Tanzania: Dua ya Kuliombea Bunge...

Napata shaka kama WAbunge walio wengi wanamcha Mungu, maana kwa dua hiyo ni nzito sana tusingetegemea tunaona wanafiki ndani ya bunge wanaopindisha ukweli kwa kuunga hoja hata zisizostahili mia kwa mia
 
Bubu Msemahovyo,haujajua kwamba kuna Wakristu na Waislamu majina tu?Ndani mwao Mungu hayupo na hiyo sala wanaisema kwa mdomo tu lakini moyoni hakuna kitu.
 
....''tukitaja majina ya wauza sembe hakuna MBUNGE atakaye pona'' Lukuvi.

Hayo maombi na ayapokee SHETANI.
 
Kuna haja Dua ziongozwe na Kasisi mmoja kuwakilisha Wakristo na Imam mmoja kuwakilisha Waislam wakisha maliza wanatoka nje ya Bunge na wabunge kuendelea na kazi yao. Hii itawafanya wawe na adabu kuheshimu uwepo wa Mwenyezi Mungu hapo Bungeni.

Nasema watashika adabu kwa sababu sasa hivi hakuna hiyo kitu kwani huyu anayejifanya kuongoza dua jana alikuwa nje ya maadili leo wanamuona akiongoza dua ndani ya bunge hawawezi kutilia maanani uzito wa dua na kikao cha bunge lenyewe, tufanye mabadiliko hayo ili kutenganisha dini na siasa kwa vitendo.
 
Kuna haja Dua ziongozwe na Kasisi mmoja kuwakilisha Wakristo na Imam mmoja kuwakilisha Waislam wakisha maliza wanatoka nje ya Bunge na wabunge kuendelea na kazi yao. Hii itawafanya wawe na adabu kuheshimu uwepo wa Mwenyezi Mungu hapo Bungeni.

Nasema watashika adabu kwa sababu sasa hivi hakuna hiyo kitu kwani huyu anayejifanya kuongoza dua jana alikuwa nje ya maadili leo wanamuona akiongoza dua ndani ya bunge hawawezi kutilia maanani uzito wa dua na kikao cha bunge lenyewe, tufanye mabadiliko hayo ili kutenganisha dini na siasa kwa vitendo.

Mkuu, je mabunge yote duniani huwa na dua kama hizi kabla ya vikao au ni Tanzania tu?
 
Kuna uhusiano wowote wa dua katika kuombea bunge la katiba na yale matendo ambayo yanafanywa na wajumbe wa katiba hasa ukizingatia manung'uniko mengi yamekuwa yakitolewa na wananch juu ya uwezekano wa baadh ya wajumbe kuchakachua katiba ambayo kiukweli ni maoni ya wananchi wa jamhuri ya muungano wa tz.

Je kunaweza kukawa na athari kubwa kwa maana kwamba ni kumdhihaki mwenyezi Mungu?

=======

Nimeiona hii kwenye gazeti la Mwanachi la leo linalohusu 'Dua ya kuombea Bunge inayosomwa kama kasuku.

Dua hii inasema kama hivi:

Ewe Mwenyezi Mungu Mtukufu,Muumba wa Mbingu na Dunia,umeweka katika dunia Serikali za Wanadamu na Mabunge ya Mataifa ili haki ya itendeke.Twakuomba uibariki nchi yetu idumishe uhuru,umoja.haki na amani,umjalie rais wetu hekima,afya njema,na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri,wadumishe utawala bora.Utuongezee hekima na busara sisi wabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na utupe uwezo wa jujadili kwa dhati mambo yatakayoletwa mbele yetu leo,ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na utsawi wa nchi yetu.Amina"

Kwenye sala/dua hii ni nzuri siwezi kukataa wala kupinga,lakini nina maswali kadhaa kuhusu hili:

1.Je Bunge letu linaitendea haki sala au dua hii.
2.Kwanini dua hii isisomwe na wabunge wote ili kila mmoja aweze kuifanyia tafakuri ya kina pale anapoomba au kusali dua/sala hii asubuhi wafunguapo Bunge.
3.Na kwanini sala/dua hii husomwa kwa haraka sana kama vile kuna muda unapotea,yaani kwanini dua hii sifanywe kwa tafakuri ya kina pale inaposaliwa?

