Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wadau, kwa taarifa tu, leo asubuhi kutokana na udhuru nyumbani nilichelewa kwenda kazini hadi saa 6 hivi mchana. Nilipotoka nikakumbuka magazeti, nikasema nitanunua Kariakoo. Nilishangaa sana kuanzia Congo Street hadi Mnazi MMoja gazeti la Tanzania Daima sikulipata, kila muuzaji asema ameishiwa.
Hatimaye nilikuja kulipata Jamhuri Street karibu na NBC. Wauzaji waliniambia siku hizi gazeti hilo huisha mapema sana na baadhi yao wanashangaa kwa nini wamiliki hawachapishi nakala nyingi.
Hatimaye nilikuja kulipata Jamhuri Street karibu na NBC. Wauzaji waliniambia siku hizi gazeti hilo huisha mapema sana na baadhi yao wanashangaa kwa nini wamiliki hawachapishi nakala nyingi.