Tanzania haitasalimika! Kenya yatumika na Magharibi kuishambulia Alshabaab!

Haiingii akilini kwamba Kenya wanaweza kuingia kwenye vita leo hii? Sidhani kuna any push factor to this extent mpaka wanaamua hivi! Na sidhani kama wana uchumi mzuri kiasi hicho wa kuafanya waende vitani leo hii! Nadhani huu ni mkakati mpya ambapo hata Tanzania inaweza kutumika siku moja. Imeonekana kuwa ni gharama sana kutumia vifaa vya kivita kutoka Ufaransa au Markani au kuleta wanajeshi Obvious, ni gharama kisiasa kwa mataifa haya na ni gharama hata kimahusiano maana tayari wanashutumiwa kwa mambo wanayoyafanya huko Libya na kwingineko. Sasa njia pekee ni kuwatumia majirani, kwa mkataba maalum.

Nikiangalia Historia ya Kenya na Somalia, bado hainiingii akilini kabisa. Na usisahau hao Al-Shabaab wakati mwingine wamekuwa wakiishi ndani ya Kenya na wakipanga mipango yao kutokea Kenya na hata baadhi ya Suply (bidhaa za matumizi) hupitia huko muhimu zaidi Mirungi (miraa) kutoka Kenya!

You may be interested on this link: allAfrica.com: Kenya: America Bans Kenyan Linked to Al-Shabaab

possible kabisa mkuu, maana hawa wamarekani wamekuwa vinara wa vita. Na most times wanapigana mbali na kwao hivyo miundombinu na wananchi wao hawadhuriki kamwe except wanajeshi. Wamejenga kambi za kijeshi all over prime areas ili waweze kudictate... Kwa uono wangu nahisi Afrika mashariki tumeingiliwa kwa janja hii. Soon watajenga kambi kwenye eneo hili ili watumalize kwani eneo halitakalika... Eeh Mungu tunusuru na fitna hii. Amin
 
USA wenyewe waliingia Somali mwaka 1992 na askari zaidi ya 30,000 chini ya Rais Bush Sr. Baada ya muda wa miaka miwili askari hao waliondolewa na Rais Clinton baada ya askari wao wengi kuuliwa [angalia film Black Hawk wakati maiti za askari wao - elite US Army Rangers - zikiburuzwa katika barabara za Mogadishu na Wasomali waliovaa shuka na malapa]. Issue sio how well equiped an army is. Ninachosema mimi ni kuwa it is wrong to compare the Kenya situation now with Tanzania's situation in 1978. Kenya wana every right to take action but kama alivyowaonya Kofi Annan juzi they have to be very careful! Somalia like Afghanistan over the past 100 years has been and will continue to be a hard nut to crack. If the Kenya Army fails in Somalia the repercussions may be even more serious for its Government and this will certainly affect Tanzania.
 
Hivi huyu anayejiita profesa mleta hoja ni al Shabaab nini maana naona anaongea ki-al Shabab al Shabaab?
 
Umaskini wa mawazo ni tatizo au ugonjwa kubwa sana kwa Mwafrika,naomba Mungu atusaidie waafrika wa Tanzania kuzaa watoto ambao kwa kiwango fulani kwenye maisha yao ya hapa duniani, wawe na uwezo wa kutengeneza predictions kupitia taaluma zao kwenye maisha yao na kupata majibu [solutions] bila kuonekana nyuma ya mafanikio yao au misuko suko yao ya kukabiliana na maisha yao basi mafanikilo yao hayo yametokana na Wazungu.

Kwanini kila jambo ni lazima kuwe na tusi kuwa Mmarekani yuko nyuma yake.Aibu hii ya kuwakuza wamarekani kwa kila jambo kuwa mkono wao hupo itaishi lini,Hivi wakenya kwani hawawezi kupambana na Al-shabaab bila kutumwa au kusaidiwa na Mmarekani na Maswaiba wake.

Wakenya wanategemea utalii kandoni kandoni mwa pwani, hivi kweli mjinga mmoja toka uko alikotoka anakuja kufanya yake kwenye ardhi ya wakenya kisha wakenya maisha ya watu wake yanayotegemea utalii yaathirike na haiba yake kimataifa ionekane mbovu kuwa si sehemu sahihi kwa usalama kisa Al-shabaab ni waafrika huo n uchafu mbaya sana sana.

