa kimya sasa hii nchi au jalala?????

Hebu tuone mbinu waliyo tumia watunis nasi tu transfer hiyo mbinu jamani.

Sijawahi kuona utawala wa hovyoo kama utwala wa awamu hii ya mwisho ya JK naona mpaka ipite miaka miwili hivi tweweza fanya waliyo fanya watunis.

Tafakarini wana JF na WaTZ wote.

Nawasilisha ni mawazo tuuuuuu.....
 
haitawezekana kwa sababu hizi
-watanzania wengi ni mafisi[waoga]wa kutupwa
-wengi wetu ni waoga wa virungu na bunduki
-wengi tuna UMIMI ,utasikia[nikaandamane badala ya kutafuta fedha familia yangu ile au niumie mimi wale kuku wengine, mashuleni na vyuoni wengi huandamana kw kulazimishwa hasa kuchelea kipondo.]
-hatuna umoja kwenye maswala yahusuyo utaifa[ tumebaki kuwa wazungumzaji wazuri sana]
-intelijensia unit [usalama wa taifa] wametapakaa kila kona,yawezekana akawa mkeo au ndugu wa karibu,watu wa dizaini hii shule za boarding tuliwaita MAYUDA.
-hatuwazi ya kesho tukifanikiwa kupata leo.
-samahani kwa hii sentensi,ILA WENGI WETU NI KAMA WATOTO WA KIKE,TUKIPEWA AHADI NZURI ZA UONGO TWARIDHIKA NA KULALA PONO.
-Wamesha tugawa kwenye makundi ya umaskini, ukwasi na udini.kwa hiyo kuungana pamoja kama tunisia inakuwa ngumu kwani maskini yupo juani kila siku kutafuta mkate wake wa kila siku,mkwasi anaogopa maandamano kulinda mali zake na wadini kila siku kulumbana

LABDA VYAMA VYA UPINZANI VIANZE KAZI YA KUONDOA HAYO MATABAKA KWA KUPANDIKIZA MBEGU YA URAIA NA MAPINDUZI MTAA KWA MTAA
 
Inatakiwa MTU MMOJA ajichome na moto hadi afe ndio tuanza vurugu kama tunisia. Me sipo tayari.
 
Matatizo ya Tunisia unayajua vizuri lakini? Kabla ya Tunisia walisema ifanyike kama Kenya, then kama Ivory Coast... na sasa Tunisia!
 
Matatizo ya Tunisia unayajua vizuri lakini? Kabla ya Tunisia walisema ifanyike kama Kenya, then kama Ivory Coast... na sasa Tunisia!
Matatizo ya Kenya Ivory Cost Tunisia Zimbabwe you name it........yote yanafanana ni udikteta, viongozi wengi hawapendi kuachia madaraka akiwemo Kikwete.
 
wana JF na watanzania kwa ujumla nina wazo ambalo naweza kusema kuwa tuatakuwa tumetatua matatizo mengi sana katika nchi yetu hii.

Mimi binafsi nimependa sana walichofanya watunisia ..... Hivi sisi hatuwezi fanya kitu kinachofanana na hicho? Maana Nchi hii siielewi kabisa kama vile hakuna Raisi au Waziri wa mambo ya ndani.
Mambo yanafanykia kienyeji sana kila mtu anatoa tamko wenye nchi wamekaa kimya sasa hii nchi au jalala?????

Hebu tuone mbinu waliyo tumia watunis nasi tu transfer hiyo mbinu jamani.

Sijawahi kuona utawala wa hovyoo kama utwala wa awamu hii ya mwisho ya JK naona mpaka ipite miaka miwili hivi tweweza fanya waliyo fanya watunis.

Tafakarini wana JF na WaTZ wote.

Nawasilisha ni mawazo tuuuuuu.....

Tunisia, msomi mmoja aliemaliza masomo yake Chuo kikuu baada ya kukosa ajira, aliamua kufanya biashara za machinga na Askari wa jiji la Tunisia kumsumbua kila mara na mwisho Askari waliharibu mali yake, hivyo kijana huyo kuchukua hatua ya kujichoma moto na kupoteza maisha yake! ndipo nchi ikalipuka kama ulivyosikia!

Hivyo kama unataka ya Tunisia yatokee hapa kwetu, basi nakushauri nenda pale Jijini Dar na ujichome moto mpaka ufe kama yule shujaa wa Tunisia halafu kazi iliyobakia tuachie sisi uone jinsi tutakavyompeleka JK puta!

Hiyo ndio mbinu iliyotumika Tunisia!
 
Back
Top Bottom