Inawezekana hoja hii ilishawahi kuletwa hapa na sikuiona basi naomba mnisamehe,ila ningependa tuitafakari dua hii na kuiomba serikali yetu au Bunge letu liichulie DUA hii kwa moyo na kila mtu ndani ya Bunge awe anaisoma na kuitafakari,ninadhani itabadilisha dhana nzima ya uchangiaji usiona tija,uchangiaji wa mipasho na matusi kwa wabunge wa pande zote mbili.

Karibuni nyote tuijadili.
 
nadhan ndo mana umaskini umekithiri ktk nchi,kikubwa ni kuomba mwenyez mungu kufukuza pepo mchafu anaenyemelea kuingiza mambo ambayo ni kwa ajili ya kunufaisha kikundi cha watu hasa ccm.
 
Kweli hakuna mantiki maana kuna hawa akina UKAWA walipanga kumzomea Rais wetu!
 
kuna uhusiano wowote wa dua ktk kuombea bunge la katiba na yale matendo ambayo yanafanywa na wajumbewa katiba hasa ukizingatia manung'uniko mengi yamekuwa yakitolewa na wananch juu ya uwezekano wa baadh ya wajumbe kuchakachua katiba ambayo kiukweli ni maoni ya wananchi wa jamhuri ya muungano wa tz.je kunaweza kukawa na athari kubwa kwa maana kwamba ni kumdhihaki mwenyezi mungu?
Hapo ushatoa jibu sio swali tena mdau.Hizo dua wanazoanza nazo ipo siku sitawarudia wao wapige meza wee tutajua mwisho wao tuu.
 
Mungu hana upendeleo kwa mtu yeyote na pia Mwenyezi Mungu hachoki kusamehe dhambi zetu ndio maana hamna mtu mkamilifu hapa duniani, kama dhambi kila moja ana dhambi.
 
Mungu hana upendeleo kwa mtu yeyote na pia Mwenyezi Mungu hachoki kusamehe dhambi zetu ndio maana hamna mtu mkamilifu hapa duniani, kama dhambi kila moja ana dhambi.

kweli ni sawa lakini wanasema samehe saba mara sabini,hawa ccm toka waanze kuwakosea wananch haijafika tu ukomo wa kusamehe?
 
kuna uhusiano wowote wa dua ktk kuombea bunge la katiba na yale matendo ambayo yanafanywa na wajumbewa katiba hasa ukizingatia manung'uniko mengi yamekuwa yakitolewa na wananch juu ya uwezekano wa baadh ya wajumbe kuchakachua katiba ambayo kiukweli ni maoni ya wananchi wa jamhuri ya muungano wa tz.je kunaweza kukawa na athari kubwa kwa maana kwamba ni kumdhihaki mwenyezi mungu?
dua ni nzuri ila anaeisoma dua hiyo si mtu mwema
 
kuna uhusiano wowote wa dua ktk kuombea bunge la katiba na yale matendo ambayo yanafanywa na wajumbewa katiba hasa ukizingatia manung'uniko mengi yamekuwa yakitolewa na wananch juu ya uwezekano wa baadh ya wajumbe kuchakachua katiba ambayo kiukweli ni maoni ya wananchi wa jamhuri ya muungano wa tz.je kunaweza kukawa na athari kubwa kwa maana kwamba ni kumdhihaki mwenyezi mungu?

Kama ulisoma ule waraka wa kakobe ndo matokeo ya haya tunayoyaona Leo.watu walipuuza ule waraka sasa kinachotokea ni matokeo.
 
Najua Wengi Mtanibeza Na Kusema Sina Hofu Ya Mungu Lakini Kiukweli Na Kiuhalisia Bado Sijaona Umuhimu Wa Kuliombea Bunge Kwa Sababu Zifuatazo:

1.Haki Inaonekana Waziwazi Kukandamizwa Na Viongozi Hasa Kwa Upande Wa Upinzani, Spika Akiwa Kama Kiongozi Anafanya Hili.

2. Bado Matusi Na Mizaha Imekuwa Fashion Bungeni, Hii Ina Maanisha Wabunge Wetu Licha Ya Kuomba Dua Kwa Mungu Bado Hawana Hofu Ya Mungu.

3.Vitisho Dhidi Ya Wabunge Wanaotetea Maslahi Ya Wananchi Bungeni Bado Vinashika Kasi Kubwa Kila Kukicha.


Wakuu Kwa Sababu Hizi Sioni Kama Kuna Haja Ya Kufanya Unafiki Wa Kumuomba Mungu Atangulie Katika Shughuli Za Bunge Ilhali Bado Watu Wanafanya Kinyume Na Maagizo Ya Mungu.
 
Back
Top Bottom