Hatuitaji kikundi cha Al-shabaab na mwenendo mzima wa maisha ya Wasomali huko kwao ambayo yametapakaa na hata hapa kwetu tayari tulishaumizwa na tunaendelea kuumizwa na A-shabaab lakini watawala wetu kwa kutokupenda kuonekana kuwa wako tofauti na waafrika wameuchuna mpaka wenye uthubutu waamue [guts] ndio nasi kuja kuwa tunaibuka kuwa tunasupport kwa kuiga badala ya kuanzisha kama viongozi wa kupambana na yale yanayopingana na maslahi ya wengi.Enzi ya Mwalimu Watanzania walikuwa FRONT LINERS LEO HII WATANZANIA NI BACK BENCHERS, wa yale yote mambo ya msingi ya binadamu.Ndio tuliipokosea siku hizi kwenye siasa zetu za kimataifa

Leo hii watanzania wamekubali Wasomali toka somalia kuja kufungua biashara zao hapa Dar es Salaam na mikoa mingine pembezoni mwa bahari .Hata kenya walianza hivyo hivyo kuwakumbatia wasomali lakini malipo yake ndio hao ya kudololesha maisha na uchumi wa Kenya hivyo anaefuata kwa athali za Wasomali wa Al-shabaab ni Tanzania, Zanzibar.

Ukitaka kujua Athari za Al-shabaab waulize Watanzania akiwemo mwanachuo binti wa kike aliyetekwa na Vikundi vya Al-shabaab, na kuishi nao miezi sita wakiyumbishwa kwenye bahari miezi sita [6] hakika ukivaa kiatu cha raia hao wa Tanzania Uwezi kushabikia upumbavu na ushenzi wa wahuni hao. Kwa taarifa hiyo binti yetu huyo almanusra kubakwa na mmoja wa hao wahuni,isingekuwa busara yake leo hii,angeibuka na mimba ya kutuletea Mtanzania mwingine zao la uthalimu wa Al-shabaab pasipo hiari ya Binti huyo.

Zamani maslahi ya Mtanzania mmoja mmoja mpaka kuunda kundi, makundi na hatimae Taifa yalikuwa na thamani kubwa sana.Lakini leo Mtanzania anawezwa kutekwa lakini bidii za Serikali yetu kumuangaika Mtanzania kupitia haki yake ya Katiba imekuwa ni hadithi za vitabuni.
 
Kwa namna yoyote ile wanayoyafanya Al Shaaban hayapendezi na hayavumiliki kabisa. Kenya kama nchi nyingine wanachallenge kubwa ya uamuzi gani wachukue dhidi ya magaidi hawa. Choice ya nini wafanye ndio changamoto waliyonayo.

Kwangu mimi, mathalan, njia ya kupigana na hawa jamaa naiona ina ugumu wake. Tukumbuke kuwa wasomali wapo sehemu nyingi sana East Afrika, wengi wakiwa ni wafanyabiashara wakubwa with so much wealth. Hawa wanaweza kusaidia kusupport war ndani ya nchi ya Kenya. Wanaweza kutumia pesa kufinance terrorism kwa kutumia vijana wa kisomali ndani ya Kenya.

Naweza kuamini pia kuwa while jeshi la kenya limeenda somalia kuwage war kuna adui (Al Shabab) ambao wameachwa Kenya na wanaweza kufanya lolote kwani wanaijua Kenya vizuri sana. Kifupi ni kuwa Kenya wanapambana na adui aliyepo ndani ya nchi yake, wanaweza wakaua watu wengi sana Kenya na kuharibu infrastructure na hivyo kuifanya vita iwe ni ya adui wa ndani na wa nje.

This to me is my biggest worry. Mie nilikuwa nadhani US wangerudi tena kuwapiga hawa jamaa kwa kutumia high tech weapons na kudestroy their millitia strength while Kenya na East Africans waonekane kama hawahusiki kuliko hivi ambavyo tumeamua kuingia front wakati tuna adui pia ndani ya mipaka yetu.

Kingine ni kuwa kuna baadhi ya hawa wasomali ambao wapo mpaka kwenye decision making levels katika nchi zetu hizi, je tuna uhakika gani kuwa siri zetu hazivuji kwa hawa jamaa. Again i am gutted by evils committed by Al Shabab ila how to stop them needs a lot more of thinking.

I am just thinking aloud.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom